Huna Sababu ya kuumiza kichwa na mleta hoja hakuwa na Sababu ya kuleta hoja kama hii ya kipuuzi. Cha msingi mwacheni Magufuli afanye kazi yake na kama hukumchagua kaa kimya msimuhujumu.
Watanzania wa ajabu!! Mtu unaibia na kajitokeza Mtu anakusaidia kumkamata mwizi baadae unaanza kumtuhumu namna alivyomkamata sio!! Kwataarifa yako staili iliyobaki ya kuwakamata ni hiyo hiyo--zingine zote zilifail. Kama huna cha kuandika kwa kimya acha johnpombemagufuli na Majaliwa wapige kazi...
Nawashangaa sana watanzania kwa kusahau mapema--watu wote waliondolewa kwenye uwaziri kwa tuhuma na kashfa za kifisadi kipindi cha JK wasahau uwaziri. Alafu huyu jamaa kawapa bei gani mbona mnampa promo for nothing? Mnasahau huyu ndio alisema pesa za escrows sio za umma? Hatumtaki kama mmekula...
Taarifa haijitoshelezi!! Anataka kumpindua nini? Na tangu lini gazeti la Mawio ikaandika habari njema za Zitto? Kubenea acha siasa chafu, tumekupa ubunge ufanye kazi--punguza majungu na usianze kushambulia watu makini. Pambana na CCM na sio Zitto
Iweje atambue matokeo ya ubunge yaliyotangazwa na NEC ila kwenye urais asitambue?!! Kwani kuna NEC mbili? Si moja tu? Tulianza uchaguzi vizuri na matokeo yanapokelewa kwa Amani sana, please usiharibu mwishoni--kauli hizo ndio unajishtaki ICC mwenyewe iwapo jambo lolote likitokea
Mbona kashinda Sasa! Tatizo la washabiki wa Alikiba mnaendeshwa na kidoti na Wema! Kamwe hamtafanikiwa kupeperusha bendera ya Tanzania maana upo kimajungu wakati wenzenu wanafanya kazi
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.