Mkuu ndio maana mnafeli mitihani kwa kutoelewa kilichoandikwa, wapi pameandikwa Magufuli ndie aliyemtengeneza huyo unayemsema? rudia tena kusoma ndio utajua aliyeandika anamaanisha mtu huyo uliyemuandika na sio Magu! Unakurupuka na mambo ya ukabila wakati hata andiko hujalielewa.
Hah hah hawa wote ni team Mbowe, wengi wao nawafahamu kindakindaki, hii Chagga Development Manifesto itabaki mali ya Dj Kim Il Sung, mwenyekiti wa maisha.
Kwani kuugua UKIMWI ni dhambi sijui kwanini watu mnaogopa kusema marehemu kafa kwa UKIMWI? Raisi Kaunda na Mandela waliwahi kutangaza kuwa watoto wao wamekufa kwa UKIMWI, kusema mtu kafa kwa UKIMWI si dhambi na kifo kipo tu hata ukisema au usiseme kuhusu Ukimwi siku ikifika utaondoka tu. Kuogopa...
Hawa wengi wao elimu zao za magumashi sema tu wanabebwa na ma Godfather wao wengi wao wamesoma hapo IFM, diploma za Banking wakawa chawa wa maMD waliokuwepo enzi hizo na kukabidhiwa vijiti vya u CEO, utaona mtoa CV hajaandika shule na vyuo alivyosoma, wapo wengi kwenye taasisi za kifedha hasa benki.
Mwenyewe nilikuwa naenda USA enzi za Trump utadhani naenda Kibaha,hakukuwa na shida yoyote baadae ikaingia Corona ndio nikaacha kwenda, panapo uhai mwakani natia tena timu USA.
Kaka unajidanganya tu, wenzako hawatumii au kuweka benki hizo pesa zetu za madafu, wenzako wanatamba na USD$, hizo pesa za madafu ni za mboga na kuwanunulia nyama choma wajumbe,kwa hiyo hawaathiriki kwa lolote,pia wenzako wana akauti zao ughaibuni, tena akaunti za USD$.
Kwenda Staten ni ferry boat ya bure, zina rangi ya njano,ukiwa Brooklyn bridge na Statue Of Liberty unaziona zileee, Queens ndio nyumbani asilia ya mwamba Trump
Miaka ya nyuma Alaska ilikuwa Urusi,miaka ya nyuma Marekani ililinunua jimbo hilo kutoka Urusi na hata waziri wa fedha wa marekani wa miaka hiyo alilaumiwa sana kwa uamuzi wa kutoa pesa kununua jimbo hilo na wananchi wa Marekani, lakini baadae uamuzi huo umeinufaisha Marekani kwani Alaska ina...
Sasa analia lia nini kama hana njaa, yeye alimfukuza dereva aliyekataa kupanga mafaili bila sababu za msingi,wacha apate ukichaa kwa kulialia kila kuchwao, maisha si lazima uajiriwe, kuna lundo la watu wameachishwa kazi zao na hatuwasikii kulialia mitandaoni.
Sea boyz Magomeni, Kariakoo karibu na msikiti wa Manyema, Morogoro rd karibu na kituo cha mafuta opp na Mtendeni Pr Schoo, Posta Kisutu na mwisho kabisa Stambuli Cafe millenium tower Makumbusho. Nyingi ya hizi cafe zilimilikiwa ama na wahindi au waarabu. Mimi nilijifunzia kompyuta kitambo sana...
H
Huyu comrade sijui huwa anaongea na nani kwa maana wenzake na marafiki zake karibu wote washatangulia mbele za haki, labda waliobaki ni mzee mwenzake mlamba asali, BT, na bwana tembo na hawa wote wamestaafu japo wengine ni wastaafu wasiotaka kustaafu!
Waliokuwa wanasoma shule private ni wale waliofeli mitihani ya kuingia kidato cha kwanza na kidato cha tano, enzi hizo walikuwa takataka, wengi wao walikimbilia shule za seminari, pale Mbeya tulikuwa na Sangu Secondary School, na Darisalama palikuwa na Kinondoni Muslim, kule Kilimanjaro boys'...
Mkuu mbona unaandika uongo, kwa taarifa yaks huyo kiongozi wa Hamas hakuvamiwa wala kushambuliwa na waty,aliuwawa kwa bomu giliotegwa chumbani mwaka miała miwili iliyopita, kosa alilolifanya mheshimiwa marehemu ni kawa anafikia sememu hoyo hoyo mara ajapo Tehrani, Mossad kwa kutumia waty wa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.