Katika agenda tisa zilizosababisha kuundwa kwa tume ya kusaka maoni ya maridhiano, mradi ukipewa jina la Mpango wa Kujenga Daraja, yaani Building Bridge Initiative (BBI) Kenya, nyingi zinaihusu na Tanzania, lakini ipo kubwa zaidi.
Moja ya agenda ambazo zilibebwa ili kuzitafutia ufumbuzi ni...
Katika pitapita nimekutana na taarifa inayomuhusu Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na ikanifurahisha sana kwa jinsi alivyo na huruma na wananchi wake. Nikawaza jirani zao wangeambiwa "hili ongezeko mtalipa na asiyetaka atafute nchi anakoona kuna faa". Habari kamili:
--------
Rais Uhuru Kenyatta...
Ni mawazo yangu tu kwamba katika familia au nchi huwezi leta maendeleo wewe baba au mkuu wa nchi kwa kuwakandamiza unaowaongoza. Mfano, mtoto wako anakosea unampa adhabu asiende shule. Mfano mwingine ni mkuu wa nchi au kijiji anasema hataki watu wake wajadili utendaji wake, sasa nani atamshauri...
Naomba kutahadharisha kuwa ni muda mrefu NIDA imekuwa ikisuasua kutoa IDs kwa sababu ya ukata. Sasa naona wamekuja kivingine kuwashirikisha SSRA ili mifuko ya hifadhi ya jamii ndiyo itoe fedha za kugharimia. Kimsingi ni fedha za wanachama ndo zinatumika. Hapa nachelea kusema ni bora serikali...
Samahani wana jamvi,
Ukiweka mada yoyote hapa jF isiyo ya ngono, mapenzi, au udaku haipati wateja. Lakini ukiweka mada inayoendana na hayo niliyo yataja, utashangaa inavyopata washabiki. Je, hivi vijana wa kitanzania mnayoyafikiria ni mapenzi tu? Au JF imevamiwa na wageni zaidi?
Inanishangaza...
Naomba kutoa wito wangu kwa wizara ya maji kwamba ni wakati sasa ifikirie kuchukua maji mto rufiji kwa ajiri ya wilaya za Ilala, Temeke, Mkuranga, Rufiji, Ikwiriri, na maeneo jirani. Nasema haya kwa sababu mto Ruvu umeelemewa na kina chake ni kidogo kwa hiyo unaweza hudumia wilaya za Kibaha...
Nimesoma kwenye RT.com na kukutana na story inayohusu msichana wa kitanzania angalau aliyeelimika kuthamanishwa na ng'ombe watano. Kwa habari zaidi soma hapa chini.
Nadhani ni wakati sasa mambo ya mahari tukayaacha na tukawekeza zaidi kwenye heshima ya utu wa mtu.
=======
More than a third...
WanajF,
Mimi nakereka sana kuona miji ambayo iankua kwa kasi kama Morogoro bado mamlaka husika hawajiongezi na kupeleka huduma za jamii kama maji kwa haraka kabla maeneo mengi hayajawa over-populated. Mfano ni eneo la Kihonda na kuelekea kata ya Lukobe na maeneo jirani. Katika kata hii hakuna...
Nadhani baadhi ya watendaji wa CRDB Bank watakuwa members humu Jf. Nawaomba simu zao za huduma kwa wateja watwambie kama hazitumiki basi waziondoe. Kwanini mnamsubirisha mtu kwa dakika 7 wakati analipia hiyo simu??
Naomba kushauri kwamba vyombo vyetu vya ulinzi viangalie kwa makini vurugu za Tanga kama zina uhusiano na mradi wa bomba la mafuta la Uganda - Tanga. Wakumbuke hoja mojawapo ya kuacha njia inayopita kwa jirani ilikuwa ni ukosefu wa usalama.
Sasa nawasiwasi kuwa inawezekana kuna watu...
Nimelazimika kuandika ujumbe huu baada ya kuona yaliyotokea wakati wa uchaguzi na hata mpaka sasa. Polisi yetu imatumia nguvu kubwa kweli kupambana na masikini wapiga kura wenye hamu ya kumchagua kiongozi wao wampendaye.
Mbaya zaidi ni pale wanapotenda kazi zao kwa maagizo ya kisiasa zaidi ili...
Nawakumbusha wamiliki wa mabenki nchini kwamba kila kipindi anapokuja raisi mpya kunakuwa na matukio mengi ya uvamizi wa mabenki. Kumbuka mwaka 2005 tulishuudia benki nyingi zikivamiwa wakati huo Mahita akiwa IGP.
Mwaka 2010 uvamizi haukuwa mkubwa kwa sababu raisi aikuwa na kila dalili za...
Bandugu naomba kujua ni kwa nini marekani ilifikia hatua ya kutumia bomu la atomic huko Japani?
Na kwa nini Japani hakulipiza kisasi? au walikubaliana nini hasa mpaka wajapan wakaridhika?
Ni hayo tu.
Naomba Kilwa Mkuu wa wilaya katika wilaya yake amwagize afisa elimu (W) ampe idadi ya madawati yanayohitajika katika shule zote wilayani. Baada ya hapo amwite mkurugenzi wa wilaya/mji/manispaa pamoja na mkuu wa idara ya ujenzi na idara ya misitu na mkuu wa idara ya mali asili.
Kisha awaagize...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.