Hatuna watu sahihi wa kufanya hiyo kazi Mzee, Mipira mingi inadondokea kwa Vini na yeye huwa hana pasi za mwisho nzuri kwa wenzie., hapo labda Ancelloti amrudishe kati na Rodrygo atokee kushoto.
Kipindi cha kwanza kimeisha, kiukweli hatujacheza vizuri, vijana wamekosa umakini sana haswa kwenye ukabaji wa mipira ya adhabu, watu hawaruki sijui shida ni nini.,
Carlo leo ameanza hivyo, Carvajal na Mendy leo wameanzia kwenye bench, ninadhani ni kutokana uchovu, badala yao, yupo Vazquez kulia, na Camavinga yupo kushoto, wakati huo huo Tchouameni amerudi kwenye kikosi, lakini akiwa na Rudiger kwenye ulinzi.,
HalaMadrid
Hiyo ni hatua ya mtoano kijana, hakuna atayekumbuka kama ulipiga pasi ngapi ama ulimiliki mpira kwa asilimia ngapi, kinachoangaliwa ni nani amesonga mbele tu basi.,
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.