Binafsi nimependa ukweli na uwazi wako hujaona aibu kuandika yaliyo moyoni mwako, kwa hili itakusaidia kusonga mbele maana tunasonga mbele kwa kujifunza.
Nirudi kwemye mada, nakushauru uendelee kufanya kazi hapo na uendelee kusave as much as possible hata kwa kushindia mihogo. Nina uhakika...
Kilicho ndani ya moyo wake kinaweza kuwa ndiyo jibu sahihi ya kile Mungu alichomuandalia na vile vile kinaweza kuwa siyo sahihi.
Ili awe na uhakika sasa ndiyo anatakiwa kumuomba Mungu yeye ndiye mwenye majibu yote.
Kuhusu suala la wazazi wake sijaona pahala alipoandika amegombana nao, ila wao...
Fanya kilicho ndani ya moyo wako, ushakuwa mtu mzima sasa hutakiwi kuyumbishwa na mawazo ya wazazi/ndugu hatma ya maisha yako iko mikononi mwa Mungu na wewe mwenyewe.
Nafasi waliyo nayo wazazi/ndugu zako ni kukushauri tu na kukuonyesha njia sahihi katika maisha.
Muombe sana Mungu yeye ndiye...
Hili ni janga lingine chini ya jua, yaani mtu kukopa unaomba tena kwa kubembeleza halafu kulipa hutaki tena maksudi kabisa.
Si ajabu mtu huyu anamuomba Mungu abariki maisha yake wakati yeye anabomoa ya wengine.
Ndugu ni vyema ukalipa tu deni lako ni ishara ya uungwana na ustaarabu katika...
Inabidi ujitathimini mwenyewe, waswahili wana mseme wao " ndege wafananao huruka pamoja". Ukiona marafiki/watu unao waamini wana chembe za kutokuwa wa aminifu kwenye pesa jiangalie sana na wewe yawezekana uko hivo hivo.
Wapo watu wengi tu waaminifu kwenye pesa, sasa kwasababu haujakutana nao...
Ni kweli makato ya kufanya hii miamala yamekuwa makubwa mno, juzi nimetoa pesa kwa wakala M pesa yaani 350,000/= nakatwa shilingi 6000/= kama service charge. Kwa kweli ilinitia uchungu.
Kuna haja ya hii mitandao ya simu kupitia upya gharama za huduma zao. Maana kwa mwendo huu tutashindwa hata...
Umeweza vyema harusi si tukio la muhimu sana ila ndoa ndiyo tukio la muhimu sana. Unaweza ukafunga ndoa halali na ukapata baraka zote kutoka kwa Mungu, pia unaweza ukafanya harusi kubwa sana na usipate baraka zozote toka kwa Mungu.
Nachotaka kusema hapa ni kuwa ndoa ni mpango wa Mungu na harusi...
Kwako wewe muanzisha uzi ni wazi umekwazika sana, kama ndiyo umestaafu nikupe pole sana. Unaweza ukazitukana sana hizo taasisi za umma na hata serikali kadri uwezavyo lakini mwisho wa siku hautakuwa umesaidia chochote zaidi ya kudhihirisha upumbavu wako.
Kwanza ulitakiwa kujua sababu ya...
Asante ndugu, nilikuwa nashangaa tu kumbe ni kitabu cha Yoshua na sio Sira. Makosa kama haya kwenye uandishi husababisha habari nzima kupuuzwa na kuonekana ni ya uongo.
Ni vyema kabla huja post kitu chochote kwenye hii mitandao ukapitia upya kile ulicho andika ili kuondoa makosa kama haya.
Mimi naomba kujua hicho kitabu cha SIRA ndiyo kipi? Kipo kwenye Biblia ipi, agano la kale au agano jipya?
Sijawahi sikia wala kukiona kabisa aina hii ya kitabu, naomba kueleweshwa tafadhali kwa mwenye ufahamu na kitabu hiki.
Waziri wa Kaskazini
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.