Dini ni mawazo ya wanadamu ya namna ya kumtafuta Mungu. Yesu hakuja kuhubiri mawazo ya wanadamu bali alihubiri wokovu na msamaha wa dhambi. Yesu hakuja kuanzisha dini bali alileta msamaha wa dhambi duniani. Hicho ndicho mimi ninachohubiri, wokovu na msamaha wa dhambi tulioletewa ba Bwana Yesu...
Narudia tena, Yesu Kristo pekee ndiye mpatanishi kati mwanadamu na Mungu, tena ndiye anayetuombea kwa Baba. Acheni utapeli wa kuwafanya watu watoe sadaka ya ukombozi, huo ni wizi.
Pole sana, kwa hiyo wewe unazini kwa sababu una mtumishi wa kukuombea na unatoa sadaka ya ukombozi!
Mimi nimeokoka, huo ujinga uko mbali nami. Ninawafundisha watu njia ya kweli, ambayo ni Yesu Kristo.
Acha kuwadanganya watu, eti watoe sadaka ya ukombozi wakati Yesu alishatoa uhai wake kwa ajili yao.
Siamini kabisa katika hilo. Ninachokiamini ni kwamba, mpatanishi kati ya mwanadamu na Mungu ni Yesu tu. Leo hatuhitaji mpatanishi mwingine zaidi ya Yesu.
Nimeelewa sana. Kwenye post yako umeweka orodha ya dhambi ambazo unasema mtu akizifanya hataweza kusamehewa mpaka amwone mtumishi wa Mungu, tena akiwa na sadaka ya ukombozi. Mimi nasema hivi, hiyo sio kweli. Mtu yeyote akiamua kumrudia Bwana Yesu, hata kama awe amefanya maovu ya namna gani...
Imeandikwa tukiziungama dhambi zetu yeye ni mwaminifu navwa haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote, haijasema ukienda kuombewa kwa mtumishi fulani, utoe na sadaka.
Msamaha wa Mungu tunaupokea bure kwa njia ya imani ya Yesu Kristo. Hakuna msamaha leo hii unaopatikana...
Dini ni mpango wa ibilisi kuwafanya wanadamu wapumbazike huku Mungu wamemwacha mbali mno. Mungu kwa upendo wake ametuletea wokovu kupitia kwa Yesu Kristo, lakini dini imeingizwa hapo katikati ikawafanya watu wasiuone wokovu tulioletewa. Leo watu wanang'ang'ana kushika dini na madhehebu yao...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.