Habari wana jukwaa. Mnyonge mnyongenj, haki yake mpeni.
Natoa pongezi nyingi sana kwa Mh Waziri Kangi Lugola kwa uamuzi wake uliojaa utu na busara wa kuwaagiza Ma RPC kutozuia mabasi kutembea usiku kwa sababu za kiusalama.
Uamuzi huu unapaswa kupongezwa kwa sababu umetuondolea aibu kama Taifa...
Ndg wanaJF naombeni msaada wenu wa mawazo na wa haraka juu ya tatizo lifuatalo.
Nimejiwa na rafiki yangu asubuhi na mapema leo kuniomba ushauri ambao kutokana na ugumu niliokutana nao, imebidi nije hapa jamvini kuomba mchango wenu wa mawazo ili nami niweze kumsaidia huyu ndg.
Issue yenyewe...
Katika siku ambayo mwili umesisimka kwa uzalendo ni leo baada ya kusoma msimamo wa mzee wa Upako kuwa Tanzania ni BORA KULIKO UKRISTO NA UISLAM. Ahsante kwa kutukumbusha.
Jamani kwa hali ilivyo Loliondo, natamani kuona jinsi kampuni ya kwanza itakayo instal mawasiliano kwenye kijiji cha Samunge. Swali, je ni kampuni gani ya simu hapa tz itakayokuwa ya kwanza kujenga mnara wa mawasiliano huko Samunge kwa jinsi wanajf mnavyoyaona makampuni hayo. I, humbly submit.
Kuna jamaa yangu kaniomba ushauri juu ya tatizo linalomkabili. Yeye kaoa mke. Baada ya kufiwa na mdogo wake wa kike, ndugu waligawana watoto wa marehemu na yeye(jamaa) akapewa mtoto m1 ili amtunze na hasa ikizingatiwa kuwa hakuwa na baba. Matatizo ya mke ndo yakaanza. Mara simtaki huyo mtoto kwa...
Wana jf, hivi kwa sasa tunahitaji Katiba mpya kwanza au tunahitaji kufanyika kwa mijadala rasmi juu ya Katiba mpya. Nimeulilza hivi kwa sababu kuna watu wanataka tudai Katiba Mpya bila ya kujali kuwa hakujawahi kuwepo kwa mjadala rasmi juu ya Katiba mpya. Tusipoiona haja ya kufanyika kwa...
Wanajf na wapenzi wa mpira wa miguu, naamini kuwa sote ni wenye furaha baada ya ushindi wa timu yetu. Hata hivyo naamini kuwa ushindi huo hautakuwa na maana yoyote, iwapo Tanzania haitakuwa bingwa wa Tusker Challenge Cup kwa 2010. Kwa kuwa kushinda au kushindwa kwa Stars hapo kesho ni furaha au...
Wanajf kama kuna mtu anafuatilia mtiririko wa matukio atakubaliana nami kuwa mwaka huu Senene zimekuwa nyingi mpaka hata zikidondokea kwenye glass ya bia hazifi. Je hii ina maanisha nini. Kwa wenzetu wa Bukoba watakuwa na jibu. Naombeni mtujuvye.
Wanajf poleni mihangaiko ya life. Mimi ni husband wa somebody. Tumejaliwa watoto wa4 lakini wote ni wa kiume. Kwa kuwa jitihada zetu za kupata baby girl zimeshindikana, nawasilisha ombi kwa mwanamke yeyote aliyetayari kunizalia mtoto wa kike. Lakini awe pia na nia kama ya kwangu na uwezo wa...
Darling
Nadhani sasa ni miezi inayokaribiana na mwaka tangu tumeanza uhusiano wetu wa kimapenzi.Ndani yake tumefaidi mengi kutoka pande zote.Tumejifunza mengi. Tumefanya mengi.Tumeona mengi.
Darl naomba nikiri kwamba moyo wangu wa baridi juu ya mapenzi ya kweli ni wewe ndiye uliyeufanya ukawa...
Wakuu heshima mbele.
Kwa masikitiko makubwa,
Na kwa haki yangu ya Kikatiba ya kutoa maoni.
Naomba kutoa mtazamo wangu juu ya huduma zitolewazo katika Hospitali ya Mwananyamala.
Kwa sasa limekuwa jambo la kawaida kusikia katika vyombo vya habari kuwa kuna mjamzito amepatwa na tatizo la...
Mimi ni Mswahili mzaliwa wa Bongo. Naomba kujitokeza kwa mara ya kwanza katika Forum yetu adhimu kutafuta rafiki wa kawaida. Sibagui dini wala kabila.
Sifa za rafiki anayetakiwa.
Awe mpenda kiswahili.
Awe mhalisi na mpenda ukweli.
Awe mpenda nchi yetu lakini asiwe kama Ngwangwa ak.a...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.