Zijue aina za CCTV-Camera na kazi zake

idtech

Member
Jan 4, 2016
91
222
Kuna aina mbalimbali za CCTV-Camra ambazo zimegawanywa katika makundi mbalimbali kutegemeana na aina ya kamera,ufanyaji kazi wake,Lensi iliyotumika,
Hapa tutaongelea aina nane maarufu(Common) za CCTV Camera

1 Dome CCTV Camera

Hii ni aina ya kamera ambayo ina umbo la duara. Mara nyingi kamera hii hutumika katika ulinzi na usalama wa ndani. Maduka na viwanda vingi hupendelea Kufunga aina hii ya kamera. Moja kati ya faida kubwa ni kuwa huumfanya muharifu ashindwe kujua jicho la kamera limeangalia upande gani. Pia kamera aina hii inaoption ya kuweza kuzungusha jicho kadili operator atakavyo amua kulingana na hali ya usalama. Lakini pia aina hii zipo ambazo ni automatic zinazungusha jicho ili kuweza kukava eneo kubwa zaidi kwa kamera moja.
dome-jpg.365496
Dome CCTV-Camrea



2. Bullet CCTV Camera

Hizi ni kamera ambazo zina umbo refu (cylindrical shape) . Kamera hizi hutumika katika matumizi yanayohitaji muonekano wa mbali (Long Distance View) huchukua picha na matukio katika sehem amabayo ni fixed. Hazina control za kuzoom ama kupan/tilt (Manipulation of camera activity). Mara nyingi kamera hizi huwa zina waterproof iliyo kwenye lenzi yake kwa aijri ya kuzuia maji ya mvua mawe ya mvua pamoja na aina yoyote ile ya vumbi.
waterproof-cctv-bullet-camera-with-ir-500x500-jpg.365497
Bullet CCTV-Camera



3. C-Mount CCTV Camera

C-Mount CCTV camera zina lenzi amabavo unaweza badilisha kulingana na matumizi yako (detachable lens). Mara nyingi CCTV Camera lens huchukua eneo kati ya 35 na 45ft lakin ukiwa na C-Mount unaweza weka lens inayochukua zaid ya 45ft
c-mount-jpg.365498

C-Mount CCTV Camera Pamoja na lens zake


4. Day/Night CCTV Camera

Aina hii ya kamera inasifa moja kubwa ya kuweza kufanya kazi katika mazingira ya mwanga hafifu na yenye mwanga mkubwa. Kamera hizi hazina Infrared illuminators kwa sababu zinauwezo wa kuchukua picha vizuri katika mazingira ya mwanga hafifu na mwanga mwingi.
day-night-camera-jpg.365500
Day/Night CCTV-Camera




5. Infrared/Night Vision CCTV Camera

Zina uwezo wa kuchukua picha katika mazingira yasiyokuwa na mwanga kabisa. Hutumia Infrared LEDs kuweza kupata picha ya tukio
infrared-camera-jpg.365504
Infrared/Night vision CCTV Camera

6. Network/IP CCTV Camera

Kamera hizi husafirisha picha zake kwa njia ya mtandao. Zipo ambazo ni wired na zipo ambazo ni wireless. Faida mojawapo kuu ya kamera hizi ni kuwa unaweza kuzifunga nyumbani na wew ukiwa kazini kwako unaweza ona nini kinaendelea nyumbani. Vivyo hivyo unaweza funga kazini kwako na wewe ukiwa mahala popote duniani ukaendelea kuona kazi zinavyofanyika.
ip-camera-jpg.365505
Network/IP CCTV Camera



7. Wireless CCTV Camera

Hizi ni aina ya kamera zisizotumia wire kusafirisha picha zake. NB sikila wireless ni IP CCTV
wireless-jpg.365506



8. High-Definition HD CCTV Camera

Aina hii ya kamera hutoa picha katika muonekano ang’avu. (High-Definition). Mara nyingi hutumika katika mabenki na makasino.
hd-jpg.365507


KARIBU IdTech. Tunafanya:-

full service CCTV design, installation, support, monitoring services and integration with audio and access management security systems, including all key CCTV camera system types, components, accessories and concepts such as:



    • IdTech will install the right CCTV camera for your business (including IP, infrared, low-light, HD, verified, wireless, day/night, c-mount, bullet, dome, waterproof)
    • 24/7 CCTV camera monitoring at our remote monitoring station
    • DVRs (digital video recorders)
    • CCTV camera towers and columns
    • CCTV telemetry systems
    • Deterrent CCTV systems
    • Covert CCTV systems
    • Motion detection systems
    • Integrated audio / CCTV systems
    • Video Analytics/Predictive software
    • CCTV camera lenses
    • CCTV monitors
    • CCTV multiplexors
    • CCTV illumination
    • CCTV switchers
    • Fibre optic CCTV transmission
    • Networked CCTV transmission (IP CCTV transmission)
    • Wireless CCTV camera systems
Tupo Mikocheni Mkabara na Jued Building
 
I
naomba tofauti kati ya IP camera, WiFi na wireless camera
Network IP camera zinatumia Internet kusafirisha picha zake. unaweza kuakises picha zake hata kwa kutumia simu yako ya mkononi popote pale ulipo.
WiFi=wirles. Nazo hutumia Internet kusafirisha picha zake lakin ni za masafa mafupi.(short range distance)
 
Mkuu nauliza tu; Nikitaka kuweka kamera kwenye makazi yangu, kwa ajili ya ulinzi wa kujilinda mwenyewe pande zote nne za nyumba, niweze kuamshwa ajapo mtukaribu na nyumba (tuseme mwizi) niamshwe (alerted) yawezekana nijue yupo upande gani?? Itaweza kuwa ka kiasi gani? Gharama ya juu na chini pia.
 
Nime-install icamspy kwenye simu ni nzuri, je mleta mada kuna namna naweza kui link na mojawapo ya CCTV camera hapo juu?
 
Back
Top Bottom