Ni kitu ambacho siku zote sijakielewa, na labda ndugu zangu Waislamu watanisaidia hapa. Kufunga najua ni suala la kujipa muda wa kutafakari matendo na maisha yako na kuboresha uhusiano wako na Mwenyezi Mungu. Sasa sielewi kwa nini jambo hili lihusianishwe na kuonekana au kutoonekana kwa mwezi...
Nataka kufuga bundi kuzuia uharibifu wa panya wa mazao shambani kwangu, ila sasa hii jamii ninayoishi nayo wakiona nakusanya bundi hawanielewi, wanadhani mie mchawi. Halafu mie nawaona bundi wako wa-cute!
Nifanyeje? Wasije wakanichoma moto ndani ya nyumba yangu.
Sidhani kama kuna Mtanzania ambae hajui mazuri ya Magufuli akiwa raisi wa Tanzania, atapinga kwamba Magufuli hakuwa na roho ya uzalendo kwa Tanzania, alichukia ufisadi, alichukia watu ambao anawaona walikwamisha bidii zake za kuindeleza Tanzania. Hakuna Mtazania atakaepinga kwamba Magufuli...
Tuongee peupe leo, uwazi na ukweli. Mtu yeyote makini atagundua kwamba karibu kila kauli anazotoa Mwigulu zinalenga kutaka kuonyesha Raisi Samia ni bora sana kuliko alivyokuwa Raisi Magufuli. Tunakiri kwamba kuna baadhi ya mambo Raisi Samia ni bora kuliko alivyokuwa Raisi Magufuli, lakini tuseme...
Mwaka jana, June 2023, wakati waziri wa mambo ya nje akiwa Dr Tax, serikali ilitoa hili tamko pale Bungeni
Leo April 2024, serikali imetoa tena tamko hilo hilo pale pale Bungeni mbunge wa viti maalumu Suma Fyandomo alipouliza swali kuhusu uraia pacha.
Sasa nakumbuka tumekuwa na matamko kama...
Hii sio taarifa ya tukio bali ni tathmini ya utendaji wa jeshi letu la Polisi katika kukiuka haki za wananchi wa Tanzania, binadamu walioapa kuwalinda.
Hivi karibuni huko Kibaha kumetokea tukio la mtu kuuwawa kwa risasi, na mwili wake "kuokotwa" na wananchi. Ndugu wa mtu alieuwawa wanasema mtu...
Nimekuwa nikijiuliza sana hili swali, kwamba ikiwa iko wazi na dhahiri kabisa kwamba raisi wa Tanzania anaekuwa madarakani, anaamua kwa makusudi na huku akijua hilo, au kwa kushauriwa vibaya, au kwa kutoelewa, anavunja Katiba ya Tanzania (yaani kufanya uamuzi au kuchukua hatua inayoenda kinyume...
Mara nyingine nikiwaza mambo yanavyofanyika hapa Tanzaniia, naona kama tumekuwa jumuiya fulani katika uwanja wa fujo. Tunaishi kwa matamko ya Raisi, mawaziri, wakuu wa Polisi, wakuu wa mikoa na mara nyingine katibu mwenezi wa CCM!
Hivi hakuna watu wenye akili nchini, na hasa viongozi, wakaona...
Kama ulikuwa unafikiria kwamba baada ya umeme wa bwawa na Nyerere kuanza kupatikana basi matatizo ya mgawo wa umeme yatakuwa yamekwisha, basi sasa ni wakati wa kubadili mawazo yako.
Tanesco wanasema kwamba, mgawo wa umeme Tanzania kimsingi hautokani na ukosefu wa umeme wa kutosha, bali ni kwa...
Juzi hapa niliweka thread JF iliyosema wengi wa matajiri wa Tanzania ni wanasiasa na sio wafanya biashara, nikiwa na maana kwamba utajiri wao haujatokana na kufanya biashara bali umetokana na nafasi zao za kisiasa au uongozi serikalini kujitajirisha - urefu wa kamba zao. Kwa wengi wetu huo ni...
Watu wengi wakisikia maneno ya kina Tundu Lissu , Mbowe na kadhalika, yakionyesha kutoridhishwa na raisi Samia katika majukumu yake kama raisi wa Tanzania, wanapata hisia kwamba watu wa upinzani ndio wanaomnyima raisi Samia usingizi wa usiku. Ukiwaza hivyo uko nje kabisa ya mstari.
Changamoto...
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.
Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo...
Juzi hapa kulikuwa na tukia la askari Polisi mkuu wa kituo cha polisi Mwanakwerekwe, Zanzibar, akishambuliwa hadharani, na wananchi wakishangilia japo waliona askari alikuwa amezidiwa (angalia picha hapa chini).
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharib, amewalalamikia wananchi kwamba...
Hili ni jambo ambalo wenye hekima wanalielewa siku nyingi, na labda wengine wengi sasa wameanza kulielewa, kwamba kutokuwepo kwa usimamizi wa kiserikali wa upande wa bara kunatokeza nafasi kwa raisi akitoka Zanzibar kuwa na uwezekano wa kufanya mambo kwa namna ambayo inatoa maslahi makubwa...
Tumefikia sasa kwamba hapa nchini tuna watumiaji wa barabara wa aina mbili - Watanzania wa kawaida, na Watanzania "wenye nchi" ambao sheria za barabarani haziwahusu.
Hili kundi la "wenye nchi" ni wale ambao hawataki kabisa wabugudhiwe katika kuendesha juu ya spidi inayoruhusiwa, au wakae kwenye...
Ni kawaida kwamba katika nchi nyingi matajiri wakubwa utakuta ni wafanya biashara, lakini sio Tanzania. Kwa sasa wanaoongoza kwa kuwa matajiri wakubwa Tanzania ni wanasiasa waliopo madarakani au waliokuwa madarakani huko nyuma. Halafu wanafuatiwa na viongozi wa serikali, pamoja na ndugu zao...
Ni kweli maafa ya mafuriko yanaitwa natural disasters, lakini sio lazima natural disasters zilete maafa kwa raia na mali zao.
Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe, ubinafsi, kutojali, na uongozi mbovu kwa ujumla wa viongozi wa serikali. Si mara ya kwanza Dar es...
Kwa mtu ambae hana fani ya uhandisi angeona kwamba Dar es Salaam ya Chalamila ilifanya kazi nzuri sana miezi ya October na November 2023, kuziba mashimo mengi sana yaliyokuwa barabarani. Lakini baadhi ya mainjinia walituambia kilichokuwa kinafanyika ulikuwa ni utoto na kupiga fedha za serikali...
Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.
Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI...
Nimewahi kulizungumzia hili, na nitalizungumza tena. Watanzania bado tuna akili mbovu sana ya kuuona uteuzi kama fursa ya "kuula" au kufaidika kibinafsi.
Tunalaumu ufisadi, huku mtu anaefanya kazi TRA asiponunua gari miaka miwili baada ya kuanza kazi tunamwona mjinga! Ni wazi kwamba kama jumuia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.