Nalazimika kuja na post hii kutokana na matukio kadhaa ya hivi karibuni ambayo yanayojitokeza tukiwa barabarani tunakimbizana na mkate wetu wa kila siku. Nashindwa kuelewa kama matukio haya yanatokana na uwezo mdogo wa polisi wa usalama barabarani kuongoza magari au ni maelekezo maalumu ya...
Mheshimiwa John Pombe Magufuli, ni Rais uliyejipambanua kama mtu usiyeogopa kitu na mwenye uwezo wa kutumbua majipu. Kazi hii ulijipa mwenyewe pale bungeni mwaka jana ulipolihutubia bunge kwa mara ya kwanza. Tunakupongeza sana kwa ujasiri huo na kwa kukubali kujipa kazi ambayo kimsingi ni ngumu...
Ndugu Magufuli akiwa Tabora aliahidi km 10 za barabara kwa madai kwamba anayo tayari bajeti ya kutengenezea Barabara hizo, Leo akiwa Kigoma pia ameahidi km 10 za barabara na kwamba bajeti yake ipo tayari na kutaja kuwa no kiasi cha sh 800 bilioni. Tunataka Maelezo kutoka NEC, kwamba Magufuli...
Tangu juzi umeme katika jimbo la ukonga umekatwa. Umeme huu ulikatwa saa moja kamili wakati taarifa ya habari ya channel ilipokuwa inaanza. Kwa harakaharaka vijana walijiridhisha kwamba TANESCO walikata umeme ili watu wasione msafara wa Lowassa kwenda kuchukua form. Lakini hadi kufikia hivi leo...
Waziri Sitta akiwa anatambua kabisa kwamba nchi ipo katika hali ya dharura, kutokana na mgomo wa mabasi, hajachukua hata hatua moja ya kushughulikia hali hii. Tulitegemea katika hali hii ya dharura, waziri mwenye dhamana ya uchukuzi angechukua hatua ya kubadilisha ratiba ya train ili angalau...
My Take
Inashangaza sana unapoona watu kama akina Ritz, faizaFox, Lizaboni, Mwigulu Nchemba, stroke na makanjanja wengine wa Chama twawala wanavyokisifia chama chao na Kikwete wao, huku nchi ikiendelea kuumia kutokana na kushuka kwa maendeleo ya binadamu pamoja na kushuka hata kwa thamani ya...
Ufisadi mkubwa unafanywa na manispaa ya Ilala katika ujenzi wa barabara ya kutoka Pugu kwenda majohe. Barabara hii ilianza kujengwa tangu mwaka 2012 na haijawahi kumalizika.
Daima barabara hii hujengwa nusunusu na kwa pole pole sana, kiasi cha kwamba mvua inapokuja huharibu kabisa na kuifanya...
Niseme tu ukweli kwamba polisi kwangu ni adui yangu namba moja. Nikiwa katika shida na ninahitaji msaada wa polisi sijawahi kuupata. Tuliwahi kuingiliwa na majambazi tukapiga simu polisi, walikuja dk tano baada ya majambazi kuondoka - hapa naongelea majambazi waliokaa ndani kwa zaidi ya saa...
Kwa sasa karibu mikoa yote ya Tanzania inakabiliwa na katizo la umeme la kila siku. Vijiji vya pembezoni mwa Dar Es Salaam kama vila Pugu Majohe, vinakosa umeme kila siku kuanzia saa kumi jioni au wakati mwingine kuanzia saa moja na nusu jioni hadi saa sita za usiku. Wakati mwingine wakazi wa...
Taarifa za Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda kutangaza nia ya kugombea Urais mwaka 2015 iliwashitua wengi sana hasa wakulima ambao hadi hivi sasa hawana mahali pa kuuza mahindi yao huku, Pinda akiwa hana majibu ya matatizo haya ya wakulima. Mizengo Pinda ambaye amekuwa waziri mkuu wa Tanzania kwa...
