Search results

  1. Beauty Eva

    Umem-miss nani?

    Ni rafiki uako yupi hujui alieda wapi na huwa unam-miss sana na unatamani itokee siku mkutane tena? Mtaje labda na yeye yupo humu na atakusikia[emoji7] Mimi naanza na Fatma Ahmed Tamim, nilisoma nae Jamhuri High School Dodoma na alikuwa anaishi Area C
  2. Beauty Eva

    TAKUKURU Arusha ni kambi ya mateso

    Ni miongoni mwa taasisi chache sana nchini Tanzania zilizokuwa zimebaki na heshima na mtu alijiona salama sana akiitwa katika ofisi za chombo hiki. Kwa sasa hali imebadilika. Mheshimiwa Sirro, tupia macho yako hapo. Mheshimiwa Mkurugenzi Mkuu Wa TAKUKURU ndugu Mbung'o tupia macho yako hapo...
  3. Beauty Eva

    Niondokee na mkono wako wa sweta

    Ptuuuuu!! Wanaume (sio wote) muwe na japo akiba kidogo ya aibu. Unatumia nguvu nyiiingi kumshawishi mwanamke. Unakubaliwa. Mnaenda hoteli, unalipia na unaagiza vinywaji. Muda wa kujigijigi unafika, unavua nguo zako.. kumbe mkono wa sweta. Looo, hunipati ng'ooooooo Kwendraaaaaaa
  4. Beauty Eva

    Baada ya kunikosa mimi sasa anamtaka dada yangu kimapenzi

    Habari zenu ndugu! Ushauri wenu ni muhimu sana Kuna mkaka mmoja mstaarabu sana kwa muonekano wake na hata katika mazungumzo yake. Kaka huyu tunatoka nae sehemu moja, ameoa na ana watoto. Shughuli zake anafanyia Arusha. Mkaka huyu siku za nyuma baada ya kugundua nipo chuoni alikuwa anakuja...
  5. Beauty Eva

    Wana chit chat, nimeipenda sana video clip hii.

    Huyu jamaa nimempenda sana. Full kigugumizi katika eneo la penati
  6. Beauty Eva

    Hivi ninyi wanaume, mmerogwa?

    Siku hizi kumekuwa na matangazo katika vyombo vya habari na hata mabango mtaani yamejaa ujumbe unaofanana. *Ujumbe unaojulisha umma kuwa kuna dawa za kurefusha na kunenepesha uume. Au Ujumbe unaojulisha kuwa, kuna dawa inayoweza kukufanya ukae kifuani kwa mwanamke kwa muda mrefu. Nani...
  7. Beauty Eva

    Ninaanzaje kukukubali?

    Kijana Shabab kabisa. Unapaka poda, unalegeza sauti na kuongea kama mwanamke. Mwili unaulegeza kama mwanamke. Outing unakula soseji moja na nusu glasi ya juisi, halafu unajitia huwezi kumaliza. Maongezi yako yote, ni kujisifia. Gari unaloendesha umeazima..Lol Mwanaume unatakiwa ujiamini. Ishi...
  8. Beauty Eva

    Nakutakieni mwaka mpya mwemaaaa (2018).

    Hello friends. Nakutakieni mwaka mpya (2018) mwema, na ninamuomba Mungu atufikishe salama. Nawapenda woooote ndugu zangu wa www.jamiiforums.com na hasa wana wa chit chat
  9. Beauty Eva

    Wanajf/MMU ninawatakia Sikukuu njema

    Wanajf/Wana-MMU.. Ninawatakia sikukuu njema ya Krismas na Mwaka mpya. Tusisahauliane kwa vyuku na vinywaji. Ninawapenda sana.
  10. Beauty Eva

    Wiki mbili zitanitosha kujua gari?

