Sukari ya sh 500 ni g 150 na Kuna zilizopekiwa tayari Kwa ujazo wa g 150 na unaweza kupima wewe mwenyewe Kwa ujazo huo ingawa siku hizi sukari ya ujazo huo tunauza sh 600. Ila hiyo sukari ya sh 300 hata mimi nahitaji uzoefu .
Kuzaa watoto ni jukumu langu, siwezi kuchukua kitu ambacho si jukumu langu kikaingilia au kuathiri jukumu langu. Kwani wewe unalea watoto wangapi yatima? Pamoja na hayo yote kusaidia ni moyo wa mtu na ndio maana hata masikini wanasaidiana wenyewe kwa wenyewe kwa kile kidogo wanachopata.
Vinginevyo Dunia ingeshuhudia wale wasiooa/kuolewa wangekuwa matajiri zaidi kuliko waliooa/kuolewa na hawana watoto. Na wale waliooa/kuolewa na wakawa na mtoto mmoja au wachache wangekuwa matajiri zaidi kuliko wenye watoto wengi. Binafsi nina watoto wengi na ninaishi vizuri kuliko baadhi ya watu...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.