Kama jamaa ameweza kujiunganishia dizeli kwa muda bila vyombo vya ulinzi kushtuka ni hatari kwa usalama wetu na miundombinu ya taifa. Mbinu mpya za ulinzi na usalama zinahitajika ili mtu kama huyo akijaribu tu akamatwe kabla kutekelezwa.
Bunge linataka kujadili au kushauri nini kwenye hukumu wakati si jukumu lake? Waliofungua mashitaka ndio wa kudai hukumu kama wanataka kuchukua hatua zaidi. Vinginevyo tunaka kuingiza siasa kwenye muhimili wa Mahakama.
Hapa naona kuna taratibu au mkataba hauko vizuri. Tumeshamlipa 90% Mzabuni na kivuko hakifanyi kazi miaka 2 sasa kutokana na mapungufu. Nani anafidia huu upotevu na chombo chenyewe kinazidi kuharibika kutokana na mazingira ya bahari? Mbona hatuna taarifa ya kesi yoyote ya usuluhishi kuhusu hiki...
Wabongo tuliaminishwa kuwa masuala yote yanahusu utawala wa soka na matatizo yake hayapelekwi mahakamani na ukipeleka nchi inafungiwa. Kumbe ni kututisha sisi nchi changa. Mpingeni sasa huyu Mwendesha wa Marekani na kuifungia. Fifa imesambaratika kwa wiki moja tu.
Hii inaweza kutokana na mkataba mbovu uliopo. Mauzo ya kitu yanakamilika fedha ikishalipwa na kutekeleza kinachotakiwa kufanywa na pande zote. Kama hilo halifanyiki mkataba unavunjwa mnatafuta wabia wengine sio kusubiri miaka 14 bila hata kuwa na nia ya kuchukua hatua.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.