Natafuta mganga wa kienyeji hapa Dar es Salaam

CCNP Engineer

JF-Expert Member
Apr 13, 2017
462
1,276
Marafiki zako ndio ndugu zako.
Huwezi kuinuka maishani peke yako tu bila network na connection za jamaa zako.

Lakini hao hao marafiki wanaweza kuwa adui wa maendeleo yako.
Wakawa maadui zako kwa sababu mbali mbali.

Kuna jamaa yangu wa karibu sana sana sana aisee... Aliniomba mimuazime Laki tano. Alikua anataka kuoa, mshahara ulikua hujatoka. Akaahidi mshahara ukitoka tuu pesa yangu naipata.

Sasa ni Mwezi wa tatu huu jamaa ananizungusha, sms hajibu...
Kwangu hakanyagi tena, na kuna nguo aliziacha hapa getto kwangu hajaziijia. Ananikwepa.

Ameoa fresh. Kaja kutafuta chumba nasikia huko Tabata fresh.
Pesa yangu hataki kunilipa.

Sasa nataka nimfanyie ubaya.
Natafuta mtaalamu wa mambo ya visasi nimfanyie jamaa kitu ambacho at least nitapoza machungu ya pesa zangu.

Kama sio kunilipa pesa zangu na fidia juu, basi wote tupate maumivu.

Mwenye kumjua mtaalamu (sio mbabaishaji) hapa Dar anisaidie wakuu. Niko serious.

Napatikana Kinondoni.
Niko serious.
 
Hahahaha! Mganga ni wewe mwenyewe! Peleka madai yako kwa Mwenye Enzi Mungu, hakika atakusikia! Kinuie kabisa! Utapata mafanikio! Kuna ndugu ambao unastahili kuepukana nao kama ukoma!
Mola akutangulie!
 
Wote ulio wahi kuwa kosea nao wange fanya hivi ungekuwepo leo hii ungekuwa salaama,pesa inatafutwa mkabizi mungu ndo atahukumu unaweza mlipizia ukawa unajifungia milango kama unajua dini utanielewa ila kama dini ni mtihani,basi kazi njema
 
Sikukuu ya Idd imekaribia,utaambiwa lete mbuzi na kuku mweupe ili familia ya mganga ijichane kwenye sikukuu
 
Ni vizuri kuandikishana mkiwa mnapeana pesa ya kukopeshana, haswa kama haujui mtu na sio ndugu yako yaani sibling au mzazi. Kuwa yukoje katika kulipa deni, inasaidia sana baadae.

Sasa hivi ungekuwa unaenda kumshitaki na kuonyesha karatasi aliyoweka saini ya kupokea pesa hizo yenye majina na anuani yake hata namba za simu na shahidi/mashahidi.
 
Marafiki zako ndio ndugu zako.
Huwezi kuinuka maishani peke yako tu bila network na connection za jamaa zako.

Lakini hao hao marafiki wanaweza kuwa adui wa maendeleo yako.
Wakawa maadui zako kwa sababu mbali mbali.

Kuna jamaa yangu wa karibu sana sana sana aisee... Aliniomba mimuazime Laki tano. Alikua anataka kuoa, mshahara ulikua hujatoka. Akaahidi mshahara ukitoka tuu pesa yangu naipata.

Sasa ni Mwezi wa tatu huu jamaa ananizungusha, sms hajibu...
Kwangu hakanyagi tena, na kuna nguo aliziacha hapa getto kwangu hajaziijia. Ananikwepa.

Ameoa fresh. Kaja kutafuta chumba nasikia huko Tabata fresh.
Pesa yangu hataki kunilipa.

Sasa nataka nimfanyie ubaya.
Natafuta mtaalamu wa mambo ya visasi nimfanyie jamaa kitu ambacho at least nitapoza machungu ya pesa zangu.

Kama sio kunilipa pesa zangu na fidia juu, basi wote tupate maumivu.

Mwenye kumjua mtaalamu (sio mbabaishaji) hapa Dar anisaidie wakuu. Niko serious.

Napatikana Kinondoni.
Niko serious.
Ninae mtu hatare sana tena anaweza kumuondoa hata duniani kwa radi,ila gharama yake laki tano,malipo ni baada ya kazi,ila na wewe ukimrusha pesa zake,ujue umeliamsha dude
 
Acheni ujinga basi.
Mie nimeomba mtu mwenye kumjua mtaalamu wa visasi anisaidie.

Wala sijasema nina shida na ushauri wenu huo mwingine.
Mwenye kumjua mtaalamu ndio nitamsikiliza hapa. Kama hujui pita kushoto.
ni - PM mtu wangu kuna mtaalam yuko Chalinze anatengeneza radi mpaka kwa mwekundu tu inategemea na unavyompanga na bargaining power yako
 
Siku zote hasara roho .... Japo kuwa ni jasho lako nadhani ni vyema kuamini atakulipa kwa sababu huwezi kujua hali yake.

Pia kumbuka huko unakotaka kwenda unaweza ukatumia fedha kiasi cha hiyo uliyomkopesha au hata kikazidi na usifanikiwe kile ulichokidhamiria.
 
Back
Top Bottom