Ni kweli kabisa kwamba aliyeandika article ya The Economist ana lake jambo ikiwa ni pamoja na kukasirishwa na hatua ya Tanzania ya kukataa kuiingiza ardhi katika moja ya "mali" za EAC. Lakini pia ni kweli kwamba uchumi wetu na mambo yetu kwa ujumla yamekuwa na hitilafu kubwa ya kuendeshwa...
Asiduwaze vipi wakati kila kitu hapa ni izeee. Ni hao waliomtuhumu ndio wanaotakiwa kutuhumiwa na wananchi waliowatuma kuilinda ikulu yao na wala si huyo mwananchi ambaye alitaka tu kuonesha ni kwa kiasi gani kila idara ina matobo ya kutisha.
Bila ya kuwabana wote kwa umoja wao na katika makundi yao ipo hatari watu hawa nikiwa na maana ya wale wote wanaosikika zaidi katika siasa za TZ wakatupelekesha na hatimaye tukajikuta tunacheza mduara ngoma isiyokuwa na staili yoyote ili mradi unazunguka na kutingisha kiungo chako chochote.
Vita...
Matusi ya Wakenya ndugu zangu ni ya kuanzia zama zile za Ujamaa. Lakini ukweli ni kwamba suala linalowakera zaidi Wakenya ni ardhi. Wanataka ardhi iingizwe katika moja ya mali za pamoja za Jumuiya ya afrika Mashariki. JK anasema hapana hilo haliwezekani kwa sababu moja tu ya msingi.... Kwamba...
Tunarudi pale pale kwamba mapambano yanayofanyika bila ya kuwa na itikadi iliyo wazi ina hatari ya kueneza na kuendeleza yale yale ambayo yanapigwa vita na baadhi ya washiriki wa mapambano yenyewe.
Kwa nini Sitta na SSG yake hawaweki wazi itikadi yao mbele ya umma ili tujue kwamba kama wakiingia...
Hivi waandishi wa TZ ni rahisi kiasi hicho? Shilingi elfu kumi??? Hao UWT nao kweli laki moja? Napata taabu kuamini stori kama hiyo. Kumbuka bei ya mafuta iko juu na hongo ni lazima iwe na mvuto..... Tukitunga tutunge kwa akili zaidi....
Katika zama hizi kweli tunahitaji kuanza kupembuana kwa mazingira na mandhari ya mahala tulipozaliwa na/au kukulia? Hii si ni sawa na wale wanaosema kwamba shughuli anayoiweza Mswahili nikiwa na maana ya Mwafrika ni kucheza ndombolo yaani kuburudisha tu na kamwe si shughuli kama ya kuongoza...
Sawa nakubali kwamba timing ni muhimu sana lakini unafanya mapinduzi ili upate nini? Nina maana lazima kuwepo na malengo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Tuseme tumefanikiwa kukiondoa chama tawala kutoka katika madaraka, jambo ambalo litawezekana kama kweli kuna dhamira ya kweli miongoni mwa...
Mzee Mwanakijiji hili linanipa shaka kwa sababu kwangu mimi muda uliobakia hadi kufikia masanduku ya kura ya mwaka 2010 ni mfupi mno. Itikadi inahitaji kuainishwa mapema na wale wanaokubaliana nayo wajitokeze na kujipembua kwa uelewa wao wa itikadi yenyewe ili waweze kushiriki katika mapmabnao...
Nakubali kwamba njia ni mapambano lakini si ni lazima mapambano yenyewe yaongozwe na itikadi ambayo iko wazi na inayoeleweka kwa wale walio mstari wa mbele na wale wanaohamasishwa kujiunga na mapambano yenyewe?
Pengine moja ya sababu kubwa zinazotufanya baadhi yetu kushindwa kushiriki...
sio kwamba tumeanza kuchanganya mambo? sitaki kuamini kwamba haya ni mapambano ya kikabila. nadhani tuchimbe kwa undani na kurejea historia ya matabaka na historia ya uchumi wa nchi yetukwani kwa kuanza kusema kwamba kuna usukuma na uchaga tunarahisisha mno mambo.
Lakini pia kuna jambo moja linajitokeza wazi kwamba hatuwezi kuendesha serikali kwa kusubiri watu wakwaruzane ndipo eti sheria ifuate. Ni vyema sheria ikafuata mkondo wake na ndio sababu vyombo mbalimbali na asasi kama vile TAKUKURU vikaundwa.
Kama TAKUKURU haifanyi kazi hadi ifanyiwe sasa...
Ni vyema vielelezo vikafanyiwa kazi na kama kuna kesi basi na ipelekwe kwa Pilato ili pengine atusaidie kutusogeza mbele kwenye ajenda nyingine mpya ya kuleta maendeleo kwani tumesimama katika ajenda moja kwa muda mrefu na hatuoni kama tunapiga hatua. Ufisadi ni hatari ndiyo kwa Taifa letu...
It is a pleasure indeed to join your ranks. Let me say Hi to all of you and hope that I will not only benefit from your sharp and critical minds but will also enjoy exchanging news and views.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.