Mnataka kubaki mjini je kuna namna gani ya kuendesha maisha maana umesema miradi iko kijijini na mzee amestaafu? Pesa ya kuhudumia familia mnategemea itoke wapi?
Au wazee watakuwa wanajishughulisha na nini iwapo mnabaki mjini au mtalima lami...joke!
Uendeshaji wa miradi ukoje huko kijijini...
Mkuu wewe mwenyewe hujiamini kubaki na huyo binti. Unataka wife akuaminije? Ebu tunza ndoa yako wewe usijeponzwa na kichwa cha chini, utaharibu ndoa yako na familia ya upande wa mkeo.
Au unafikiri mkeo yeye hatongozwi huko kazini? Au anavyokulindia heshima unamuona mjinga! Kwa taarifa yako...
Mimi hapa namhurumia mke wa jamaa. Usikute alikuwa anafanya mpaka kazi za ziada kusapoti familia huku akijua mwenzie ana matatizo kazini....yani wanaume jamani! Una una matatizo kazini anaona haitoshi anatafuta mchepuko, anaona haitoshi anaupeleka mchepuko wake mpaka nyumbani. Anazaa nao...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.