Kama unahisi ni kufuja, hamasika na ww siku moja uwe prof. Hayo mengine hawapewi. Hata mshahara usiseme wanalipwa mishahara mikubwa. Hata hiyo laki sita kwa ajili ya nyumba usiseme ni hela kubwa. Naomba nikuulize swali dogo tu. Naomba uniambie bei ya kupanga nyumba hata ya vyumba vitatu au vinne...
Huyu mtu aliyeanzisha hii thread ameianzisha kwa nia ya kupotosha. Kwanza hakuna profesa hata mmoja anayeishi kwenye hizo nyumba mia tatu. Ni uongo tu ameamua kukuza habari
Jamani tusiwe wepesi kuwaita wataalam wetu majina yasiyofaa. Kumbuka muda na nguvu inayotumiwa na hawa watu mpaka kufikia hatua hii ya uprofesa. Mbona hiyo ni hela ya kawaida ukilinganisha na maslahi ya waheshimiwa wengine
Tuache kuudanganya umma wa watanzania kuwa kuna profesa au Dr aliyefukuzwa kwenye nyumba ili kupisha waheshimiwa. Kwanza kwa taratibu za utumishi wa umma profesa na senior lecturers wote ni lazima wapewe nyumba za kuishi. Hata pale wasipopatiwa nyumba wanalipwa pesa kila mwezi ili kulipia makazi...
Hali ni mbaya kwa waathirika wa tetemeko. Nashauri serikali ianzishe madaftari ya rambirambi katika wilaya zote nchini ili watanzania tutoe tulichonacho kuwasaidia wenzetu. Hili litasaidia sana kama likisimamiwa vizuri. Hali ni mbaya jamani. Michango hii inaweza kuipunguzia serikali mzigo huu...
Naomba serikali iangalia namna ya kupangua hoja zilizojengwa na majirani zetu ili tu majirani hao kuhakikisha bomba linapita kwao. Hili bomba lina manufaa kwa nchi . Nashauri serikali iangalie maeneo ambayo inaweza kuwapunguzia hawa wawekezaji au kuwamotivate ili bomba hili lipite hapa. Biashara...
Jamani wizara ya afya tusaidieni kutumbua jipu hili watu tunaathiriwa na hawa wanaovuta hovyo. Ukipita njiani huku mijini unapishana na watu wanavuta ovyo. Kwenye bar ndo kabisa wanapokezana. Kwa nn wasiwekewe utaratibu maalum ili hata wanapovuta wasiathiri wenzao? Wizara ya afya hili ni jipu lenu
Mimi nashangaa kitu kimoja. Hivi mbona marais wa Kenya, uganda Rwanda nk wanapoongea kiswahili wakakosea mbona hatuwasemi kwamba hawajui kiswahili. Ukweli ni kuwa rais kwa lugha yoyote atakayoongea ujumbe lazima uwafikie walengwa. Kumbukeni ni nchi ngp zimeendelea bila hata wananchi wao kujua...
Jipu la NHIF likitumbuliwa itakuwa safi kabisa. Watu tunakatwa hela kubwa ila tuko restricted kuweka wategemezi. Mfano mimi nakatwa laki moja kila mwezi hapo bado mke wangu na bado za mwajiri. Lakini wazazi wangu wakienda hospitali huko mikoani waliko madaktari wanawaangalia shingo upande...
Tena TRA wawe macho na private sector kwenye suala la kodi. Ngoja niwape mbinu moja maana mi pia niwahi kufanya kazi huko. Twende moja kwa moja shule za private. Unakuta mfano mwl analipwa jumla milioni moja ila mshahara anaandikiwa labda 250,000. Nyingine inayobaki wanaandika eti ni allowances...
Acha wafanyabiashara walipe kodi. Mi ni mtumishi nakatwa laki tano kwa mwezi kwa mwaka milioni sita. Mfanyabiashara anayelipa hyo kodi najua nikionyeshwa biashara zake ni mamia ya mamilioni. Acheni kulalamika wafanyabiashara tujenge nchi yetu
Mi nashangaa sana mtu mzima mwenye elimu anapokuja na hoja za ubaguzi wa watanzania huku amesoma na anaijua historia ya nchi yetu vizuri. Tanzania ina makabila 120 na zaidi. Hivi kila kabila tukisema lazima litoe waziri na katibu mkuu nchi itatawalika? Mi ni mhangaza na kabila langu halijawahi...
Mh Rais nakupongeza kwa kuwa na ubunifu wa kuona kuwa Siku ya leo watanzania wote tufanye usafi. Niko safarini kutokea Dar kwenda mkoani ila suala hili limepokewa vzr na watanzania maana ktk maeneo mengi ya Dsm usafi unaendelea. Hata hivyo mh rais naomba uitangaze kila jumamos ya mwisho wa mwezi...
Napenda nitoe ushauri wangu juu ya namna ya kuwafanya watu wawe na kasumba ya kudai risiti. Nashauri serikali itumie vyombo vyake km TRA na vingine kuwa wanafanya ukaguzi wa kushitukiza kwenye magari binafsi na daladala kukagua bidhaa zilizonunuliwa na mteja na kudai mnunuzi aonyeshe risiti...
Mi nadhani kuendelea kuwekea vikwazo vya hapa na pale upinzani na hasa ukawa tunawapa umaarufu bila sbb. Wangewaacha tu waendelee na mambo yao. Watu wanaweza kutengeneza huruma na kujikuta Ukawa unazoa kura. Nakumbuka huruma ndiyo ilmsaidia Zuma
Jamani Dr, Magufuli ni mtu makini na amefanya kazi ya kuonekana naomba watanzania tumpe nafasi. Sisemi kwamba EL si mchapakazi hapana. Sema hofu yangu anatumia nguvu kubwa kuusaka urais.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.