Maoni: Walimu wa masomo ya Sayansi wapewe malipo ya ziada

Blue Bahari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,229
1,141
Ndg wana JF habarini.
Mimi ni mwalimu wa masomo ya Sanaa ktk idara ya sekondari. Nalazimika kuandika mada hii kwa kuwa naguswa na majukumu mazito waliyonayo walimu wa masomo ya Sayansi (chemistry, biology & physics).
Kiukweli tuliopo humu jukwaani hakuna ambaye hakufundishwa na mwalimu wa Sayansi kulingana na mitaala yetu ya Elimu (aidha kidato cha kwanza na cha pili au mpaka kidato cha nne na kuendelea... Linapokuja suala la majukumu kwa walimu tajwa-walimu wa Sayansi wanamajukumu mengi kama vile:-
  1. Kufundisha "theory" za masomo husika (chemistry, physics, biology). Na shule nyingi za serikali-kama vile za kata, walimu wa masomo ya Sayansi wana vipindi Vingi kwa wiki (si chini ya 25) tofauti na walimu wamasomo ya sanaa.
  2. Kutafuta na kuandaa specimens au kuandaa solutions/ vifaa kwa ajili ya practicals.
  3. Kuelekeza na kusimamia namna ya ufanyaji wa practicals husika.
  4. Kazi za kusahihisha ni theory na practicals.
  5. Kazi zingine walimu hao wanazozifanya ni kama vile, kuandaa notes, mipango kazi ya mwaka mzima, maandalio ya masomo sawa sawa na walimu wa masomo ya sanaa.
Walimu hao wanazidiwa na majukumu hayo kwa kuwa shule nyingi-hususani za kata, hazina Lab technicians, ambao ndiyo kazi zao za kuandaa na kusimamia practicals na hivyo kumlazimu mwalimu ashughulike yeye mwenyewe.
MAPENDEKEZO.
Ni wakati muafaka Serikali yetu ione umuhimu wa malipo ya ziada kwa walimu wa sayansi. Katika hili aidha walipwe mshahara mkubwa zaidi ya walimu wa masomo ya sanaa, au mshahara uwe sawa sawa lakini walimu wa masomo ya sayansi wawe wanapewa posho kama wakuu wa shule wanavyopewa kwa sasa.
FAIDA ZA KUFANYA HIVYO.
  • kutaongeza hali na hamasa zaidi kwa walimu wa masomo ya sayansi kujituma zaidi katika kazi.
  • Wanafunzi wengi zaidi kufaulu masomo ya Sayansi.
  • Kupatikana kwa walimu wengi zaidi wa masomo ya Sayansi na kuifanya kauli mbiu ya mkuu wa nchi "Tanzania ya viwanda" ieleweke zaidi.
NOTE:
Kama serikali haina pesa za kuwalipa mishahara mikubwa zaidi walimu wa masomo ya Sayansi au kuwalipa posho za ziada, basi iajili Lab technicians ili kuwasaidia majukumu walimu hao.

=================================
MAONI MUHIMU YA WADAU WENGINE.

Si hayo tu kinacho shangaza hata vyuoni hao watu wanasoma kwa ada tofauti, ukienda arts 800,000/= Science 1,200,000/= wakianza kazi scale ni moja na kulipa mkopo wasayansi atadaiwa nyingi zaidi, ukiacha huo wingi wa majukumu ya kazi
 
organization ya walimu haipo strong na haitakuwa 7bu wanafitiana wao kwa wao...Na wapigaji ni wengi mno huko CWT
Mfano serikali ikasikia kilio hiki na kuamua kuwa-motisha, je in nani wa kuwafitinisha?
 
sio walimu wa science tu walimu wote,ualimu iko katika stressful jobs in the world,walitakiwa wawe na payscale sawa na majudge ama watu wengine wanaolipwa vizuri,hii ingefanya pia watu makini waaply ualimu,sio sasa hivi wanaenda watu ambao hawajafanya vizuri ngazi ya chini
 
sio walimu wa science tu walimu wote,ualimu iko katika stressful jobs in the world,walitakiwa wawe na payscale sawa na majudge ama watu wengine wanaolipwa vizuri,hii ingefanya pia watu makini waaply ualimu,sio sasa hivi wanaenda watu ambao hawajafanya vizuri ngazi ya chini
In kweli walimu wote wana changamoto lukuki, lakini kwa upande walimu wa Sayansi ni zaidi ya stressful. Na ndiyo maana natoa pendekezo walipwe zaidi.
 
