Kupayuka! Mbinu mpya ya kubaki kileleni?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,754
1471653538205.jpg
Kileleni kuna raha yake ni kuzuri na kila kitu kinakuwa chini yako...kilele ni kilele tu hasa kikiwa cha mafanikio umaarufu nk...hakuna anayependa kushuka chini...labda kiwe ni kilele cha matatizo hapo hakuna anayependa kubaki
Kuna vitu special hutufanya tuwe kileleni....wasanii wetu ni kutokana na kazi zao...lakini zinapokosa mvuto kwasababu ya ubunifu matatizo na mahitaji ya nyakati na kuanza kuporomoka, hutafuta njia nyingine ya kubaki kileleni.

Njia hiyo si ile iliyowapandisha! Hii ni shortcut iliyojaa kuchanganyikiwa, unaweza kuona wasanii wetu wengi wamebaki na umaarufu wa tuhuma za mambo ya ajabu kuchambana mitandaoni na kufanya mambo mengi ya kutia kinyaa alimradi tu wawe midomoni mwa watu na kwenye kurasa za media.

Wanasiasa nao ni waathirika wa umaarufu na mmojawapo ni mkuu wa mkoa wa Dsm...Ukiangalia matamko aliyokwishatoa (ambayo mengi kimsingi na kiuhalisia hayatekelezeki)utagundua kuwa ana mradi maalum wa kutafuta kiki na kubaki kwenye kurasa za vyombo vya habari na midomo ya watu.

Amegundua udhaifu wa media zetu hazina tafakuri ya kina, huandika chochote na kikapokewa kwa mlipuko na kuzua mijadala isiyoisha.....kwa njia hii anajihakikishia kubaki kileleni japo kwa kupayuka! Lakini je yuko peke yake?
1471654505982.jpg
 
Kweli kuna udhaifu mkubwa katika media za Tanzania.

Halafu waandishi wa habari ni waoga hawahoji kwa kuuliza maswali magumu ya msingi ili kuondoa ukakasi, wao waandishi kazi yao ''kunakili'' yale yanayotoka ktk meza kubwa neno kwa neno.

Angalau hapa Jamiiforums tunahoji masuala kwa kina waje wajifunze au kama wanaogopa basi waandishi waseme ''mitandao ya jamii inasema hivi, je wewe bwana mkubwa una nini la kusema juu ya hoja hii ilivutia maswali mengi katika mitandao ya jamii.
 
Kweli kuna udhaifu mkubwa katika media za Tanzania.

Halafu waandishi wa habari ni waoga hawahoji kwa kuuliza maswali magumu ya msingi ili kuondoa ukakasi, wao waandishi kazi yao ''kunakili'' yale yanayotoka ktk meza kubwa neno kwa neno.

Angalau hapa Jamiiforums tunahoji masuala kwa kina waje wajifunze au kama wanaogopa basi waandishi waseme ''mitandao ya jamii inasema hivi, je wewe bwana mkubwa una nini la kusema juu ya hoja hii ilivutia maswali mengi katika mitandao ya jamii.
bagamoyo tatizo ni bahasha na kutanguliza maslahi binafsi mbele! Ukionekana ni mjuaji sana unahoji sana mkutano mwingine huitwi ng'ooo
 
Dr. Juma Mwaka pole, kilele ulichokuwepo sasa tunatafuta kigagula mpiga manyanga mwingine tumuweke. Weee umaarufu ulioupata unakutosha, umekuwa maarufu kuliko hata Magu?
 
Dr. Juma Mwaka pole, kilele ulichokuwepo sasa tunatafuta kigagula mpiga manyanga mwingine tumuweke. Weee umaarufu ulioupata unakutosha, umekuwa maarufu kuliko hata Magu?
 
Ndio mbinu za watu wasiojiamini mkuu, mambumbumbu, dizaini falain hivi kama ya ulevi, maana hata mlevi akilea ndio hupayuka, sasa napayuka kwa kuwa hata mkuu anapayuka, nafyatua tu kila kitu nionekani mchapa kazi.
 
Back
Top Bottom