Naomba watakapokujibu waunganishie na mimi majibu ya suala linalonitatiza . HIVI INAKUAJE UNAKATA LESENI YA BIASHARA KISHA UNAANZA BIASHARA NA MWAKA UNAOFUATA UNAKATA TENA LESENI YA BIASHARA ILE ILE NA MALIPO TENA ? Je , nayo hii inaitwa kodi ?
Wizi huu sio mpya . Ushafanyika sana kwenye pub hapa mjini . Ni kweli pale Mlimani city matapel wanajazana sana bar hasa samakisamaki . Naomba management ya pale wawe macho . Niliwahi kutoka pale nikafuatwa na mmojawapo katika kundi lililokaa bar hiyo akataka kunizoea nikamtukana sana .
Mimi nilikua mpenzi wa kuangalia bongo movie mpaka DVD zao nilinunua sana . Lakini sasa nimeacha baada ya kuona movie moja bibie kaudhiwa na mpenzi wake akaamua kujiua . Alikwenda moja kwa moja dukani akanunua sumu ya panya , baada ya kutoa fedha na kupewa sumu hiyo , akasubiri chenchi !
Lazima ulipe . Maana Serikali ndio iliyokupa mtaji wa kuanzisha biashara yako . Ikakuongoza , ikakuonyesha frem ya duka lako . Ikakupa dalali wa kukuonyesha mwenye nyumba , ikakulipia gharama za dalali ! Kisha ukaingiza bidhaa Dukani kwa gharama zilezile ulizolipiwa . Labda ulalamikie gharama za...
Kweli kabisa . Sijaona watu wavivu kusoma kama wa TZ .Ukiwa na gazeti unasoma anakuangalia weee ! Then anakuomba gazeti nae asome . Mara PAAAP ! Kapindua ukurasa wa michezo . Anasoma kichwa cha habari tu na kukugeukia kutaka uchangie maoni yake . Haendelei kusoma . !
Kweli kabisa . Yale ni mabanda na sii jengo . Mungu atunusuru na hawa wanaojiita wasomi . Ardhi ni thamani inayokua sii sawasawa na kununua kitu kingine . Ilikuwaje waruhusu eneo nyetii kama lile kujenga mabanda badala ya angalau floors 4 ili kukidhi mahitaji kwa manufaa ya chuo na nchi ?
Hii tabia ya wamama kupandikiza chuki watoto wamchukie baba yao kwa sababu ya wao kutofautiana nimeishughudia kwa macho yangu . Ukiangalia utagundua ameamua kuwatumia watoto kwa maslahi yake binafsi . Yaani kama kawauzia kesi wao ili liwe ni suala la familia nzima . Wale watoto wanaoingia kwenye...
! Kukamilisha swali lako ungemuuliza kama yeye ni mwenyeji wa Mtwara . Lakini nahisi tatizo alilonalo ni mfadhaiko au alerge . Kwa mfano mtu ukijawa na hofu anaweza kutoa mkojo bila kujitambua .
Bado ukaendelea kumshirikisha mumeo , wewe ukaenda mahakamani kuweka zuio na yeye harakaharaka katafuta wakili kutoa ushauri , tena wa kumjenga / kumnusuru . Nakuambia utake usitake mtakuja kuachana tu . Tatizo lenu mna udhaifu wa kupenda pale mnapopenda . Hamsubiri kupendwa . Wewe ulijenga...
Wakenya wakitangaza mlima Kilimanjaro uko kenya tunalalamika . Sisi wenyewe tukitumia brand ya mlima Kilimanjaro ili ijulikane uko Tanzania , tunalaumiana . [emoji1241]
Nimekuelewa . NI UZINZI TU . Kuna kesi inaendelea mwanamke alikodi watu wa kwenda kumuua mumewe pamoja na mtoto wake mkubwa aliyezaa na mwanamke mwingine kabla ya ndoa yao ya kikristo na mumewe ili aweze kurithi mali . Wale Jamaa walichukua pesa lakini kwa huruma yao wakamtonya jamaa na kumpa...
Kuna dada yangu kaolewa na kabila tofauti , sio mchaga na tunaheshimiana sana shemeji yangu. Wakanipa kijana toka kwa kabila la shemeji yangu nikamkabidhi duka . Hana kitanda , hana chumba , anaishi kwangu , kula kulala kwangu . Kahonga wanawake kila wakija Dukani anawapa vitu bure kwa matarajio...
Pole sana . Je , benki wamewaambia kiasi halisi mnachodaiwa ? Usije kupiga hesabu wewe mwenyewe kwa kiasi mlicholipa mkaona mnadaiwa million 6 . Deni lina riba na kadiri siku zinaongezeka deli linazidi kuwa kubwa . Hapa JF ni sehemu sahihi ulioomba ushauri lakini weka picha ya nyumba mtapata...
Hiyo point no 3 . Pale niliposoma ' MAJORITY OF WOMEN ARE PROFESSIONAL PROSTITUTES ' . Je inawezekana wanatumia uasili wao wa kuwa mwanamke kupata mali ? Maana siku moja nilikuwa naangalia taarifa ya habari mwanamke anavunjiwa nyumba huku akilia na kusema nitapata wapi nyingine , mimi mjane ...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.