Nahitaji msaada wenu tafadhali, nimejaribu mara kadhaa ku install ir 2204 kwenye pc lakini ikifikia hatua ya kuunganisha waya, inakaa muda mrefu halafu inaandika imeshindwa kutambua devise niliyounganisha, nifanyeje???
Wakuu habarini za muda huu, nimehamia nyumba ambayo kuta zake zimepakwa rangi ya mafuta, bahati mbaya kuta ni nyeusi sana, either ni kutokana aliyekuwepo alikuwa anapikia ndani. Nimesafisha lakini ule uchafu hautoki.
Sasa nauliza je nawezaje kupaka rangi ya maji juu ya huu ukuta wenye rangi ya...
Habari wakuu,
Ninahitaji sana mkata wa Dawasa unaohusu huduma kwa mteja,nimejaribu kutafuta kwenye website yao lakini nimekuta kurasa kumi tu na nyingine hawaja ziweka.
Msaada tafadhali.
Wadau naomba kuelimishwa kuhusu moneymaker Pump. Je, ina uwezo wa kusukuma maji umbali gani? Ubora wake ukilinganisha na hizi pump za laki tatu za Kariakoo?
Naomba kujua na bei zake na wapi nitaipata kiurahisi kama nikiridhika kuwa ni bora zaidi.
Wakuu naomba kuuliza,nimebadilisha simu baada ya simu yangu ya awali kukataa kuwaka,hivyo nimefungua account ya whatsApp kwenye hii simu mpya kwa namba ile ile ya kwanza,changamoto ni kuwa nimepoteza magroup ya awali na kumbukumbu zake zote, swali!! je kunauwezekano wa kurejesha ma group...
habari za muda huu wakuu,nina printer aina ya HP Deskjet 2130All-in-One,nina print kazi zangu vizuri tu, ila ku scan document ile app kwenye desktop haifunguki kabisa,na hii imenitokea kwenye printer kadhaa za hp, lakini canon hainisumbui kabisa,naomba msaada tafadhali.
Wakuu nimeanzisha kilimo cha mipapai.
Nilitegemea nitumie mvua za masika ili kupunguza gharama za umwagiliaji, lakini kwa bahati mbaya mvua za mwaka huu si nyingi.
Nimepata wazo la kuwa na madumu ya maji yale ya kuuzia maji, lita 12(mfano uhai na masafi) kwamba nikiyapata hayo najaza maji na...
wakuu naomba msaada,nina laptop aina ya DELL Latitude e6400,kuna wakati inaonyesha vizuri ila kuna wakati mwanga unakuwa hafifu sana hata ni ngumu kuona kitu. Msaada tafadhali
Wakuu ninawazo la kufungua stationery eneo la gongo la Mboto DSM,japo Mmi ni mgeni kabisa, naomba kama kuna mzoefu na maeneo hayo,kuhusu bei za frem,je panalipa kwa biashara hiyo?na wazo jingine la kuboresha. Asante
Nina inverter aina ya Genus 800va, nimeambiwa inaweza kutumika kama back up sestem,kwamba Umeme unapokatika inajiwasha yenyewe. Betri ninazo ,shida ni namna ya kuunganisha,Mwenye ujuzi Tafadhali
Habari za muda huu, nimepatwa na tatizo na ninashindwa kulitatua, nilienda kwenye control Pannel na kufuta program zote za itunes kwa kuwa sizihitaji kwa sasa, lakini baada ya kufanya hivyo ninashangaa niplay audio au video yeyote haina sauti. Tafadhali naomba msaada wenu.
wakuu ninatumia umeme wa sola kwa ajili ya umeme wa nyumbani, kwakuwa panel zangu ni za volt 24, na inverter ni ya volt 12, huwa kila siku asubuhi nina charge betri kwa mfumo wa volt 24(nina betri mbili), na jioni tukirudi home,nina disconect solar pannel halafu ninaunganisha inverter kwa mfumo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.