    Habari zenu ndugu zangu. Ninataka kujifunza kuendesha gari, haya magari madogo ya familia. Je, wiki mbili zitanitosha kujua kuendesha manual na automatic?
  11. Beauty Eva

    Hongera dada kwa kuhitimu na kupata shahada

    Japo Shahada ni kitu cha kawaida siku hizi, sina budi kukupa hongera na pongezi tele dada yangu mpenzi. HONGERA SANA. nisaidieni kumu-wish dada yetu.
  12. Beauty Eva

    Happy birthday dada yetu mpenzi

    Happy birthday dada yetu. Mungu akuzidishie furaha na heri nyingi katika maisha yako. Dada yetu, tunakupenda na tunakuthamini sana.
  13. Beauty Eva

    Nabaki na Ukatoliki wangu. Mchungaji ameniogopesha

    Mara moja moja huwa naenda kuabudu katika moja ya makanisa ya maombezi na uponyaji hapa Arusha. Sasa, mchungaji wa kanisa hili amekuwa akinitongoza kila mara anionapo na hata kwa simu. Mwanzo alikuwa akinipigia simu usiku kwa ajili ya maombezi, lakini baadae ikawa baada ya maombezi...
  14. Beauty Eva

    Wanamichezo (footballers) msaada wenu tafadhali

    Wapenzi wangu wanamichezo. Naombeni mnisaidie, maana kila siku nimekuwa nikijiuliza maswali haya matatu na majibu sipati. Maswali ni haya yafuatayo:- * Ni kwa nini unapopigwa mpira wa adhabu (faulo au penati), wachezaji wa timu mpira unapoelekea hushika sehemu zao za siri? * Je, kiongozi wa...
  15. Beauty Eva

    Safarini Dar: Msaada wa hoteli nzuri bei ya wastani

    Wana MMU, hasa wa Dar na Dom. Ninasafari ya Dar, Naombeni kujua hotel/lodge nzuri jirani na Stendi ya mabasi ya mikoani. Iwe ya bei ya wastani kama shilingi 20,000 hadi 30,000 kwa siku. Iwe jirani na chakula kinapopatikana na pia isiwe vichochoroni. Pia Lodge yenye sifa hizo hizo kwa Dodoma...
  16. Beauty Eva

    Hotel/Lodge Dar na Dom

    Ndugu zangu, msaada. Ninasafari ya D'salaam na Dodoma wiki ijayo. Ninaomba kujuzwa hotel/Lodge nzuri na za bei ya wastani isiyozidi shilingi 30,000. Mambo ya kuzingatia:- Iwe safi na yenye usalama. Iwe sehemu ya wazi (si ndani ndani sana ya mji). Ikiwa jirani na stendi ya mabasi ya kwenda...
  17. Beauty Eva

    Katika mapenzi, usithubutu kupekua historia/experience ya mwenzi wako

    Upo mapenzini na labda umemkuta mwenzi wako tayari akiwa mkubwa "si bikra". Katika hali hii usipende kupekua maisha ya kimapenzi aliyokuwa nayo awali. Anza pale mlipokutana ninyi. Kupekua pekua hakufai, maana unaweza kupewa ukweli ambao utakuumiza maisha yako yote. Mfano, wewe mwanaume...
  18. Beauty Eva

    Mapenzi yetu katika siasa yanatuondolea hata uwezo wa kufikiri

    Sisi Watanzania ni watu wa ajabu sana, hasa linapokuja suala la siasa. Mapenzi yetu katika siasa yanatuondolea hata uwezo wa kufikiri. Tazama jambo hili:- Majuzi, serikali ilizuia mikutano ya vyama vya siasa katika maeneo ambayo vyama hivyo havikushinda. Wapo watu wamefurahia sana jambo hilo...
  19. Beauty Eva

    Mapenzi ni Uhuru au utumwa?

    MMU! Ni utumwa au Uhuru? Ukiwa katika mapenzi, unakuwa hauna privacy. Muda wowote mpenzi wako anaweza akachukua simu yako na kuipekua. Wengine unakuta mpenzi wako anakuwa na passwords zako za akaunti zako za benki, na hata za mitandao ya kijamii. Kwa baadhi ya ndoa, kama mwanamke ni...
Back
Top Bottom