Tume huru ndio imesababisha kura kuhesabiwa na kutangazwa kwa haki huko Kenya. Hongera kwa wote waliopigania demokrasia ya kweli, hasa tume ya Uchaguzi kuwa huru.
Tunaangalia Bomas mubashara kusubiri kutangazwa kwa matokeo ya urais.
Makamo wa kwanza anatoka upinzani Kwa mujibu wa muafaka baada ya mazungumzo ya Rais Hussein Mwinyi na marehemu Maalim Seif.
Hivyo anaweza kuwa na msimamo tofauti na msimamo wa CCM wa serikali mbili.
Hongera kwa Serengeti girls! Mmeweka historia kwa kufuzu.
Lakini Bunge lisingetengua kanuni na kuwaingiza ndani ya ukumbi. Wangekaa tu kwenye gallery kama wageni wengine. Vinginevyo itaanza tabia ya kutengua kanuni.
Tuache mizuka.
Nimekikumbuka chama cha UNIP cha Zambia cha kina Keneth Kaunda. Hakipo kwa kuwa kilikubali kushindwa kwenye uchaguzi.
Kingekuwa bado kinatawala kingekuwa sehemu ya shughuli hiyo kwani nacho kilikuwa chama cha ukombozi.
Ngoja tusahihishe kidogo.
Wakati wa Nyerere akiwa rais hakuitwa Mtukufu, aliitwa Ndugu rais, au Mwalimu.
Wabunge waliitwa Ndugu mbunge.
Nadhani ni Mzee Mwinyi aliyekuja kuitwa Mtukufu.
Wabunge nao wakapitisha hoja kuwa waitwe waheshimiwa.
Mkuu Matola waambie hao wanaodhani kuwa maendeleo yao yataletwa na kugawa mikoa yao, wilaya zao, tarafa zao au kata zao, kwa maana ya kuzigawa na kuunda nyingi zaidi.
Kinachotakiwa ni kuwa pesa zitumike kupeleka maendeleo maeneo yote, huduma za miundombinu ya barabara, elimu, maji, umeme na...
Nchi masikini zinang'ang'ania kuongeza idadi ya mikoa au majimbo yao, haswa ili kukidhi matakwa na matamanio ya viongozi wa kisiasa. Gharama kubwa inaenda kwenye utawala. Huduma za jamii zinabaki nyuma.
Nchi tajiri hazishughuliki na kugawa states/ landers/ counties au cantons zao. Zinahakikisha...
Wasitambuliwe!
Hawana faida zaidi ya kuendeleza na kuendekeza ukabila na ukanda.
Walithaminiwa kutokana na ujinga wa zamani wa watawaliwa (subjects) wao.
Hongera ziende kwa Baba wa taifa Mwalimu Nyerere kwa kuutupilia mbali upuuzi huu wa uchifu.
Huko Zambia safari hii watangaza matokeo (huku kwetu ni wakurugenzi na tume) na pia mahakama zilikataa kuhalalisha haramu, wakatangaza ya kweli.
Lungu alitawanya mpaka wanajeshi majimbo mbalimbali wakati wa uchaguzi na hasa baada ya uchaguzi mambo yalipoanza kumuendea mrama.
Wakurugenzi, tume na...
Wakatwe kodi kwenye mishahara na posho.
Wakatwe pesa ya kuchangia mifuko ya hifadhi ya jamii.
Posho ya vikao iondolewe kwani wapo kazini.
wabunge/Spika wasiwe na uwezo wa kujipangia kufanya vikao vya posho.
Chato ilikuwa kijiji ndani ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.
Baadaye ikawa wilaya ikimegwa kutoka Biharamulo.
Ulivyoundwa mkoa mpya wa Geita mwaka 2012 Chato ikawekwa mkoa huo mpya, ikiondolewa kutoka mkoa wa Kagera.
Hakuna haja wala hoja kabisa ya kuanzisha mkoa mpya eneo hilo. Ni mtu...
Muacheni Rais Samia achague analoona ni chaguo bora. Litakalomsikiliza na kumsaidia katika majukumu, siyo litakalosikiliza 'wazee' ambao wakati wao ulishapita, walishaongoza zamani ilitosha. Walisahau nini ambacho wanataka kukirudia Ikulu?
Kweli mkuu mkaliman
Unajua hata Malkia wa sasa Elizabeth asingekuwa malkia wa Uingereza ila baba yake mkubwa Edward Albert (baadaye alikuja kuwa Mfalme Edward VIII) alijiuzulu ufalme baada ya kutawala kwa siku 326 tu kuanzia tarehe 20 Januari mpaka tarehe 11 Disemba mwaka huohuo 1936 ili naye...
Nadhani hakuna kabila linalowakilisha jingine, mfano itamkwe kuwa vazi la Wagogo linawakilisha pia Wanyaturu, Wanyiramba au Warangi wakati si vazi lao. Pia mavazi ya Wamasai kuwakilisha Wachagga na Wapare wakati si mavazi yao.
Pia umetumia kigezo kipi kugawa kanda? hakuna Kanda ya Ziwa wala...
Sofia Simba wakati akiwa mwenyekiti wa UWT alipendekeza kuwa mbunge wa viti maalum awakilishe miaka isiyozidi kumi (vipindi viwili), yaani agombee ubunge wa jimbo baada ya miaka mitano ya viti maalum na asiposhinda agombee tena jimbo baada ya miaka 10 ya viti maalum. Asiposhinda hapo basi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.