Naweza kusema watu wengi sana hawakuamini kama Kikwete angeweza kumaliza msimu wake wa miaka mitano ya mwisho bila ya mambo kukwamia njiani. Kikwete alioneekana ni kiongozi dhaifu sana, asiye na maamuzi wala uwezo wa kuifikisha nchi popote. Wengi walidhani uwezo wa Kikwete aliokuwa nao wakati...
Kutokana na trend ya maendeleo ya chama ya siku za hivi karibuni, kuanzia kwenye uchaguzi wa madiwani, nashawishika kwamba huu ni wakati mzuri sasa wa Mbowe kuondoka.
Ni dhahiri kwamba Mbowe ameshindwa kukiongoza chama au anazeeka kama mwenzake Lipumba kiasi cha kukifanya chama kianze...
Ndoa ya Rais wa Marekani Barak Obama na Michelle Obama ipo hatarani kuvunjika kufuatia kitendo cha Obama kuonekana katika picha za kimahaba na waziri mkuu wa Thailand Shinawatra. Inasemekana picha zenye kutiliwa shaka pia zilipigwa kati ya Obama na waziri mkuu wa Denmark.
Habari za ndani...
Ndugu zangu,
Nikiwa kama mwanachama mwaminifu na mtiifu wa CHADEMA, najitokeza tena kwa mara nyingine kuelezea maskitiko yangu juu ya minyukano hii inayoendelea ndani ya CHADEMA.
Niweke wazi kwamba ninasikitishwa sana na mwenendo wa kisiasa uliopo ndani ya CHADEMA hivi sasa, na ukimya wa...
Kila kunapokucha tunasikia makelele mengi sana kuhusu matumizi ya hela ya CHADEMA na mapungufu mengine mengi ya viongozi wa chama. Tulianza kuyasikia haya tangu wakati wa akina Mtela, na sasa akina Mwigamba. Lakini hatujawahi kusikia hata mtu mmoja anahoji matumizi ya hela na mapungufu ya...
Tangu Alhamis ya wiki iliyopita watu wa maeneo ya kigogo, majohe na kisarawe tunakabiliana na mgao mkali wa umeme ambao unaanza tangu saa nne za asubuhi hadi saa tatu za usiku au zaidi. Hatujui kama maeneo mengine ya Dar yanshida hii pia, but hali ya huku ni mbaya sana, na inashangaza kwb hadi...
Mwanzoni mwa mwezi huu nilileta hapa post ya kupendekeza Kikwete azungumze na Kagame ili wayamalize. Wapo wanaona mbali, waliisifia post ile na wapo wanaoona karibu walinitusi, kunikejeli na hata kuniita Mnyarwanda. Sasa Kikwete amesikiliza pendekezo langu, na hapa chini ni uthibitisho. Tena...
Sina uhakika ilikuwa ni lini, lakini inaonekana video iliwekwa youtube tangu mwezi wa tano. Na wala sijui kama ilishaletwa hapa or not. Lakini kama haikuletwa basi pata burudani ya jinsi Wanyarwanda wanaoishi Uingereza wanavyomchukia Rais wao.
Sijaamini macho yangu kwamba Rais huyu anachukiwa...
Waafrika huwa tunaamini kwamba ukimcheka mlemavu, au ukimsema vibaya mama mwenye mtoto mlemavu basi na wewe utapata ulemavu au utazaa mtoto mlemavu. Hii kwetu ni myth na kila mmoja anamheshimu mtu mwenye ulemavu bila kujali usumbufu anaoweza kuwa nao. Tuna familia nyingi za watu wenye ulemavu na...
Hivi inawezekanaje hasa hadi majirani zetu watuchezee namna hii? A Kenyan tea, halafu inaitwa Tanzania, pamoja na ramani ya Tanzania na twiga ambaye ni alama ya Tanzania? Hivi kweli hawa wenzetu wanaweza kuuza bidhaa zao kwa kutumia vivutio vyetu kwa style hii? I once saw a Kenyan Coffee with a...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.