Habari wana JF,
Ndugu zangu wana JF, sisi wengine hatujakwenda shule hivyo ni vyema kuitafuta elimu kwa wajuzi.
Hivi panapokua na Serikali goigoi; Serikali inayofanyakazi kwa mazoea na kwa kutojali, hususani suala kushughulikia wizi mkubwa wa mabilioni unoanikwa na vyombo husika kila mwaka,na...
Habari wanaJF.
Kwa wafuatiliaji wa mambo nchini,matukio ya wizi wa mabilioni ya pesa nchini sio jambo la ajabu.Tunasema ni wizi kwa sababu mazingira yenyewe yamejaa ukakasi na hata Serikali imeshindwa kutoa majibu yenye mashiko.
Kwa mfano EPA,IPTL,MEREMETA,NDEGE MBOVU YA RAIS,RADA...
Habari zenu wanaJF,
Kama ilivyo ada kwa mujibu wa Katiba yetu, mwaka huu pia kutakua na Uchaguzi Mkuu hapo mwezi Octoba.Ni fursa kwa wananchi kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani.Ni katka harakati hizi za kusaka 'uheshimiwa' tutashuhudia minyukano, kejeli, matusi, vitisho n.k.
Lakini pia...
Ndugu zangu wataalamu wa umeme naomba mnielimishe mtiririko wa wiring kutoka mwanzo mpaka kwenye mashine ya kusaga au kukoboa.Ni vifaa gani viwepo na hatua zake mpaka kuwaka kwa mashine yenyewe.Maana nasikia starter,gea switch n.k.Karibuni tuelimishane.
Habari ndugu zangu.'Title' ipo wazi hapo juu.Naomba muongozo wenu tafadhali,ni vitu gani vinahitajika na gharama zake pia.
Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
Habari wanajf.
Kichwa cha habari kipo wazi hapo.Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 32.Natafuta msichana/mwanamke awe mpenzi na hatimaye awe mke wangu.Awe mrefu kiasi,asiwe kibonge,umri miaka 22 mpaka 30.Awe muislamu
Rangi yoyote.Aliye serious aje pm tuyajenge zaidi.
Sent using Jamii...
Ujinga ni hatari.Ujinga adui mkubwa mno.Ujinga humfanya mtu kuwa mtumwa wa hiari au wa lazima.Ujinga ni MTAJI MKUU wa shetani na wafuasi.Ujinga ni mtaji wa wanasiasa uchwara,wachovu na wasaka ulaji.Ujinga ni mtaji wa watawala madhalimu.Ujinga ni nyenzo ya matapeli,majizi yanayotumia peni na...
Ni katika nchi ya KUFIKIRIKA.Ni katika awamu hiyo ambapo ilikua 'msimu wa mavuno' kwa manyang'au na mapaka shume wa kila namna.Walikula bila ya kunawa na walisaza bila ya kufuta midomo.WALIRARUA vibaya rasilimali za nchi na kwa makucha ya chuma na KUTAFUNA fedha za umma kwa meno yenye sumu kali...
Habari wanajf.
Kwa mahitaji yako ya fundi viyoyozi na majokofu pamoja na friza,ni PM.
Installation ya viyoyozi na kuziosha,utengenezaji wa mafriji na mafriza.Huhitaji kuhangaika,huduma yetu ni hapo hapo nyumbani kwako au ofisini kwako.
Karibuni sana.
Habari wanaJF,
Inawezekana ni mada isiyoeleweka au ikawa ngumu kueleweka lakini wapo watakaonielewa.
Mambo wanayofanya wanadamu Leo; tena wenye akili timamu na wengine na elimu zao ni ya ajabu na aibu kubwa. Ni namna fulani ya uzuzu. Mwanadamu leo hii anafanya mambo ya hovyo kama mnyama au...
Nimekuja huku kukumbushana tu maana hata mimi ukumbusho huu unanihusu.
