Natamani kuwepo na chuo cha kuwaandaa wale wote wanaotamani kuwa Wakuu wa Nchi hapo mbeleni. Ni jambo tata sana mtu kusimikwa Ukuu lakini mhusika akiwa hana maandalizi ya kazi hiyo.
Elia, usikate tamaa, miaka yako inakuruhusu kuendelea mbele kwa ari kubwa na nguvu kubwa zaidi. Kama mbuge nje ya bunge endelea kuwatumikia wananchi wako na ushirikiane nao kwa karibu. 2020 ii karibu.
Mawazo yangu: Sasa hivi hospitali zetu zinakomalia kutokusalimu amri kuwa wameshindwa kutokana vitisho. Wanaogopa kupoteza kazi. Hasa ukizingatia mgonjwa mwenyewe anatoka kundi la "malofa" hupelekwi nje hata iweje.
Mgombea A: "wewe ni kiongozi mstaarabu sana. Uliendesha kampeni za kistaarabu kweli maana sikukusikia ukinitukana hata mara moja. Isipokuwa wapambe wako ndio niliwasikia wakiporomosha kampeni za matusi. Au uliwatuma?" Jibu toka Mgombea B: Hapana. Halafu kimya.
Ningekuwa mimi Mgombea B pia...
Dunia ya leo hakuna siri tena. Ukitaka magazeti unapata mitandaoni. Ukitaka yanayojiri bungeni unapata mtandaoni. Siri ni nini na iko wapi? Huenda siri iko usalama wa taifa na jeshi la wananchi kwa kiasi fulani. Waliyozungumza hao wabunge ni mambo ya wazi kabisa na sio ya siri.
Nilitegemea angesema, kajifunza haki ya matokeo kuhojiwa mahakamani panapotokea malalamiko yeyote ya wagombea urais kuepuka malalamiko ya wizi wa kura. Na pia, umuhimu wa kuwa na Tume huru ya uchaguzi na mwisho pia viongozi wakuu wa mihimili ya serikali kutoteuliwa na mtu moja (Rais). Lakini eti...
Uhuru aliungwa mkono pekee kama mgombea. Ndio maana mahakama ilimsafisha kuwa hana hatia katika kesi hii. Mwenye hatia ni IEBC kutokuendesha uchaguzi kwa kufuata katiba. IEBC wamelitia taifa la Kenya hasara na nadhani hata Uhuru mwenyewe atawawajibisha. Kumuunga mkono mgombea tarajia mawili...
Nimeona hata kesi ikiwa inaendelea, lakini wananchi hawakatazwi kujadiliana yanayoendelea mahakamani kupitia tv, radio n.k. tofauti na kwetu ambapo huruhusiwi kabisa kuzungumzia chochote kwa jambo lililoko mahakamani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeona hata kesi ikiwa inaendelea, lakini wananchi hawakatazwi kujadiliana yanayoendelea mahakamani kupitia tv, radio n.k. tofauti na kwetu ambapo huruhusiwi kabisa kuzungumzia chochote kwa jambo lililoko mahakamani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Yeye kasema: Pamoja na kuwa mkataba unaruhusu yale yote mnayofanya .........nataka kujiongezea umaarufu .... ninyi tulieni nikimaliza nendeni mahakamani mtalipwa fidia na gharama za kesi.... halafu katika fidia ongezeni dau langu.
Wao: Hilo nalo ni jambo. Sisi tunatulia na tutajiandaa kwenda...
Ndio maana kila wizara akipelekwa hadumu anabadilishwa. Nashangaa sijui mwenyewe hajitambui!!!!! Hata hivyo nadhani isingekuwa kuiepusha serikali ya awamu ya nne isianguke (kama alivyodai mwenyewe katika ripoti ya Richmond), muda huu angekuwepo kijijini akishiriki kuumia uchungu wa hali ya maisha.
Kuna hili la matumizi ya simu dereva anapoendesha gari. Madereva wengi sana hufanya kazi hizi mbili kwa wakati moja. Kama sio hitilafu ya gari, basi nadhani alikuwa anaongea na simu au anaangalia sms wakati akiendesha. Nitaunga mkono iwapo faini kubwa itatozwa kwa dereva yeyote atakaepatikana...
Hi itakuwaje endapo 25% ya mawaziri, 25% ya wakuu wa mikoa na wilaya, 10% ya Makatibu wakuu, 10% ya Wakurugenzi wa halmashauri na wote walioimba "tuna imani na Lowassa" ndani ya CCM wakajiuzuru ndani ya mwezi moja kuanzia sasa. Hali italeta watu kujitambua kuwa uongozi sio wa mtu moja kwa...
Hisia zangu zinanilazimisha kuamini kuwa hii ilikuwa mpango mahususi wa kufuta headline ya kutumbuliwa kwa Nape na madudu ya Makonda kuvamia Clouds studio. Haya yaliyoonyeshwa kugunduliwa na Rais, yalishagundulika mapema ndio maana hakuagiza waliohusika wachukuliwe hatua.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.