Sishangai kwa kauli za jk kwani mara nyingi huwa ccm wanaropoka pasipo kufikiria madhara ya kauli zao. Huwezi kutamka maneno kama hayo katika nchi ya kidemokrasia na kama si ya kidemokrasia ni bora watangaze wazi kwamba hakuna kuwa na vyama vingi kuliko kupoteza resource kuingia kwenye uchaguzi...
Bombu inaelekea hadithi hii ni ya kutunga na siyo hali halisi iliyotokea. Iweje wewe mke wa mtu na unajua 100% huna mtu mwingine zaidi ya mume wako akutoe nyumbani kwenda eneo la kukutana? Hapa inaonesha kwamba kuna wengine. Hukujiuliza suppose mumeo anakukuta sehemu hiyo wakati hana taarifa za...
Hivi hizi live coverage za TBC1 ni nani anayezilipia kwa shughuli kama hizi za kuwasha mwenge au mikutano ya CCM? TBC wasijishau kwamba wao ni chombo cha taifa kinatakiwa kijiendeshe kibiashara pamoja na kupewa ruzuku na serikali ambayo ni kodi ya wananchi
Hayo ni majina yanafanana tuu si yule aliyejivua gamba na kuvaa gwanda. Waandishi wa habari walimuuliza PM jana juu ya jina hilo na hayo ndiyo yalikuwa majibu yake. Kama una uhakika kwamba PM kadanganya tena, leta ushahidi hapa.
Ukisema "Lowassa nadhani hakuhangaika na Huu msiba wa kisanii" unataka kutuambia nini? kwamba Lowassa ni makini sana kuliko wana ccm wenzake au serikali ya ccm? sidhani. Bila shaka hayupo nchini maana naamini kabisa angekuwa wa kwanza kufika katika msiba huo kwa malengo ya kisiasa.
Wanasahau kwamba uchaguzi ule hawakushinda bali walichakachua. Pia wasisahau kwamba baada ya 2015 wao watakuwa chama cha ushindani na kanuni hizohizo kama hazitabadilishwa leo zitawaathiri wao vilevile na wasije kupiga kelele.
Huyu Ngereja hajui anachokisema. Hana uhakika na anachokisema. Wala hajui kama ndege zinaruka moja kwa moja nje ya nchi. Ni waziri wa namna gani huyu? Hatakufikiri kidogo hawezi? Ni mara ngapi amewashuhudia maofisa wa BOT wakikagua dhahabu JNIA? Je BOT ni wataalam wa dhabu mpaka wakague wao...
Ukiona magari ya deraya yanatumika either kuwalinda viongozi au kusuppress umma ujue kwamba uongozi uliopo haukuingia ki halali madarakani. Kiongozi aliyeingia ki halali hawezi kuwa na msururu wa walinzi kwa sababu hana hofu na wananchi waliomchagua. Ukiona vyombo vya ulinzi na usalama...
Ukiona magari ya deraya yanatumika either kuwalinda viongozi au kusuppress umma ujue kwamba uongozi uliopo haukuingia ki halali madarakani. Kiongozi aliyeingia ki halali hawezi kuwa na msururu wa walinzi kwa sababu hana hofu na wananchi waliomchagua. Ukiona vyombo vya ulinzi na usalama...
Tatizo la viongozi wa nchi ni kulewa madaraka kiasi kwamba wanashindwa kutofautisha shughuli ya serikali na shughuli ya chama. Ndiyo maana Tunduma wana wapopoa kwa mawe kwa sababu wanatumia raslimali za serikali kwa manufaa ya chama, kitu ambacho si sahihi hata kidogo. Waacheni wapigwe mawe tuu...
Kwa maoni yangu si busara sasa hivi kwa BOT kufikiria kuchapisha noti ya TZS 20,000 kwa sababu mpaka sasa noti iliyo kubwa zaidi ambayo ni TZS 10,000 siyo watanzania wengi wa kawaida ambao at any time utakuta anayo mfukoni. Ni katika miji mikuu tuu ndiyo utakuta watu wengi wana hiyo TZS 10,000...
Siyo inawezekana TAKUKURU hawafanyi kazi zao vizuri. Hilom halina ubishi kwa sababu TAKUKURU wapo kwa ajili ya ccm na si kutimiza wajibu na majukumu ya kuundwa kwa kikosi hicho. Hakuna chombo chochote cha usalama kinachofanya kazi kwa weledi, itakuwa TAKUKURU?
Habari hii imekosa maelezo kama mapatano hayo yalifanyika wapi na wapatanishi walikuwa ni akina nani na yamefanyika lini. Kwa picha tuu kila mtu anaweza kutoa maelezo yake kulingana na anavyoiona picha.
Kama Mkimbizwambio unaweza kudadavua habari hii na kuitolea maelezo itakuwa vizuri sana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.