COLLOH-MZII RELOADED
JF-Expert Member
- Apr 6, 2017
- 7,544
- 3,130
The guy who queued to vote with githeri on his hands has his Photoshop photos gone viral ... Trending #1 in Twitter.
Here are a sample few.
-------------
Licha ya kuwepo miongoni mwa wananchi kuhusu matokeo ya kura ya urais, Wakenya kwenye mitandao ya kijamii Jumatano na Alhamisi waliunganishwa na picha ya mwanamume mmoja aliyekuwa akifurahia mlo wa Githeri kwenye foleni ya kupiga kura hapo Jumanne.
Mwanamume huyo ambaye amebandikwa jina 'Githeri Man' alinaswa na kamera ya mmoja wa wapiga kura akila mchanganyiko wake wa mahindi na maharage alioutia ndani ya karatasi ya plastiki katika kijibaridi cha asubuhi ya Jumanne.
Hadi wakati wa kuchapishwa kwa habari hii, jina lake halikuwa limetambulika wala anapoishi, kituo ambapo alipiga kura yake na aliyeipiga.
Kwenye Twitter Githeriman picha ya mwanamume huyo ilihaririwa na kuwekwa katika hali ambazo ziliibua msisimko mkubwa na utani usio na kifani.
Mojawapo ya picha hizo ilionyesha mwanamume huyo akiwa katikati ya Rais Kenyatta, Naibu Rais William Ruto na vinara wa NASA Raila Odinga na Kalonzo Musyoka.
Katika picha nyingine, alionyeshwa akifika Canaan. Msisimko wa safari ya Canaan ulianzishwa na Bw. Raila Odinga aliyasema atakuwa 'Yoshua' na kuwaongoza wakenya kutoka 'Misri'.
Alionekana pia akiwa kondakta, huku pia akitokea katika studio za Runinga za NTV na Citizen. Kwenye Spoti haikuachwa nyuma kwenye uchangamfu huo, mwanamume huyo alionekana kwenye picha mbalimbali.
Daniel Ndambuki wa Churchill Show anamsaka amhoji katika kipindi chake. Mimi niko tayari kumchangia pesa. Kubeba kwake githeri kunaonyesha alikuwa amejitolea kupiga kura. Amewaunganisha wakenya wote katika wakati wa taharuki. Tusherehekee maisha yake.
Ni kuhaririwa kwa picha hiyo ambako kulichangia wakenya mtandaoni kupunguza jumbe za chuki baada ya mwaniaji urais wa NASA, Raila Odinga kudai kwamba mfumo wa KIEMS wa IEBC ulidukuliwa usiku wa kuamkia Jumatano na kuweka matokeo ya uwongo.
Here are a sample few.
-------------
Licha ya kuwepo miongoni mwa wananchi kuhusu matokeo ya kura ya urais, Wakenya kwenye mitandao ya kijamii Jumatano na Alhamisi waliunganishwa na picha ya mwanamume mmoja aliyekuwa akifurahia mlo wa Githeri kwenye foleni ya kupiga kura hapo Jumanne.
Mwanamume huyo ambaye amebandikwa jina 'Githeri Man' alinaswa na kamera ya mmoja wa wapiga kura akila mchanganyiko wake wa mahindi na maharage alioutia ndani ya karatasi ya plastiki katika kijibaridi cha asubuhi ya Jumanne.
Hadi wakati wa kuchapishwa kwa habari hii, jina lake halikuwa limetambulika wala anapoishi, kituo ambapo alipiga kura yake na aliyeipiga.
Kwenye Twitter Githeriman picha ya mwanamume huyo ilihaririwa na kuwekwa katika hali ambazo ziliibua msisimko mkubwa na utani usio na kifani.
Mojawapo ya picha hizo ilionyesha mwanamume huyo akiwa katikati ya Rais Kenyatta, Naibu Rais William Ruto na vinara wa NASA Raila Odinga na Kalonzo Musyoka.
Katika picha nyingine, alionyeshwa akifika Canaan. Msisimko wa safari ya Canaan ulianzishwa na Bw. Raila Odinga aliyasema atakuwa 'Yoshua' na kuwaongoza wakenya kutoka 'Misri'.
Alionekana pia akiwa kondakta, huku pia akitokea katika studio za Runinga za NTV na Citizen. Kwenye Spoti haikuachwa nyuma kwenye uchangamfu huo, mwanamume huyo alionekana kwenye picha mbalimbali.
Daniel Ndambuki wa Churchill Show anamsaka amhoji katika kipindi chake. Mimi niko tayari kumchangia pesa. Kubeba kwake githeri kunaonyesha alikuwa amejitolea kupiga kura. Amewaunganisha wakenya wote katika wakati wa taharuki. Tusherehekee maisha yake.
Ni kuhaririwa kwa picha hiyo ambako kulichangia wakenya mtandaoni kupunguza jumbe za chuki baada ya mwaniaji urais wa NASA, Raila Odinga kudai kwamba mfumo wa KIEMS wa IEBC ulidukuliwa usiku wa kuamkia Jumatano na kuweka matokeo ya uwongo.