Habari wana jamvini? Katika hangaika yangu nimepata wateja wa mafuta ya alizeti, nimesikia yanapatikana Singida, tatizo sijui pa kuanzia ili kuyapata na kuyaleta Dar ili kusupply. Naomba msaada wenu kwa wanaojua mchakato mzima. Tupigane na umasikini tulijenge taifa
Habari wanajamvini!
Naomba kujua kama biashara ya nafaka inalipa. Nataka kufungua duka la nafaka, nikianza na mchele mahindi na maharage.
Tulijenge taifa
Habari wana jamvini,
Napenda kujua kama ni kweli hizi biashara za mitandao zinazofanywa na kampuni kama Forever Living na GNLD zinaweza kumkwamua mtu kimaisha.
Hamjambo wandugu,
Nimejifunza kupamba kumbi za sherehe. Sina uzoefu sana. Kwa sasa napamba kwa gharama ndogo sana ili kupata uzoefu.
Kama kuna mtu mwenye uzoefu na kazi hii, naomba kufuatana naye kwenye kazi zake hata kwa kulipa ili nipate uzoefu zaidi.
Asanteni
Habari wandungu,
Mimi si mzoefu wa kilimo, naomba wataalamu na wazoefu wa kilimo wanijulishe kuwa ni kilimo kipi kipo juu zaidi (faida kubwa) kati ya mahindi na mpunga?
Asanteni wana jamvini
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.