Kuna jamaa yangu alikua mwalimu mzuri mno WA physics na maths alikua na diploma kisha alienda Udsm kuchukua degree!!! Lakini aliamua kuacha kufundisha akajiunga na veta shinyanga kujifunza grader ( katapila) na excaveter !! Sikuamini masikio yangu aliponielezea !!! Kwa sasa yupo na mradi mkubwa na serikali analifuhahia katapila !! Nasema hajutii uamuzi wake
 
Kuna jamaa yangu alikua mwalimu mzuri mno WA physics na maths alikua na diploma kisha alienda Udsm kuchukua degree!!! Lakini aliamua kuacha kufundisha akajiunga na veta shinyanga kujifunza grader ( katapila) na excaveter !! Sikuamini masikio yangu aliponielezea !!! Kwa sasa yupo na mradi mkubwa na serikali analifuhahia katapila !! Nasema hajutii uamuzi wake
Yap, wakati mwingine ni sahihi kabisa kubadili gia angani kwa kuangalia fursa nyinginezo.
 
Tayari serikali imeshaanza kuajiri watalaamu Wa maabara Kwa awamu..na kuhusu posho tuko Kwenye mchakato tunafikiria kutoa posho kwa walimu wote katikati ya mwezi ili kupunguza ukali Wa maisha..huu sio utani just wait and see.
 
Ipo hivi Mtoa Mada miaka ya nyuma walimu walikuwa wanaposho ktkt ya mwezi kama ilivyo kwa majeshi ila waliondoa tusubiri miujiza Labda hii serikali yetu sikivu wanaweza rudisha. Ualimu Siyo kazi mbaya ila inategemea ualimu unafanya na Nani? Awamu ilizopita walimu wakianza kazi baada ya miez 6 wanakopesheka nakujiletea maendeleo tofaut na sasa ngum kwa kua makato makubwa loan board.
 
Tayari serikali imeshaanza kuajiri watalaamu Wa maabara Kwa awamu..na kuhusu posho tuko Kwenye mchakato tunafikiria kutoa posho kwa walimu wote katikati ya mwezi ili kupunguza ukali Wa maisha..huu sio utani just wait and see.
Mkiliweza ili mtakua mmeweza vunja mfupa alioushinda fisii na hatimae vifoo vya wtt kwa kupigwa vitapotea kabisa....
 
Mchawi wa mwalimu ni mwalimu ona sasa hapa mwalimu anavyowabagua wenzake
Siwabagui walimu wengine, Ila naeleza hali halisi. Walimu wa Sayansi wanavipindi vingi vya theory kisha vipindi vya practicals ambavyo mwalimu mwenyewe hupanga ratiba yake.
 
Waalimu wote wanafanya kazi ngumu, pia issue ya practical na mitihani yake walishaijua kabla ya kusomea. Hakuna haja ya kulalama hapa, kwani walilazimishwa kusoma science?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwalimu wa art ana vipindi chini ya 15 kwa wiki wakati mwalimu wa masomo ya Sayansi ana vipindi zaidi ya 25 kwa wiki, nani mwenye majukumu zaidi?
walimu wote wakiwa masomo ya sanaa; je, masomo ya Sayansi yafutwe kwa kuwa hayana walimu?
 
Ipo hivi Mtoa Mada miaka ya nyuma walimu walikuwa wanaposho ktkt ya mwezi kama ilivyo kwa majeshi ila waliondoa tusubiri miujiza Labda hii serikali yetu sikivu wanaweza rudisha. Ualimu Siyo kazi mbaya ila inategemea ualimu unafanya na Nani? Awamu ilizopita walimu wakianza kazi baada ya miez 6 wanakopesheka nakujiletea maendeleo tofaut na sasa ngum kwa kua makato makubwa loan board.
Sababu za kuondoa posho hizo ni nini?
 
Back
Top Bottom