Tanzania kama tutaweka dini kama kigezo tuendako si kuzuri, mimi nafikiri uwezo wa mtu ndo kiwe kigezo cha kwanza, uadilifu, uwazi na upendo viwe vigezo vingine.
Hata mimi naona mzee wetu huyu amekurupuka. Ila kabla sijamlaumu sana nataka nijue tu kama maoni haya ameyatoa kama maoni binafsi na sio kwamba alikuwa anakusudia kuwakilisha chama. Kama alikusudia kutoa maoni yake kama yeye basi ana haki ya kufanya hivyo. lakini naomba viongozi wa chama...
Mimi sielewi sana lakini nadhani wanakuwa viwango vyao tofauti na vya huku bara. ila ni mawazo yangu tu. Halafu nina uhakika kabisa kuwa elimu ya juu si jambo la kimuungano ila secondary si elimu ya juu lakini sijawahi kusikia matokeo yao ebu nguja niangalie kwenye tovuti ya necta
Kweli kabisa tumekuwa jamii ya hovyo jamii yenye ubinafsi uliopindukia, jamii ambayo watu wanajijali wenyewe tu! kila kipande cha ardhi wanataka kiwe cha kwao, hata kama si cha kwao wanafikiri wana haki ya kuchukua kutoka kwa mtu yoyete, jamii ambayo imejitengenezea mifumo ya kuwadhulumu...
Kwa nijuavyo mimi chungu ni aina ya mchwa au siafu ambao hukusanya majani na mabaki ya vyakula kwenye mashimo yao, na Kivuno ni mbadala wa neno mavuno.
Kwa nijuavyo mimi chungu ni aina ya mchwa au siafu ambao hukusanya majani na mabaki ya vyakula kwenye mashimo yao, na Kivuno ni mbadala wa neno mavuno.
Kaka mimi mwenyewe nilikuwepo kwenye mkutano na dogo mmoja alitobolewa mguuni na risasi na yeye alikuwa mbali kabisa na eneo ambako bomu lililipuka, kwa hiyo si mabomu tu waliturushia na risasi za moto pia hawa ni watu wa serikali.
Sasa mimi napata taabu kuamini eti police hawahusiki
Ndugu Kagalala, sisi watanzania tunasema zaidi kuliko kutenda kila tukio likitokea utasiki enough is enough lakini hatuchukui hatua yoyote watu wanaotuua wapo mitaani wanadunda na hakuna hatua yoyote tunayochukua mimi nafikiri ifikie mahali tukisema enough is enough tumaanishe kweli
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.