Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,782
Jina lake halisi ni Chukwudi Dumeme Onuamadike AKA EVANS... Ndie alikuwa mtekaji tajiri, maarufu na katili zaidi nchini Nigeria.. Akijulikana k Bilionea EVANS....
Historia yake ya utotoni haijulikani hasa lakini alianza shughuli ya utekaji kwa nia ya kulipwa fidia baada ya baba yake mzazi kumkana kuwa si mwanae
Hata hivyo kwa maneno yake mwenyewe anasema alianza shughuli za kuteka baada ya kufilisiwa zaidi ya Naira million 20 na mamlaka ya mapato nchini humo.. Hivyo biashara yake ya kuuza vipuri vya magari kufilisiwa....
Alianza shughuli mpya ya utekaji kwenye jimbo lake la Magodo lakini baadae mtaji ulipoongezek alihamishia shughuli zake mjini Lagos, alikokuwa kwa haraka na kupata UTAJIRI mkubwa kutokana na shughuli za kuteka na kulipwa fidia.....
Evans alikuwa na Mpenzi aliyempenda sana aitwaye Amaka... Inasemwa kuwa Amaka alikuwa mke wa mmoja wa makamanda wake... Aliyemuua ili atanue na Amaka...
Licha ya Amaka Evans pia alikuwa na mke wa ndoa aliyezaa naye watoto watano, hata hivyo mkewe huyo wa ndoa aliondoka Nigeria na kukimbilia Ghana kwenye jumba Lao la kifahari yeye na watoto wake na baadae wakakimbilia Canada.... Sababu kubwa ya mkewe kukimbia ni baada ya kugundua shughuli halisi za mumewe na kushindwa kukubaliana nazo
Je aliwezaje kuwakwepa polisi na mamlaka za usalama?
1. Evans kwanza aliunda makundi saba tofauti ya utekaji... Lakini yaliyofanya kazi kwa wakati mmoja ni mawili tu... Moja la kuteka (hapa lazima awepo) na la pili ni la kumpeleka mateka sehemu salama mpaka fidia itakapolipwa
2.Aliwaajiri na kuwatumia wanajeshi waliokuwa mahiri na wazoefu wa silaha na mbingu za kivita... Mmoja aliyekuwa ndani ya serikali alikiri kulipwa Naira Million sita katika matukio matatu aliyoyafanikisha
3. Hakuwa dhulumati wala mpunjaji wa watu wake... Kila mmoja alilipwa kulingana na makubaliano na ushiriki kwenye kila tukio
4. Pesa aliyopata kwenye fidia aliwekeza kwenye biashara nyingine halali kama usafirishaji wa mizigo na Huduma za fedha.. Kutuma na kupokea
5. Alimiliki laini za simu 162 na simu za gharama kubwa... Mojawapo wa simu zake za gharama ilikuwa ni simu mbili nyembamba aina ya Vertu moja ikiwa na thamani ya N2.6M na nyingine N2.4M
Vile vile alikuwa na simu aina ya Thuraya yenye thamani ya N800,000/= simu zake hizo zilimfanya ashindwe kufuatiliwa kutokana na mfumo wake wa ulinzi.
Thuraya haikuwa simu ya kutulia laini... Ilikuwa satellite phone na haikupoteza network iwe chini ya maji baharini au jangwani na ilikuwa water proof...
Mwisho wake ulifikaje?
Polisi walishatoa dau la Naira 30 million kwa atakayefanikisha kukamatwa kwake.. Lakini kwa miaka saba mfululizo haikuwezekana...
Wazo kutoka kitengo cha usalama la kufuatilia mawasiliano yake ndio kulifanikisha ukamataji wake.... Walianza kukamatwa watu wake wa chini... N msako ukatoka kwenye laini 162 mpaka 120 na baadae 36
Laini hizo 36 ndio zilionekana mara nyingi zikiwa na mawasiliano na watu wane... Evans aliwaita watu wake maalum sana.... Wapendwa wake... Watu hao walikuwa
. Amaka mpenzi wake (japo alikuwa na wengine watatu)
. Mama yake mzazi aliyekuwa anafahamu fika shughuli za mwanae na kumuonya bila mafanikio
. Dada yake aliyempenda sana na
. Rafiki yake aliyemwamini sana....
