Kuna mawili. Moja katolewa (lina asilimia -10). Pili kakosea ama kasau kuweka kwenye mabano kama ivi; Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma) au Makamu Mkuu wa Chuo (Utawala).
Muiran anaongea kwa niaba ya Africa, ni mamilioni ya Waafrika walifariki na kuteseka katika biahsara ya utumwa. hii ni changamoto kwa nchi za Kiafrika!
Maisha ya Bob Marley ndiyo yaliyozaa mashairi yake. Akiwa upande wa mtu mweusi daima aliumizwa na namna maisha ya mtu mweusi yalivyokuwa mabaya kutokana na mfumo gandamizi uliojengwa kwa miongo na miongo. Katika wimbo huu ana wa hamasisha Watu weusi kupigania haki zao pasipo kujali ni ghiriba...
Utetezi wa kubakwa utafunika suala la mahusiano yao? hasa ile simu ya mwanaume mwingine kupigwa na Lulu kutoka kwenda kuipokea nje? Vipi hapo? Mdogo wake Kanu aliyekuwepo katika eneo la tukio ana ushadidi huu. Je unafutika kwa utetezi wa ubakaji?
Imepitwa na wakati iwapo nchi tayari imekwisha kustaarabika kwa maana ya kila raia kufuata sheria na taratibu kama impasavyo. Kwa nchi zenye matatizo mengi na makubwa kiuwajibikaji haistahili kuondolewa. Lakini hofu kubwa pia ni namna ya matumizi yake kwa sababu kama itakuwa imejikita katika...
Mzuvendi
Bado si vibaya kutumia Kiswahili kama una mashaka na lugha ya Kiingereza. Binafsi nadhani kuna sababu mahsusi ambazo zinaweza kutumika kuruhusu mwanamke kutoa mimba. Sababu hizo ni kama vile za kiafya na uhatarishaji wa afya ya mama kwa ujumla.
Tofauti na hapo sidhani kama ni vyema...
Ikiwa umekamatwa katika misingi ya kuzingatia sheria na taratibu zote kama ulivyozibainisha na kupelekwa kituo cha polisi na kisha mahakamani ndani ya masaa 24 na mahakama kuonelea kuwa huna hatia, Je, ni hatua gani (za kisheria kama zipo)unaweza kuchukua ili kufidia hasara kubwa uliyoipata...
Matukio ya papo kwa hapo yamebeba dhana tofauti ya utuhumiwa na yale matukio yaliyotokea kitambo. Utuhumiwa wa matukio ya papo kwa hapo yana sheria zake madhubuti ya namna ya kukabiliana nayo.
Binafsi sijapendezwa na mwenendo mzima wa siasa za Tanzania. Wakati nikimsikiliza mbunge huyu ambaye sithubutu tena kumwita mheshimiwa , wazo lililoniijia ni kuwa ametumia aina ya kilevi kama bangi kabla ya hotuba yake. Katika hali ya kawaida, maneno kama haya yamezoeleka kwa watu waliokata...
Wakati wakiendelea kutengeneza,
Nasi tutaendelea kuichongea jeneza,
Ili tuiue na kuizika kabisa wakishaimaliza,
Ndiyo zetu, haina kushangaa ni full umangimeza.
Natamani kuandika hoja za ufafanuzi,
lakini nimejawa kigugumizi,
kuhusu ukweli wa habari hizi,
Kama ni kweli na sio simulizi,
Basi kavaa ile ile (kwa kihaya "zesemu") hirizi,
Ya swahiba wake yule wetu mchizi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.