Wadau, nahitaji mchango wenu, kwa yeyote anayejua kuhusu Sera ya Kilimo na Mifugo nchini, je, imefanya kazi ipasavyo? Imewanufaishaje Watanzania hasa wale wa makundi yaliyosahaulika ama yanayogandamizwa katika jamii kama wanawake? Bei za mazao zinawiana na gharama halisi za kilimo? miundombinu...
Jamaa anafaa, lakini ajaribu kuondoa mnato ingawa naamini ni hulka ya kuzaliwa wakati mwingine. public post inahitaji kuwa social, vinginevyo nafasi inaweza kukushinda, hasa kwenye sekta ya umma ambako masufuria na majungu ni mambo ya kawaida. usije ukasikia "wee mtoto, siye tuko hapa tangu...
Bahati yake jamani, maana mwaka jana aliikosa ile post ya ukurugenzi pale utalii kumrithi babu wa tanga. hongera baghosha ng'wana wane, matunda ya pugu hayo, au siyo
Sitaki kuamini kama hizi ndizo zama za yule mnyama 666!!! Yule ambaye anatajwa na manabii kuwa ndiye chukizo la uharibifu, ambalo sasa limekwishakaa mahali patakatifu...
yawezekana ni majungu hasa tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu. lakini wadau, ni kweli haya mengine yaliyosemwa i.e kushawishi mgomo wa wanafunzi wa chuo kikuu 1966 kupinga jkt na kuunga mkono serikali ya tanganyika ndani ya muungano? pengine wenye data wanaweza kutujuza ili tumwelewe vizuri...
Tusipime homa kwa viganja jamani. Siku hizi jua kali hivyo joto la mwili nalo linazidi. Vivyo hivyo, Six naye hana namna zaidi ya kuwa upande wa mapambano, na hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kuomba ridhaa ya wananchi tena. unadhani angezima hoja za ufisadi bungeni angeweza kukaa mpaka sasa?
Hii ni kukatishana tamaa. Mwenzetu ameleta hoja ijadiliwe, hajasema fulani na nani anafaa ama hafai. ni wakati wako wewe kutoa mawazo yako kuunga mkono mjadala.
Mkuu nakukubali sana, yaani umechimbua mambo ambayo wengine wetu hakuwa tunajua. Sasa, hivi ni kwanini hawa jamaa imani yao haiwataki wanawake? kwani wanawake hawastahili kuabudu? na labda niulize, maana aulizaye ataka kujua ati! hivi wao nao wana kitabu chao cha ibada mbali ya biblia na qur'an...
Sielewi unashangaa nini hapa. hivi kelele zote ambazo huwa zinapigwa kwamba kura zinaibwa huwaga huzisikii wewe? kusambaza kadi feki si jambo gumu, hata wewe unaweza kwenda kwenye chama chako na kuwaambia viongozi wako kwamba umewahamasisha wananchi wajiunge na chama hicho, hivyo unaomba kadi...
Hii nzuri, tunahitaji kujifunza kwa wanahistoria watueleze, maana waarabu waliokuja tangu enzi hizo za ukoloni tunaviona vizazi vyao wengine wakiwa hata ndani ya serikali yetu. ina maana waafrika wamebadilika ngozi na kuwa weupe?
Pengine ndiyo maana Shamsa mwangunga amejitokeza kutaka kuwania jimbo hilo. lakini mwanamama huyu aliyeshindwa kusimamia maliasili na utalii, kweli ataliweza jimbo la ubungo kama siyo kuwa mwepesi kwa 'mwenye jimbo hilo anayependwa' kijana mnyika? kundi lake linaonyesha kuwa na nguvu ya...
kwa kweli huu ni mtandao mwingine mchafu unaozidi kuua mashirika yetu na kupukutisha hata senti kidogo ambazo zingefaa zingie kwenye huduma zetu za jamii. lakini siamini kama takukuru wana meno ya kung'ata, i mean, wao wako clean kiasi gani kumfunga paka kengele?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.