Napenda kuogea sabuni hizo ambazo mara nyingine zinaitwa sabuni za magadi. Uzuri wa sabuni hizo ni kuwa zinaondoa vipele kwenye ngozi, hasa vipele vya joto.
Hakuna sehemu yeyote ile ambapo mwandishi amelituhumu taifa la Tanzania, serikali au mtu yeyote yule binafsi. Kama nimemuelewa vizuri amewalenga wale waliofanya matukio hayo. Kwa maandishi yako haya inaelekea kuwa unaunga mkono vitendo hivyo walivyofanyiwa hao wahanga na kuwatetea waliofanya...
Huo ndio uhalisia wa mambo. Kwa wale wanaoweza kukipata kitabu hiki wakisome. Kinaelezea kwa undani zaidi kwa nini watu 'weusi' wanachukiwa na watu wa rangi zingine.
Sio kweli. Madaktari wengi wameambukizwa corona kwa kutibu watu ambao wameletwa hospitali kwa magonjwa mengine au hara waliopata ajali. Unaweza kuwa umebeba virusi vya corona na huna dalili kwa sababu virusi vinachukua hadi siku 14 ili mtu apate dalili za ugonjwa. Tuwe makini corona ni hatari sana!!
Iliiogopesha kwa sababu kua wakati mwigine nilikuwa napata shida wakati wa kurudi, na nikirudi nakaa kwa muda siwezi kufanya kitu chochote, nashindwa kunyanyuka, hata kukunja kidole, ingawa nasikia kila kitu kinachoendelea.
Kuna wakati nilikuwa natoka mara kwa mara, sio kwa kupenda lakini. Nilikuwa kila nikilala baada ya muda najiona napaa na kwenda sehemu mbali mbali kama ndege. I
Nilishakutana nao nilipokuwa UDSM pale Mlimani. Walikuwa wawili, mwanamke na mwanamume, wafupi mno!. Walikuwa wanaongea na walionekana kwamba hawakuniona kabisa ingawa tulipishana nao kwa karibu sana. Ajabi ni kwamba hata mimi sikutaharuki, nikaendelea na safari yangu!
Pia epuka kula vyakula vya wanga kupita kiasi. Kula zaidi mboga za majani, matunda, samaki zaidi. Epuka kushiba sana, shiba kama nusu hivi, ila ule kila unaposikia njaa kwa vyakula hivyo hivyo. Vilevile jitahid ikula chakula cha jioni mapema ili kuepuka kulala ukiwa umeshiba ndi!!
Hata mimi ni +60 kila asubuhi napiga push ups 120 kwa interval ya 30 bila kupumzika. Vile vile nafanya situps , na jogging angalau mara nne kwa wiki. Kufanya mazoezi ni nia, unaanza kidogo kidogo halafu unaongeza jinsi mwili unavyokubali.
Sidhani kama unaishi Finland, na kama unaishi huko nadhani unaishi Pitkaniemi au sehemu kama hiyo. Tafadhali sana usijumuishe Watanzania wengine kwenye mawazo yako binafsi kwa kuwa wewe sio msemaji wao. Aalio!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.