End of part one...
Historia yake ya utotoni haijulikani hasa lakini alianza shughuli ya utekaji kwa nia ya kulipwa fidia baada ya baba yake mzazi kumkana kuwa si mwanae
Hata hivyo kwa maneno yake mwenyewe anasema alianza shughuli za kuteka baada ya kufilisiwa zaidi ya Naira million 20 na mamlaka ya mapato nchini humo.. Hivyo biashara yake ya kuuza vipuri vya magari kufilisiwa....
Alianza shughuli mpya ya utekaji kwenye jimbo lake la Magodo lakini baadae mtaji ulipoongezek alihamishia shughuli zake mjini Lagos, alikokuwa kwa haraka na kupata UTAJIRI mkubwa kutokana na shughuli za kuteka na kulipwa fidia.....
Evans alikuwa na Mpenzi aliyempenda sana aitwaye Amaka... Inasemwa kuwa Amaka alikuwa mke wa mmoja wa makamanda wake... Aliyemuua ili atanue na Amaka...
Licha ya Amaka Evans pia alikuwa na mke wa ndoa aliyezaa naye watoto watano, hata hivyo mkewe huyo wa ndoa aliondoka Nigeria na kukimbilia Ghana kwenye jumba Lao la kifahari yeye na watoto wake na baadae wakakimbilia Canada.... Sababu kubwa ya mkewe kukimbia ni baada ya kugundua shughuli halisi za mumewe na kushindwa kukubaliana nazo
Je aliwezaje kuwakwepa polisi na mamlaka za usalama?
1. Evans kwanza aliunda makundi saba tofauti ya utekaji... Lakini yaliyofanya kazi kwa wakati mmoja ni mawili tu... Moja la kuteka (hapa lazima awepo) na la pili ni la kumpeleka mateka sehemu salama mpaka fidia itakapolipwa
2.Aliwaajiri na kuwatumia wanajeshi waliokuwa mahiri na wazoefu wa silaha na mbingu za kivita... Mmoja aliyekuwa ndani ya serikali alikiri kulipwa Naira Million sita katika matukio matatu aliyoyafanikisha
3. Hakuwa dhulumati wala mpunjaji wa watu wake... Kila mmoja alilipwa kulingana na makubaliano na ushiriki kwenye kila tukio
4. Pesa aliyopata kwenye fidia aliwekeza kwenye biashara nyingine halali kama usafirishaji wa mizigo na Huduma za fedha.. Kutuma na kupokea
5. Alimiliki laini za simu 162 na simu za gharama kubwa... Mojawapo wa simu zake za gharama ilikuwa ni simu mbili nyembamba aina ya Vertu moja ikiwa na thamani ya N2.6M na nyingine N2.4M
Vile vile alikuwa na simu aina ya Thuraya yenye thamani ya N800,000/= simu zake hizo zilimfanya ashindwe kufuatiliwa kutokana na mfumo wake wa ulinzi.
Thuraya haikuwa simu ya kutulia laini... Ilikuwa satellite phone na haikupoteza network iwe chini ya maji baharini au jangwani na ilikuwa water proof...
Mwisho wake ulifikaje?
Polisi walishatoa dau la Naira 30 million kwa atakayefanikisha kukamatwa kwake.. Lakini kwa miaka saba mfululizo haikuwezekana...
Wazo kutoka kitengo cha usalama la kufuatilia mawasiliano yake ndio kulifanikisha ukamataji wake.... Walianza kukamatwa watu wake wa chini... N msako ukatoka kwenye laini 162 mpaka 120 na baadae 36
Laini hizo 36 ndio zilionekana mara nyingi zikiwa na mawasiliano na watu wane... Evans aliwaita watu wake maalum sana.... Wapendwa wake... Watu hao walikuwa
. Amaka mpenzi wake (japo alikuwa na wengine watatu)
. Mama yake mzazi aliyekuwa anafahamu fika shughuli za mwanae na kumuonya bila mafanikio
. Dada yake aliyempenda sana na
. Rafiki yake aliyemwamini sana....
End of part one...