Kama wachangiaji wengi wanaojirudiarudia hapa JF wanavyotaka kutuaminisha kuwa wana chadema wengi wamekerwa na usaliti wa Zitto basi wangeshinikiza uongozi wa chama utii matakwa yao kwa kumfukuza Zitto. kama kweli mleta uzi ana ushujaa angeanzisha uzi wa kumpa Mbowe, Slaa na CC ya chadema...
Kinachonishtua ni uharaka wa baadhi ya nchi katika kutekeleza adhabu ya kifo. Huyu kahukumiwa na muda mfupi tu kanyongwa. Iraq pia kwa Saddam, na hivyo imekuwa kwa hukumu za watu wengine. Bangladesh juzi kwa yule jamaa wa uhalifu wa kivita. Iran etc.
Ni nchi nyingi zimetoa mchango kwa ukombozi wa South Africa. Tusing'ang'anie kupewa sifa zote sisi Tanzania. Hata hivyo motivation yetu ya kusaidia mapambano ya South Africa haikuwa ili tuje tusifiwe baadae bali kutimiza ndoto ya "Africa huru".
Kwanini usiende na tisheti ama shati lako la rangi ambayo sio nyeupe kuepusha kukodi shati? Matangazo si yapo na yanaelezea rangi za nguo za kuvaa, isiwe nyeupe wala isiwe na maandishi ama nembo yoyote.
Politics si mchezo, hadi uchaguzi mkuu uishe chadema mwakani kuna majeruhi wengi tu wa kisiasa kama inavyokuwaga ccm. Na funga kazi itakuwa ni kwenye nominations za ubunge. Mungu tupe uhai kuona kitakachojiri.
Walewale wanaoongoza kwa kumtaja Zitto kama mtu asiye aminika sasa wanajikomba na kumlamba viatu awape majina ya Uswizi. Ina maana ghafla bin vuuup Zitto anaaminika tena? Duh siasa za bongo hatareee sana.
Huo ndio ukweli uliousema. Yaani inavyopondwa FB utadhani yenyewe ndio inakupa tabia hizo mbaya wakati watumiaji wana akili zao timamu na utashi wa kuamua.
Wewe unadhani huu mgawanyo unakuja kwa bahati mbaya? Unadhani aliyetoka kwenye background ya familia ya ualimu anafurahia kuwa mwalimu ama analazimika (kwa sababu hana option) kuwa mwalimu na yeye pia kama wazazi wake waliomtangulia? Hii ni social class reproduction: na ipo hapo si kwa bahati...
Nairobi sasa iko mguu na kundi moja na majiji kama Tokyo, New York, Paris huku ikiwaacha kwa mbali majirani zake wa afrika mashariki: haya ndiyo mawazo ya wakenya: ndoto za mchana.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.