04.11.2020, Saa nne usiku:
Kwani uchaguzi si umeisha?
Kwani ushindi wa ‘kishindo’ si tayari?
Kwani ‘watu wengi’ si wanawakubali?
Kwani maandamano si yameshadhibitiwa kwa nguvu kubwa?
Sasa nini sababu ya kuendelea kuminya minya mitandao ya kijamii na ‘kutupimia kwenye vijiko’?
Hivi wanajua...
Mmekuwa na tabia ya kukata matangazo kila ifikapo saa saba usiku. Sifahamu matangazo hurejea alfajiri/asubuhi ya saa ngapi. Sina hakika tatizo lilianza lini lakini mwezi Juni niliuliza nikajibiwa “kuna tatizo kwenye minara linafanyiwa kazi”. Miezi mitatu baadae, bado maelezo ni yale yale, “kuna...
Kumekuwa na wimbi kubwa la watu wanaoelekeza mashambulizi kwa upinzani, hasa mgombea wa CHADEMA, T. A. Lissu. Katika mazingira ya uchaguzi ambapo chama kimoja kinaomba kura kurejea madarakani (chama tawala) na vyama vingine (vya upinzani) vinatafuta kukiondoa madarakani chama tawala, ni udhaifu...
Wiki iliyopita nimepita roundabout ya Msamvu na kuona kazi nzuri ya kutengeneza sanamu zinazoonesha vivutio vyetu. Moja ya sanamu hizo ni ile ya chui akimkamata mamba. Nina tatizo na hii sanamu. Jamii ya chui wenye tabia na uwezo wa kukamata mamba wanaitwa jaguars wanaopatikana bara Amerika...
Ni wazi sasa barakoa za vitambaa ndio 'habari ya mjini'. Sasa niwaulize wataalamu wetu wa afya, hizi barakoa zina uwezo wa kuzuia hivi virusi? Kama jibu ni hapana, sasa kwanini hamjachukua nafasi yetu badala yake mmeacha tu wananchi wazivae?
Au tunavaa barakoa ili iweje?
Wakongwe humu mtamkumbuka huyu mwanadada wa kuitwa Lara 1, "kubwa la maadui".
Posts zake ulikuwa huchoki kuzisoma, full of wit, mtoto wa mjini haswa! Sijamuona kitambo humu. Nimemiss uwepo wake.
Naomba kujuzwa, hivi yapo maduka binafsi ya kubadilisha fedha yanayofanya kazi au ndio basi tena, biashara wameachiwa mabenki? Maana huku niliko "bureau de change" niliyozoea kuiona ilifungwa kwa muda mrefu na sasa pamebadilishwa biashara.
Mara unamsikia kijana anaimba “inama nipachike rungu”, mara binti yule nae anaimba “nikikuona nabanwa na haja”, binti huyu nae eti "piga piga piga mpaka ufungulie bomba". Kama uko na wazazi au wakwe hapo ni aibu tupu. Yaani hawa vijana siku hizi sijui wanakwama wapi? Mbona wanaimba sana matusi...
Imekuwa ni kawaida kwenye mikutano mkuu akiwa anahutubia akitokea kumtaja kiongozi fulani basi kiongozi mtajwa husimama. Wakati mwingine mtu anatajwa mara kadhaa na kila akitajwa anasimama. Imefika wakati mkuu husikika akisema "kaa tu". Sikumbuki kuyaona haya awamu zilizopita. Ni kwamba siku...
Hii nimeiona kwa baadhi ya coaster Mbeya na Morogoro. Coaster (nadhani zote) mpangilio wake wa siti ni kuwa na siti 3 kwenye raw moja, yaani mbili upande mmoja halafu njia ya kupita kati kati kisha siti moja upande mwingine (2x1). Sasa baadhi ya wamiliki wanaamua kubadilisha mpangilio wa siti na...
Kwa siku kadhaa nilizopo hapa Mbeya kumekuwa ma mwingiliano wa mawimbi ya redio yenu (88.5) na redio kiss FM (88.3), kila baada ya muda kidogo. Hali hii inakera. Chukueni hatua tafadhali.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimelipia ada kwa ajili ya ku-renew leseni ya udereva tangu mwezi Februari hadi leo hii tarehe 31 Mei naambiwa leseni bado.
Maelezo ninayopewa ni kwamba eti kuna tatizo la upatikanaji wa materials za kutengenezea hizo leseni. Really? Miezi minne! You cannot be serious!
Inafahamika kwamba ukiwa na kifurushi cha cheka cha voda, mfano cha saa 24, ukinunua kifurushi kingine kabla ya muda wa saa 24 kuisha dakika za maongezi/sms/MB zinaongezeka juu ya zile zilizokuwemo bado kwenye kifurushi.
Lakini saa 24 zikifika hata kama ukikuwa bado na dakika za...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.