Uchaguzi wa ngazi ya taifa ndani ya CHADEMA umeshabisha hodi. Hodi hiyo watoa paruwanja vijana 10,000 wa CHADEMA hadi sasa wameshasaini waraka wa kumtaka Mbowe agombee uenyekiti wa CHADEMA. Aidha vijana hao wanataka kuchanga fedha kwa ajili ya kumchukulia fomu bwana Mbowe.
Hili si jambo zuri kwa...
Dhahiri katiba yatupa haki ya kukosoa, kuhoji na hata kupinga mawazo ya kiongozi yeyote ila haitupi uhuru wa kumtukana, kumkashifu na kutumia lugha ambayo ni dhahiri ya kuudhi.
Tunapopinga vitendo vya utekaji, pia tupinge vitendo vya kutumia lugha za kuudhi dhidi ya wenzetu. Maana kukosoana kwa...
Wajomba na mashangazi,wazee mabarobaro,
Pana fungu la ghawazi, latumiwa na kigaro,
Hununua waziwazi, wanati kama nduaro.
Yale yake maongezi, yamejaa chinjarero,
Kanaswa na hajiwezi, kama nswi kwenye vyero,
Ni wa hovyo utetezi, amefanywa nini sero?
Jamani ndarama hizi, zilizo fungasha ziro...
Ziara ya ndugu Zitto, kwenye kata mikoani,
Imetufumbua mato, na kututoa gizani,
Jamani wetu watoto, wana khofu darasani,
Wanasoma vichakani, ingawa elimu bure.
Ziara ya ndugu Zitto, kwenye kata mikoani,
Imetuonesha ndoto, za watoto zishakani,
Kusoma kwao kuzito, hali mbaya si utani,
Vumbi mpaka...
Wamama na kina baba, ninayosema sikia,
Mwana kumwita Msiba, ni tabu kumtakia,
Atakuwa na uhaba, wa akili nawambia,
Mfano ni huyu daba, uchao atubwatia.
Mtoto kumwita Pombe, haifai zingatia,
Aweza kuwa mzembe, mwenye kinyaa kutia,
Ama akaota pembe, na watu akapigia,
Pengine akawa hambe, mwepesi...
Baba huyu wa wanyonge, nadhani wote twajua,
Ajabu, wacha nilonge, nipate kuwazindua,
Mnyonge bado mnyonge, hali hata kitumbua.
Baba huyu wa wanyonge, majipu ayatumbua,
Ajabu malengelenge, pamoja na visunzua,
Aviwacha vijijenge, na sasa vyatusumbua.
Baba huyu wa wanyonge, hivyo kajipambanua...
Siasa kwa mwanasiasa ni kazi, kama ilivyo biashara kwa mfanyabiashara na kilimo kwa mkulima. Zitto Z Kabwe akikaa mahabusu kwa makosa ya kisiasa ni sawa sababu ni kiongozi wa chama na siasa kwake ni kazi. Hii haina tafauti kwa mkulima kugongwa na nyoka shambani au kwa malaya kupata HIV, naam...
LEO NAWATUKANA!
1
Sianzi na ashakumu, leo ninawatukana,
Mwaufanya uwazimu, na mambo yaso maana,
Huu si ubinadamu, pia siyo uungwana,
Ben wetu yuko wapi?
2
Ben hakuwa mzimu, vipi asionekane?
Kama karuka sehemu, uhamiaji wanene,
Na kama ni marehemu, mwili wake tuuone,
Ben wetu yuko wapi?
3...
Mtu timamu hawezi kukataa salamu, na hapa ndipo nilipogunduwa huyu siyo kiongozi bali kidudumtu cha kwenye kisamvu, na kwa vitendo vyake ndiyo aichimbia kaburi CUF, inshallah ataingiya yeye na husuda zake na hao wanamtia wazimu aso kuwa nawo.
Aiwache CUF na aanzishe chama chake kama azani chama...
Kwako Mh Msigwa.
“JPM hana sababu ya kutoa sababu kwa nini amewateua KITILA NA ANNA, Sina uhakika kama waliwahi kuwa wapinzani au walikua na kazi Maalum?”
Hayo ni maneno yako Mh Msigwa, ni vijembe na uchokozi kwa viongozi wetu na chama chetu, na siku zote nyie CHADEMA ndiyo munatuanza...
CHADEMA IMENUNULIWA, UKAWA IMEKODISHWA, BORA LENDE!
Naona kuna upotoshaji mkubwa unafanywa na watu dhidi ya chama chetu cha ACT, nafikiri kuna haja ya kuweka mambo sawa au kukumbushana tu, sababu kwa watu kusahau kwao kunapelekea wakishambulie chama chetu.
Na siku zote tumekuwa waathirika wa...
LEO NAKUTUKANA.
Siandi na ashakumu, leo ninakutukana,
Nikutukane dhalimu, katiba unayechana,
Kwa hii yangu kalamu, yeo mengi nitanena,
Tangu ushike hatamu, na sheria wakinzana,
Kiti unakidhulumu, hishima tena hakina,
Nauliza nifahamu, nipa jawabu la kina,
Mfalme waenda wapi?
Mawaziri...
NISIKIZE RAIS.
1.
Kuna mambo kiongozi,
Nataka kukuusia,
Hiyari kuzingatia,
Ama kuyapuuzia.
2.
Kuna mambo kiongozi,
Usiseme waziwazi,
"Imekuwa kubwa kazi"
"Sina namna siwezi"
3.
Kuna mambo kiongozi,
Kutamka hutakiwi,
"Tuendapo sipajuwi"
"Nimekwama sielewi"
4.
Kuna mambo kiongozi,
Siyanene iwe...
Mapema mwaka 2015 Gwajima akiwa katika jukwaa la siasa pamoja na Dk Slaa alisema kuwa Dk Slaa ndiye Joshua atakayeivusha Tanzania kwenda nchi ya ahadi.(Kaanani)
Alipotabiri hivi, juu ya Dk Slaa na kuutangazia umma, CHADEMA walimshangilia, na waliuunga mkono ule unabii. Huku kwenye mitandao Dk...
Hatua za bunge la Tanzania dhidi mkuu wa mkoa wa DSM zinatuthibitishia UGUMU wa VITA ya MADAWA ya KULEVYA ulivyo si Tanzania tu bali dunia nzima.
Jiulize kwanini nchi kama Marekani yenye kila aina ya tekinololijia ya usalama na vifaa vya usalama lakini MADAWA yapo na yanauzwa kama njugu...
UMARIDADI WA PAKA.
Umaridadi wa Paka, si lolote ni ujinga,
Kote atarukaruka, haja kubwa kwenye unga,
Poleyo unayepika, bila kuanza kuchunga.
Paka wako mshirika, ulomliya amini,
Pamoja wote mwapika, na moya yenu sahani,
Moyoni alofutika, ujuwe hutaamini.
Hasira zake mkizi, si lolote upumbavu...
ANA MAZONGE MFALME.
Mfalme ana tenge, leo nawapa hadhari,
Ndimi zenu muzichunge, hizi zama za hatari,
Lakini musimvunge, kwa kupamba taksiri.
Mfalme ni mazonge, chukuweni tahadhari,
Mamboye musiyapinge, ila sifiche dosari,
Mulimzoea kenge, huyu nyoka wa hatari.
Mfalme ana singe, naomba...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.