Tusijisifu wakati tunaona mapungufu makubwa bado, tunao uwezo wa kuwa wa kwanza Afrika - dhahabu, almasi, tanzanite, uranium, gas, nk na uwezekano wa kupata mafuta, ardhi kubwa na nzuri; mito yenye maji muda wote, maziwa na bahari, misitu nk hata maeneo ya ukame tungeweza kuyabadili yakafaa kwa...
wanaokamatwa wanatumwa tu kama unavyoweza kumbebesha punda mzigo, unfortunately wanabeba pia "risks" zinazoambatana na kukamatwa wakati wenye mzigo wametulia kwenye kiyoyozi wakiangalia luninga!! tamaa ya pesa za haraka - Big Results Now
Ukweli tukiwa makini na kuwa wakweli wa dhati, katika hao hakuna rais hapo! Ni lini Tanzania tuipendayo itapata raisi mwenye nia ya kuendeleza watanzania badala ya kujinufaisha binafsi? Mwalimu alisema ikulu ni mzigo, mnakimbilia nini huko? Wanaokimbilia waogopeni kama ukoma! Tunawaogopa hasa...
Mwanadiwani
Hamjathubutu wala kuweza lolote, nchi imezidi kudidimia wakati Ina utajiri lukuki, hii si karne ya kuwa na Shule zisizo na madawati wala walimu tunabaki kujisifu kwa idadi ya shule na watoto walioandikishwa matokeo yake wanamaliza std 7 hawajui kusoma wala kuandika. Hii si karne ya...
Kuna haja kubwa kudhibiti hii milipuko inayoua raia wasio na hatia tena wakiwa katika kutimiza haki yao kikatiba, kabla ya kufikiria kupeleka majeshi DRC, Darfur, nk.
Kila mkoa una historia, iringa watadai mkwawa alipambana na wakoloni, historia hiyo! Kule kilimanjaro chifu Mandara, historia hiyo! Vita ya majimaji nayo historia! Kagera nako chifu Rumanyika, tutakuwa na makao makuu kila mahali kihistoria, ingiza hoja ingine
Dodoma yenyewe bado tunasuasua hatutaki kutoka Dar, nani hataki kuangalia meli zikiingia na kutoka? Tunazo tena upya Tabora? Nako tuweke mamlaka ya kujenga mji Mkuu? Bunge? Nk kwa uchumi upi? Maana tulionao tumeshindwa kuusimamia vizuri
Inahitajika kukaa na wananchi na kusema nao kwa kina,, shida ya politicians ni kujaribu kuleta suluhu kisiasa badala ya kiuhalisia na inawezekana wananchi wa mtwara wanaona wamepigwa changa la macho Ktk ahadi za uchaguzi ndio wanakuwa mad. Kuhusisha na upinzani kisiasa ni kuhafifisha uwezo wa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.