Kwa mazingira ya kisiasa ya sasa nchini ni kujidanganya kuwa kiongozi wa upinzani anaweza kuwa Rais kupitia njia ya kura. Kwa hiyo yeyote aliyetarajia kuwa Dr. Slaa angekuwa Rais ama hayafahamu vizuri mazingira halisi ya kisiasa au anajidanganya kwa kujipa matumaini 'hewa'. Haiwezekani kuwa Rais...
Hii tabia ya viongozi wa CHADEMA kuvaa kama mgambo itawapunguzia kura....kwa mwananchi wa kawaida .... mgambo ni alama ya unyanyasaji kutokana na wanavyotumika ingawa lengo la kuanzisha mgambo lilikuwa zuri.
Simpo....kama PhD haitambuliki...acha kutumia u-dokta. Kama wahusika waliwasilisha nyaraka feki, kamata hiyo mutu na fukuza kazi. Kama vetting process ni porous...timua hao vihiyo wanaofanya vetting....hivyo ufumbuzi ni simpo...TIMUA, TIMUA ndo heshima itarudi.
Tumekuwa na utamaduni wa kuwa na kamati kibao lakini huwa hakuna hatua madhubuti dhidi ya watuhumiwa wa ubadhirifu wa mali za umma. Ifike mahali watu wawajibishwe badala ya kuwa na longolongo tu.
Tatizo ni kusema lililo bayana.....nani asiyejua kuwa JK anachekacheka? Tumerithi tabia ya kutukuza viongozi hata kama wanatupeleka kaburini. Tulipokuwa wadogo tulikuwa tunafundishwa kusema "zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa chama"....ilikuwa mwiko kupinga 'fikra sahihi" za mwenyekiti huyo...
Hii no hoja dhaifu mno. Hivi mtoa mada unatarajia kuwa kila sekta idadi ya waislamu na wakristo kuwa sawa? Ni kitu ambacho hakiwezekani kwani nafasi za kazi hazijazwi kuzingatia dini ya mhusika bali sifa za kitaaluma na ujuzi. Serikali inaweza kwa makusudi kabisa kujaribu kuoanisha uwiano huo...
Biashara ya utumwa ilifanyika miongo kadhaa iliyopita (inasemekana bado inafanyika baadhi ya maeneo duniani) na kusababisha watu weusi kuenea maeneo mbalimbali duniani mfano visiwa vya Carrebean, Amerika ya kusini, Marekani na kwingineko.
Nimesoma kuwa watumwa wengi kutoka Afrika Mashariki...
Wakazi wa Kipawa wamwambia DC Ilala hana adabu
WAKAZI wa Kipawa jijini Dar es Salaam wamemsikitisha Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Evance Balama baada ya kumwambia kinagaubaga kuwa hana adabu.
Wananchi hao, walitoa kauli hiyo juzi ofisini kwa mkuu huyo baada ya wananchi hao, kuandamana hadi ofisi...
Tatizo ni watu wengi kukubali hizi dini za mapokeo na kuzitukuza kushinda hata wenye asili ya hizo dini. Nani anayeamini katika upendeleo kwa Mwenyezi Mungu? Vyote ni viumbe vyake, uwe mswahili, mwarabu, myahudi, mkavirondo, mdosi, mchina n.k. Kabla hao waarabu na wazungu hawajaingilia imani...
Hapo kwa ufupi CHADEMA wamechemsha! Hata mkiwatetea vipi...inaelekea uongozi wa juu wa hiki chama ni kwa ajili ya watu fulani ndo maana wanarithishana kama usultani. Hii haina tofauti na enzi ya chama kimoja ambapo mgombea alikuwa mmoja kisha fedha kibao zinatumika kwa kinachoitwa "uchaguzi"...
Source: Gazeti la Mwananchi
NILIWAHI kuelezea ukigeugeu wa CCM wanapokuwa jukwani na wanapokuwa kwenye vikao vyao kwenye safu hii. Wanapokuwa jukwaani hujifanya watu wa watu na wanapokuwa kwenye vikao vyao hugeuka kuwa adui wa watu.
Jamaa hawa wanapokuwa jukwaani huzungumza kama...
Tumeshuhudia mengi tangu Ndugu Samuel Sitta awe Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kiasi kikubwa amekuwa na tofauti na maspika waliomtangulia kwa jinsi anavyoendesha shughuli zake kama kiongozi wa mmojawapo ya mihimili ya dola. Kuna wanaomsifu kwa utendaji wake na kuna...
Nimekuwa najiuliza hivi CCM na watu wake wako tayari kukubali sehemu moja ya muungano kutawaliwa na serikali ya upinzani? Ikitokea hali kama hiyo ndo itakuwa mwisho wa muungano? Nadhani CCM wako tayari kuzuia hali hiyo isitokee kwa gharama yoyote ile. Wana JF hii imekaaje?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.