Sioni ni tatizo! Huu utaratibu upo kwenye nchi za watu na hasa ambazo zinatupa misaada. Kama ulifatilia kampeni za Obama utakuwa shahidi wa hili (donation ilikuwa inaanzia USD 10 na kuendelea) na ilikuwa kwa wamarekani na wasiokuwa wamerekani na sasa wanaendelea kutoa donation kwa health...
Kikwendu na Prof. Maji Marefu nani zaidi? na wengine unaowajua wewe kupitia nyinyiem. Nasikia kuna mmoja kabla ajaanza kuact bongo movie alikuwa anafanya biashara ya naniiiii!
sitaki kujua kama kuna ukweli ndani yake ama la! Ila tatizo ni nini mpaka ulete mada hii? Kuna tatizo mwanaume kuzaa nje ya ndoa kama ameamua kufanya hivyo? Huyo mheshimiwa mkuu wa kaya ana watoto wangapi nje ya mke au wake zake halali? Umetumwa kupost au ni akili zako mwenyewe??.Inasikitisha sana.
IMED tumeanzisha BRIDGE Program kuwapatia vijana waliomaliza vyuo ngazi zote fursa kufanya kazi kwa miezi 6 sehemu mbalimbali kwa kujitolea kujenga uzoefu na kuonyesha umahiri wao. Pia watapata mafunzo kuwawezesha kuthaminiwa zaidi na waaajiri au kujiajiri. Chukua tangazo na fomu kuomba...
na wewe ni mmojawapo au ndio wale vijana walioandaliwa na Mwiguru kwa kuwavisha combat za CHADEMA ili kuwaaminisha watanzania CDM ni chama cha vurugu. Kama haupo kati ya vijana wa Mwiguru umeyajuaje hayo? Vijana tuache kutumika kwa njaa zetu na kwa manufaa ya wengine ambao wanajielewa...
Kwani CDM anakusanya kodi au anaongoza serikali? Nina mashaka na upeo wa uelewa wako kuhusu uendeshaji wa serikali. Ulishampa nchi CDM akashindwa kutatua kero za wananchi? CCM ndio imeunda serikali lakini uwezo wa kutatua shida za wananchi ni chini ya 40%.
Unaomba msamaha na ndani yake unapiga majungu yasiyokuwa na tija kwa kuongea mambo ya kinafiki. Kitendo hicho si cha kiungwana bali unadhihirisha ni jinsi gani unavyotumika pasipo kushughulisha akili yako.
Ndio mlivyoambiwa mlivyoenda kwenye kikao chenu kilichokuwa kinaongozwa na Wasira na nyinyiem wengine kwa kutumia mabasi ya chuo cha UDOM? Tumeyasikia yote mliojadili uku wengi wa wanafunzi walioudhuria walikuja kuchukua posho na pia nasikia walikuwa wanawapigia makofi akili ndogo kwa...
Usiongee maneno usiyokuwa na uhakika nayo ndugu, uchaguzi wa 2010 makanisa yalizuia waumini kufanya kampeni za aina yoyote katika maeneo yanayozunguka kanisa ila kwa upande wa pili hali ilikuwa tofauti. kauli zako ni zi zakichochezi waziwazi tafuta point nyingine ya kumuusisha Dr. Slaa na udini...
mimi nilifikiri unaniambia ccm wametekeleza ahadi zao lukuki walizotoa 2010! Kumbe kama kawaida yao wamesomba watu kwa magari na kuwakalisha kwenye viti kwa posho ya elfu 5 na pia kuwadanganya na wabana sauti wa bongo flava? Kwa akili ya kawaida inasikitisha sana na sikutegemea kwa kijana wa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.