Mnamo mwaka 2000 Niliota ndoto nikiwa nasafiri ndani ya basi na nimekaa na kijana mmoja mtanashati sana. Tuliongea mengi lakini cha kushangaza alishuka njiani na hatukukumbuka kupeana namba za simu. Huyu kijana aliendelea kubaki mawazoni mwangu kwa muda mrefu sana.
Miaka 10 baadaye nikiwa...
Kuna jambo moja ambalo hufundishwa na viongozi wa dini mbalimbali, ambalo pia waumini hulihubiri vizuri kila mahali wapatapo nafasi ya kufanya hivyo. Nalo si jingine ni lile la ‘mwanaume ni kichwa cha nyumba,' ikiwa na maana kuwa mwanaume ndiye mkuu wa nyumba au familia. Suala hili...
Naelekea Uzeeni sasa!
Ni miaka 16 sasa tangu nifahamiane naye, alikuwa ndio kwanza amemaliza kozi yake ya uhasibu na kuajiriwa katika taasisi ya misaada ya mmojawapo ya nchi za Ulaya hapa nchini.
Alipoanza kujitegemea, alipata nyumba iliyoko jirani na nyumbani kwetu, na huo ukawa ndio mwanzo...
Jana nilikuwa nikisikiliza hotuba ya mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na idadi ya watu hapa nchini kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana wa 2012. Katika hotuba yake mheshimiwa Raisi alisema kuwa matokeo hayo ni ishara kwamba ifikapo mwaka 2016 kuna uwezekano wa idadi...
Ili niwe mwenyeji wa jukwaa hili la Chit Chat?
Kwa kifupi mimi ninaishi Arusha, lakini nimezaliwa Dar na kukulia Dar ingawa wazazi wangu ni wenyeji wa Kilimanjaro. Kule Arusha niko Kibiashara, nikisafiri safiri kwenda Nairobi na Kampala kibiashara.
kwa sasa niko Dar kwa wazazi wangu nikisubiri...
Kwa huku kwetu ni wanaume wachache sana wanaomsaidia mwanamke bila lengo la kumpata mwanamke huyo. Hata hivyo sio wanawake wengi wanaokubali kulipa fadhila kwa njia hiyo, lakini wanaume wengi hutumia misaada au ofa kama chambo cha kuwanasia wanawake.
Kwa wanawake kusaidiwa ni kusaidiwa tu huwa...
Kuna mambo madogo madogo yanayowahusu wanaume huwa watu wengi hawayaoni na kufanya tafakuri. Katika makuzi yangu nimegundua udhaifu ambao wanaume wengi wanao lakini hausemwi kwa sababu ya mfumo dume kutawala. Nimegundua kwamba sifa ndio inayowauwa wanaume wengi, kwa kutaka kwao, kuimarisha mfumo...
Nusura niwe mtoto wa mitaani
Mazungumzo haya kati yangu na Yasinta niliyafanya Mnamo Machi 2009.
Ilikuwa ni siku ya ijumaa nikiwa katika ofisi yangu mpya iliyopo maeneno ya mjini alipita binti mmoja akiwa na begi lake dogo kama yale yanayotumika kubebea Lap Top.
Alinisalimia kwa uchangamfu...
Ilikuwa ni mwaka 1999 baada ya kuwa nimetumikia shirika la umma kwa takribani miaka 20 nilijikuta nikiwa miongoni mwa wafanyakazi 70 wa shirika hilo tuliotupwa nje ya ajira kwa kile kilichoitwa ridandansi, ili kulinusuru shirika hilo ambalo lilianza kuyumba kutokana na ushindani wa kibiashara...
Jana nimekutana na kijitabu kidogo cha kijani kwenye maktaba ya baba yangu. Kitabu hicho kimeandikwa "MUONGOZO WA CCM" ambacho kilichapwa mwaka 1981, na Printpak.
Wakati nakipitishia macho nikavutiwa sana na vifungu vilivyoandikwa ukurasa wa 77 na wa 80. Naomba ninukuu maneno hayo hapa chini...
Alipofika hapa Arusha kwa mara ya kwanza ni mimi niliyempokea, nakumbuka ilikuwani mwaka 2000. Alikuwa ndio amemaliza chuo cha ualimu huko Ndala Tabora na alipangiwa kuja kufanya kazi hapa Arusha. Akiwa ni mzaliwa wa huko Old Moshi mkoani Kilimanjaro, hakuwa na ndugu wala jamaa hapa Arusha...
Alikuja pale kazini kama mteja, lakini hilo jicho, mwenzangu mpaka niliogopa, maana jicho lake liliniganda mpaka nikaona aibu, hata hivyo alipomaliza shughuli zake aliondoka na kuahidi kurudi eti kunipa lifti nikirudi nyumbani kwangu, nikamwambia kuwa mpenzi wangu atanifuata, hakuonekana kujali...
Tukio hilo nililishuhudia hivi karibuni katika viunga vya Mwenge hapa jiji Dar wakati naenda Hospitali. Nilikuwa nimesimama kwenye duka moja la kuuza Dawa kuulizia dawa fulani ambayo niliandikiwa hospitalini. Upande wa pili wa barabara kutoka katika duka hilo kulikuwa na jamaa mmoja...
Ilikuwa ni mwaka 1998 na ninaukumbuka vizuri sana huo mwaka, kwani ndio mwaka niliovunja ungo, ni kipindi hicho ambapo nilianza kushangaa maumbile yangu jinsi yalivyobadilika na nilikuwa nahisi kuwa na mamlaka makubwa sana, sikutaka kuchuliwa kama mtoto tena ingawa nikuwa bado ni mtoto, kwa umbo...
Hebu chukulia umechelewa kufika kazini , unapofika ofisini unasikia sauti za wafanyakazi wenzako wakizungumza kwa ndani, unapofungua mlango na kuingia, ghafla wananyamaza na kukuangalia kwa mshangao!
Jiulize walikuwa wanazungumzia nini?
Kwa kuangalia mfano huo kwa haraka utagundua kwamba...
Ni kweli mikono yangu imeloa damu. Nahisi damu ya dhuluma, tena dhuluma ya uhai wa kiumbe ambacho kilihitaji kuishi. Aaah! Moyo unaniuma sana lakini walisema Wahenga kuwa maji yakimwagika katu hayazoleki na pia majuto ni mjukuu. Sisi ni binadamu, kuna matukio ambayo hututokea na kamwe hatuwezi...
Kuna jamaa mmoja alikuwa na rafiki yake anayeishi maeneo ya Ukonga naomba nimtambulishe kwa jina Ulimbo , sasa siku moja wakapanga na rafikiye anayeishi maeneo ya Tabata, (naomba huyu tumuite Kizito) wakutane kwenye Baa moja maneo ya Mwenge wajumuike pamoja na kupata moja moto moja baridi...
JE HIVI UNAJUA:
Kwamba tofauti kati ya nchi masikini na nchi tajiri haitokani na umri ambao nchi inayo. Na hilo tunaweza kulitambua kwa kuangalia nchi kama India na Misri.
Kwamba zina zaidi ya miaka 2000 tangu kuwepo kwake hapa duniani lakini bado ni nchi masikini.
Kwa upande mwingine nchi...
Tofauti kati ya nchi masikini na nchi tajiri haitokani na umri ambao nchi inayo. Na hilo tunaweza kulitambua kwa kuangalia nchi kama India na Misri.
Kwamba zina zaidi ya miaka 2000 tangu kuwepo kwake hapa duniani lakini bado ni nchi masikini.
Kwa upande mwingine nchi kama Canada, Australia na...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.