Napendekeza akimaliza suala la fao la kujitoa wafanyakazi wapate haki zao pia awaamuru watoa huduma za simu wafungulie line zote zilizofungwa kwa amri ya serikali mpaka NIDA wamalize zoezi la kutoa vitambulisho vya taifa kwa sababu watu wengi hasa vijijini wanateseka sana kwa kukosa simu.
Lakini mfano umeenda kwa daktari kazini kwake kakuandikia dawa ambayo unatumia kwa miezi sita na siku hiyo umechukua dawa za kutosha mwezi mmoja,je ukienda duka la dawa ni lazima uwe na kile cheti cha daktari wakati majina ya zile dawa unazijua.
Kufungua line za simu zilizofungiwa na makampuni ya simu mpaka NIDA watoe vitambulisho vya taifa kwa kila mtanzania. Kurejesha nyumba za serikali na za mashirika ya uma zilizouzwa. Yeye raisi atangaze hadharani kwamba haungi mkono mashoga .
Kama utaweza mtafute mchezaji wa mpira wa Manchester City anaitwa Gabriel Jesus aliwahi kupata shida kama yako ili akuambie yeye tatizo hilo alilimalizaje. Yeye kwa sasa anafurahia maisha kuliko mwanzo.
mifuko yetu ya hifadhi ya jamii ni jipu nadhani mwenye mamlaka ya uteuzi apaleke vijana wake wa "kazi"kuchunguza kwa undani sababu za kuchelewesha wastaafu kupata mafao yao kwa wakati muafaka. Atakayepatikana na hatia atumbuliwe kwani hata ukimpeleka mtu toka uswazi leo ataona madudu ya baadhi...
Tumuombe ndugu yetu Pascal apeleke hii habari mahali panapohusika kusikilza shida za wanyonge kwani hali ni tete kila siku unafikiri afadhali ya jana watu tumeanza kusahau kukalia viti virefu.
Naunga mkono hoja nadhani serikali yetu sikivu watendaji wote wakuu wangeenda kujifunza namna makampuni ya watu binafsi wanvyofanya kazi hata ikibidi waende kuangalia ofisi za mabalozi wa nje waliopo nchini wanavyochapa kazi. Sehemu nyingine hata kuongea na simu binafsi ni shida lakini ofisi za...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.