digba sowey
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 7,781
- 14,099
Mkuu wa Mkoa wa DSM Paul Makonda leo February 05, 2020 amethibitisha kupokea kiasi cha Tsh. Million 600 zilizotolewa na Rais Magufuli kwa ajili ya ujenzi wa majengo matano ya Kisasa ya kituo cha Afya Bunju A, kwa lengo la kusogeza huduma karibu na Wananchi.
RC Makonda amesema wakazi wa Bunju na maeneo jirani walilazimika kusafiri umbali mrefu hadi Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya huduma ya upasuaji na kutokana na umbali mrefu baadhi yao kufariki Dunia wakiwa njiani na wengine kutumia gharama kubwa ya usafiri lakini uwepo wa Kituo hicho utafanya wapate huduma hapohapo Bunju A.
RC Makonda amesema ujenzi wa Kituo hicho unatarajiwa kuanza muda wowote kuanzia leo na utachukuwa muda wa miezi mitatu hadi kukamilika ambapo ameielekeza Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha inasimamia ipasavyo ujenzi huo.
Amesema kukamilika kwa majengo hayo kutafanya Zahanati ya Bunju A kupanda hadhi na kuwa Kituo cha Afya ambapo Serikali imepanga kutoa Madaktari na Wauguzi 58 kwaajili ya kuwahudumia Wananchi kituoni hapo
Mavuvuzela wa mabeberu kazi kwenu,makonda piga kazi baba
Sent using Jamii Forums mobile app
RC Makonda amesema wakazi wa Bunju na maeneo jirani walilazimika kusafiri umbali mrefu hadi Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya huduma ya upasuaji na kutokana na umbali mrefu baadhi yao kufariki Dunia wakiwa njiani na wengine kutumia gharama kubwa ya usafiri lakini uwepo wa Kituo hicho utafanya wapate huduma hapohapo Bunju A.
RC Makonda amesema ujenzi wa Kituo hicho unatarajiwa kuanza muda wowote kuanzia leo na utachukuwa muda wa miezi mitatu hadi kukamilika ambapo ameielekeza Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha inasimamia ipasavyo ujenzi huo.
Amesema kukamilika kwa majengo hayo kutafanya Zahanati ya Bunju A kupanda hadhi na kuwa Kituo cha Afya ambapo Serikali imepanga kutoa Madaktari na Wauguzi 58 kwaajili ya kuwahudumia Wananchi kituoni hapo
Mavuvuzela wa mabeberu kazi kwenu,makonda piga kazi baba
Sent using Jamii Forums mobile app