Sidhani kama atafanikisha kupatia ufumbuzi hili suala la umeme kwani nadhani halimuathiri yeye kama raisi na sidhani kama kashawahi kulala kiza nyumbani kwake tokea apate madaraka Kanali "Dr" Kikwete. Kukubali kwamba ataweza kufanikisha hili sifikirii kwani halimgusi hili tatizo na kwa ungwe hii...
Nadhani wanachadema na baadhi ya wanaobandika mawazo yao hapa jf hamumtendei haki Mh. Zitto Kabwe kwa nini mnamdodosa sana kweli nimeamini..."bata ukimchunguza sana hautomla". Siamini kwamba Zitto anafanya mbinu za kukiasi Chadema ila ukinzani wake na hoja zinazoibuliwa na viongozi wenzake ndani...
@Afrodenzi Nadhani sheria zipo kwani kosa la kubaka lina hukumu yake sina hakika miaka mingapi ila jamii inabidi kuwalinda wakina mama. Inastaabisha kama waganguzi (Madaktari) kweli hushiriki kwenye uovu huu wa kubaka mama zao, dada zao na watu wa jinsia hii. Kweli kutoa huduma ni wito na nchi...
Naamini haki ya watoto hawa italipwa kwani hawana makosa yoyote. Mwenyezi waongezee nguvu, wazazi waliopoteza watoto wao kwenye mazingira magumu kama haya duniani kote Amin.
Kiranga nimeangalia hapo juu naona makosa yote ya lugha yamerekebishwa kweli JF Home of Great Thinkers. Naunga mkono hoja yako
"Miafrika Ndivyo Tulivyo- Nyani Ngabu"
@Kiranga ni sawa umetoa hoja ulizoziambatanisha kwenye mabandiko tofauti lakini umeshikilia kunasibisha kizungu alichoandika Mheshimiwa na elimu yake ya UDSM. Cha msingi tuendelee kujenga hoja na kusubiri Mheshimiwa aje kueleza dhumuni lake la kuwasilisha bandiko hili hapa. Wacha miye niendelee...
@Kiranga heshima mbele mkuu, nadhani tunatoka kwenye hoja aliyowasilisha Mheshimiwa Zitto Kabwe na kutokomea kwenye kujadili lugha ya kiuandishi. Si vizuri kubezana k.h.s vyuo na kushabikia lugha ya mkoloni (kizungu). Turudi kwenye kuijibu hoja iliyo mbele yetu, kwa nini Mwalimu aliunga mkono...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.