Zinaa ni uchafu na ni njia mbaya lakini wanaadamu tumeihalalisha rasmi.Sasa ni vyema tukazingatia yafuatayo;
Ukizini na mara moja uchafu huo wa zinaa utakuandama mpaka na wewe watu wako wanne wa karibu nao waziniwe vile...
Habari wana JF,
Pengine nimetumia lugha kali kidogo lakini ndio hivyo ilivyo. Kuna hawa wanaoitwa mafisadi ambao kimsingi si mafisadi bali ni majambazi watumiao peni na karatasi kuibia umma. Malalamiko dhidi ya ufisadi ni mengi na kashfa za ufisadi ni nyingi mno. Hili liko wazi.
Hawa watu ni...
Habari wanajf!
Wanajf, 'heading' iko wazi hapo juu.Naomba ufafanuzi tafadhali juu hili la 'kulazimika' (kulazimishwa?) kuichaji simu mara tu baada ya kuinunua kabla ya kuanza kuitumia.Kuna athari gani kuitumia kabla ya kuchaji?Na nini kinaathirika;simu au betri?
Karibuni tuelimishane maana...
Habari wanajf!
Nina hoja fupi ningependa tujadili kidogo.Ni hili suala la wasanii wetu wa kiume;aidha wa muziki au filamu kuvaa hereni.Suala hili limeshika kasi na wale wanaoitwa chipukizi wanaiga bila ya kuhoji.
Sasa kwa maadili ya Kiafrika, wasanii wa namna hii wana sifa ya kuitwa kioo cha...
Salaam kwako mheshimiwa,pole na majukumu ya kazi.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,kwa uchungu mkubwa nachukua fursa kukupa muhtasari wa kile kinachoendelea Tarafa ya Mvuha,Wilaya ya Morogoro Kusini kati ya wakulima na wafugaji.Hakika hili ni tatizo kubwa na la hatari.Kama mwezi mmoja hivi uliopita...
Habari wanajf!
Kuna mambo yanaendelea duniani kwa siri kubwa.Ni kazi ngumu mno kuyagundua.Moja ya mambo hayo ni mfumo wa saa.
Saa imebeba namba sita.Yaani katika saa fulani,kuna hesabu ya namba sita.Nifuatilie vizuri tuelewane.
Utaratibu wa kusoma saa (nyakati) umewekwa kinyume,hapa kuna...
Kama kuna kauli iliyonifurahisha na kujisikia fahari kama Mtanzania kutoka kwa Mkuu wa Nchi,basi ni kauli hiyo hapo juu ya Rais John Magufuli.Hiyo ni kauli ya kiuongozi.Amekana unafiki kwa kujikweza na kujipendekeza kwa 'wajomba' kwa kuhofia kuusema ukweli.Alichozungumza ndio ukweli na utabaki...
Kuna jambo linatatiza lugha yetu adhimu ya Kiswahili.Jambo lenyewe ni 'uharibifu' wa makusudi au kutojua wa MANTIKI ya maneno ya sanifu.Kuna maneno sanifu kabisa na yenye maana iliyokuwa wazi bila ya ukakasi,lakini kuna janga limeshamiri nchini la hii misamiati kupewa maana HASI.Yaani neno...
Habari wanaJF,
Baada ya 'mnyukano' mkali wa kati ya bunge,wanaharakati,wanahabari,wapinzani,chama tawala na wananchi juu ya bunge kuonyeshwa au kutoonyeshwa 'live',hatimaye 'mshindi amepatikana'.
Bunge sasa linaonyeshwa moja kwa moja.Mnyukano huu ulikua tukio langu la pili la ajabu tangu...
Habari wanaJF,
Kama mjuavyo, kasi ya 'utumbuaji majibu' imeshamiri. Imepamba moto kiasi kwamba wapo waliobeba kaulimbiu hii 'kikasuku' bila ya kuangalia mipaka ya mamlaka zao.
Niharakishe kutamka hapa kwamba naunga mkono harakati za Rais JPM za kudhibiti wizi 'uliohalalishwa' Serikalini na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.