Niwe mkweli , mimi ni mtu wa kipato cha kati. Niliwahi kuoa mwanamke kutoka katika familia ya kipato cha chini. Ilikuwa sipati nafasi hata mara moja ya kukaa mimi na mke wangu tule pamoja mchana. Lazima shemeji ua mama mdogo au baba mdogo lazima waje kumtembelea mke wangu wakati wa kula...
Umezungumza kitu hasa. Wengi wetu tunafikiria kuiba tu. Yaani mtu akosee kukuamini na wewe unachukua nafasi hapo hapo. Na hii tabia sijui kama tutakuja kuiacha. Biashara nyingi zinakufa kwa sababu ya wizi / udokozi wa wafanyakazi.
Tuwe wakweli tu, mtu unayemchangia si ajabu ana nyumba yake, wewe unaelazimishwa kuchanga hata kiwanja huna. Ni sawa na hawa ombaomba wao wana nyumba zao wamepangisha . Hili mimi nimewasikia wao wenyewe ombaomba wakiongea. Sasa wewe unayejifanya una huruma sana unawachangia ilhali huna hata...
Kutegemea maji kuwa ndio chanzo cha umeme ni kujidanganya. Ukuna ukame wa mfululizo itakuwaje? Ufumbuzi ulikuwa gesi tu. Lakini tatizo viongozi wanaloona wao kuwa ndilo linafaa basi ni hilo hilo. Hawataki ushauri kutoka kwa wataalamu wa fani hiyo.
Kuna hospitali moja ya kinamama ipo Kariakoo mtaa wa Narun'gombe corner na Luvingstone. Nyuma ya NMB iliopo mtaa wa Luvingstone. Inaitwa Kings hospital.
Aliniambia binti yangu ambaye ni daktari, '' Baba usiende kwa madaktari vijana, hawa walisoma ili wapate vyeti sio kuelewa''. Na mimi nakubaliana nae kabisa. Bora nitibiwe na nurse mtu mzima kuliko kutibiwa na daktari kijana.
Labda inawezekana, lakini ingekuwa fikra hizo zipo sawa basi nusu ya matajiri wa hapa bongo wasingekuwepo leo hii.
Sent from my SM-A525F using JamiiForums mobile app
Tafadhali nakuomba usiache kunywa pombe. Kodi hiyo uliokuwa unalipa atalipa nani? Barabara na dawa hospitalini itakuwa shida kwetu. Tafadhali usiache. Watoto wanasoma shule kwa kodi yako. Tafadhal !!
Moja katika vitu vizito sana kuvibeba duniani ni kubeba jeneza lenye mwili wa mtoto wako. Mwenyezi Mungu akupe nguvu na subira katika kipindi hiki kigumu. Amin.
Kwa sisi ambao umri umesogeasogea kidogo ndio tunamwita nguli. Kwa kiwa tunamjua. Ulishawahi kusoma gazeti la Fahari? Kama utaweza kulipata basi lisome.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.