Wengi waliobahatika kutoa maoni yao wameelekea kumlaumu hakimu Rwizile kwa kutumia neno Facebook fun badala ya Facebook fan. Binafsi natofautiana na watoa maoni wengi kwa mantiki kwamba nikiangalia uandishi mzima wa hakimu Rwizile nimefikia kuamini kuwa hilo neno la fun limeingia pale kimakosa...
Ukiangalia kihisia utakuta Lipumba hayuko sahihi. Lakini ukiangalia kisheria, utakuta Lipumba yuko sahihi kabisa. Sasa tufuate usahihi wa kihisia? au wa kisheria? Jibu ni fupi, wa kisheria. Mwanya ulioachwa na uongozi wa CUF umemruhusu Lipumba kufanya alilofanya. Hivi sasa wa kulaumiwa ni...
Kwa vile maelezo ya kisheria yapo wazi , ni vema kuyaunga mkono maamuzi ya msajili wa vyama. Hapa kosa haliko kwa msajili bali ni kwa hicho chombo cha CUF kilichopaswa kuifanyia kazi hima hima barua ya kujiuzuru ya Prof. Lipumba. Wao wakawa wanasua sua. Chelewa chelewa , utakuta mwana si wako...
Asante ndugu yangu. Ni kweli sijaongelea suala la kuzuiwa kwa mikutano kwani wanasheria wengi walishalijadiri hilo na pengine ndio maana tunaona hali ya kulegeza kamba inazidi kuchanua. Kwani hivi punde tumesikia polisi wakinena jambo jema katika suala hilo huku wakitoa sababu zinazolenga kuleta...
Ningeweza kutumia vifungu vingine vya sheria kwa nia ya kupingana na hoja za kisheria zilizotolewa katika maamuzi haya. Lakini kwa vile sina hoja kinzani na hoja hizo , nadhani sioni umuhimu wa kutoa hoja mbadala. Lakini kwa wewe ama yeyote anayepinga hoja za kisheria zilizopelekea maamuzi haya...
Nimefuatilia maoni ya baadhi ya wanajamii hapo juu. Nimegundua kuwa katika baadhi ya watoa maoni wanaingia katika tatizo kubwa sana la kutozijua sheria na namna ya kuzipinga hoja za kisheria kwa kutumia sheria zingine. Tatizo la walio wengi humu jamvini hawajipi muda wa kutosha katika kufuatilia...
Nimefunguka. Kumbe hii Makala itakuwa imeandikwa na Acacia mining. Huenda ni hao hao wana Acacia mining wamekuwa wakitumia mwanya wa kudanganya kwamba bidhaa zao zinapitiliza kwenda nchi jirani ili kukwepa kulipa kodi . Lakini wakishafika mahali fulani hugeuza njia na kuzipeleka kwenye maghala...
Kosa ni kosa halina rangi. Ikiwa ni watanzania wamekosea wachukuliwe kuwa watanzania waliokosea. Kitendo cha kuangalia rangi zao ama uasili wao ni kuingia katika kosa lile lile kama wao isipokuwa hili linakuwa ni kwa upande mwingine. Tuondokane na tabia ya kubagua watu bali tuangalie makosa ili...
Si tafsiri nzuri kubeba neno la lugha nyingine kama lilivyo na kuliegesha katika Kiswahili chetu. Kwa kiasi kikubwa linakosa maana na uzito kama ambavyo lingetumika neno lenye kulenga mazingira ya lugha yetu. Mathalani, neno "habari moto moto" au lolote lenye kushabihana na hilo lingeonesha...
Ama kwa hakika akili kila mtu ana zake. Hawa akina Mbowe ni juzi juzi tu walipokea mafisadi chamani . Je, walipeleka kwanza taarifa zile katika gazeti la serikali? ama kama si huko je, walikisusia CHADEMA kwa kupokea kikosi kile cha mafisadi? Hawana kitu cha maana hao jamaa. Walau kama fedha...
Ama kwa hakika akili kila mtu ana zake. Hawa akina Mbowe ni juzi juzi tu walipokea mafisadi chamani . Je, walipeleka kwanza taarifa zile katika gazeti la serikali? ama kama si huko je, walikisusia CHADEMA kwa kupokea kikosi kile cha mafisadi? Hawana kitu cha maana hao jamaa. Walau kama fedha...
Sioni kama kuna tatizo kumtuhumu mtu na kisha kuruhusu uchunguzi ufanyike dhidi ya mtuhumiwa na kisha kumpeleka mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake. Mara zote nimekuwa nikifuatilia nimegundua kuwa hayo yamekuwa yakifuatwa. Wanaoongelea udikteta sijui kama wanafahamu maana ya udikteta...
Mawazo ya Nyerere yanaelekea kutimia kwamba kuunda Taifa moja la Afrika lenye nguvu duniani kama nchi moja ni lazima tuanze na umoja wa kikanda . Kwame Nkrumah hakuona iwe hivyo , lakini ukweli wa ndoto ya Nyerere ndio unaojidhihirisha kadiri siku zinavyopita.
Tatizo la Gagnija ni mkabila. Hivyo yeye hajali mambo ya chama bali ni mambo ya ukabila. Hivyo siyo rahisi kumpanua kifikra na ndiyo maana anaishia matusi. Ni kuachana naye. Yeye amebaki na Mwakalinga wake hata kama hakuwa chaguo la kura za maoni ili mradi tu ni Mwakalinga. Ni kuishiwa fikra za...
Jamani achene kugombana . Hakuna anayeweza kuthibitisha kuwa yule ni Makonda ama si Makonda. Ile ni picha ya mtu tunayemwona akitutazama na yule mwingine hatuna hakikisho kama ni nani. Labda huyo mhusika Ridhawani tunayemwona kwa sura anaweza kutoa neon punde kuhusiana na hilo ili yote miipasho...
Jamani tusimshambulie yeye kama yeye bali tujikite katika hoja hizi zilizo mbele yetu kama ni za kweli ama la. Tukifanya hivyo tutaingia upuzi ule ule wa Jerry wa kumshambulia mwenzie bila kushughulikia agenda iliyokuwa mbele yake. Huo ni uvivu wa kufikiri
Heri huyu amefungua account ya fedha zake binafsi kuliko wale walioliibia taifa kwa ufisadi mkubwa. Katika hili mwacheni Mbowe aende zake anzeni na kurudisha kwanza yale mabilioni yaliyotoroshwa nje kifisadi. Kama hiyo BOT ina meno mbona imekaa kimya kusema kitu hata baada ya ile orodha ya walio...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.