Binadamu yeyote anaweza kuingizwa mkenge, sasa yeye tayari ameshajua aliingizwa mkenge. Kwa nini anasita kufanya uamuzi haraka? Mamlaka anayo ya kufanya hivyo. Wote wanaoendesha hiyo kesi ni wateule wake.
Sawa hakuwa malaika, lakini unapokuwa kiongozi wa nchi(raisi) huwezi kuropoka hovyo hovyo kwa kisingizio eti siyo malaika ana upungufu kama binadamu wengine. Kiongozi lazima ajiheshimu. "Baki na mavi yako nyumbani" hayo siyo maneno ya kusemwa na raisi wa nchi hadharani tena kwenye umati wa watu.
Duh....!
Raisi aliunda tume ijue ukubwa wa tatizo na imletee mapendekezo ya nini kifanyike.
Na tume imefanya ilichofanya na kuleta mapedekezo ya nini kifanyike. Tume haijatunga sheria, imeleta mapendekezo tu.
Raisi hafungwi mahali popote na hayo mapendekezo ya tume. Raisi ana washauri wake...
Eti Wakenya ni wajanja wajanja! Kwa hiyo tutafute wajinga wajinga ndiyo tufanye nao biashara? Utajifunza nini kwa wajinga? Tunahitaji watu wajanja tena zaidi ya hao wakenya, hapo tutakuwa na la kujifunza. Nikupe mfano mdogo, Timu ya Simba 2019 ilipoingia group stage ilikuwa inafungwa mabao mengi...
Hapo sasa, na hicho kitu kingine wanataka kiwe nini? Naamini hata hicho kitu kingine wakuhoji wangehoji tu. Ni nani chini ya jua anaweza kufanya kitu kila mtu akaridhika?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.