Sanaa ya kifo

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,790
42e6a14c8b4a9b299b842cd9a83af7c3.jpg
Hii ni habari ngeni kabisa kwa wale watakaobahatika kusoma hii mada na pia wale wenye kupenda kujifunza vitu vipya ni sanaa ya kifo katika uhalisia wetu bila kuchanganya na doctrines za kiimani na kiasili.

Kwenye mada nyingi tumeona uhayawani wa mwanadamu tumeona kwa sehemu kubwa jinsi kiumbe hiki kiitwacho binadamu kilivyo kipumbavu na kisicho na chembe ya uelewa kuhusu yale yatokeayo na ayafanyayo kila siku.

Binadamu anaongozwa na hisia zaidi ya vile avipendavyo kuliko uhalisia na uelewa wa yale yanayotokea kila sekunde kila dakika na kila saa ya pumzi yetu
si mara haba tumeona tumeona picha zinazowakilisha matukio mbalimbali ya kutisha na kusikitisha matukio ya ajali nk. Wengi tumeyaandikia maelezo ya mbwembwe kulingana na hisia zetu na umahiri wetu katika kuonyesha uchungu lawama hasira nk.

Matukio hayo ni wenzetu ambao tayari hatunao tena ni marehemu wameshamaliza safari yao hapa duniani na sasa wako mahali pengine wakipumzika au wakiendelea na safari yao lakini katika hatua nyingine.
Hawa tunawaita wafu, kila mmoja akiwa kafikia umauti wake kwa style yake.

Wengine kwa mateso makubwa wametuachia majonzi na huzuni ambazo zina chukua muda kufutika katika hisia na kumbukumbu zetu, lakini pamoja na hayo yote natuangalie kwa mtazamo mwingine hiki kitu kinachoitwa KIFO ili tuweze kuwa na ufahamu mwingine tofauti na ule tuliozoea kuwa nao huko nyuma kwa njia hii ile huzuni simanzi na majonzi kwa wapendwa wetu vinaweza kupungua na kutufanya tuishi kwa utulivu zaidi.
------------------------------
Si watu haba ambao hawatakubaliana nami kwa kile nitakachoandika hapa wengi watanihukumu kwa namna ya ajabu kabisa siwalaumu kwakuwa ni mazoea ya wengi kuwa wanafiki na waoga kupindukia, na kuwa na ile dhana ya kuwa kinachosemwa na wengi ndio sahihi ndio ukweli ndio uhalisia
Hatutaki kubadilika Hatutaki kujifunza mambo mapya hatutaki kusoma na kuzitafsiri hisia zetu za ndani kabisa kwa muktadha mwingine.

Tunakumbuka kusahau kuwa ni katika hizo hisia zetu za ndani kabisa ndimo kweli yetu inapotoka na kweli hiyo tunapobahatika kuifahamu hatuna budi kuitafsiri kwa wengine bila woga wala kuficha ficha hata kama tutaitwa majina yote mabaya na kuonekana tunakwenda kinyume na kanuni za kutunga za mwanadamu.
****************************

Sehemu ya pili

Kifo kwa tafsiri ya rahisi na iliyozoeleka kwa mwanadamu si neno zuri si neno la kuvutia wala kutajwatajwa hovyo ni neno lililonakshiwa kwa vikolombwezo vyote kwa kutisha na kuogofya sana lakini Kifo ni jambo bora na la bahati nadra kutokea, kifo ni daraja la kuvukia kwenda kwenye hatua nyingine ya maisha ya juu zaidi mepesi zaidi mazuri zaidi! Kifo ni mwendelezo wa uumbaji ni kama tunaposema elimu haina mwisho uumbaji nao hauna mwisho.
 
Sehemu ya pili

f932cac6903feda5168161fafd17d20d.jpg
Kwahiyo hiyo kwa wale wafu ni kwamba wamekwenda kwenye hatua nyingine ya maisha wameingia kwenye daraja lingine wamefaulu mtihani wa kifo ndio maana wamevuka na kuendelea...kwahiyo kifo ni mafanikio....kwahiyo kama bado unaishi maana yake ni kwamba hujafikia hatua ya kwenda kifoni au umefeli mtihani wake...
Hapa duniani tupo binadamu tunaokadiriwa kufikia bilioni sita wake kwa waume ni katika dakika hizi zenye sekunde sitini masaa 24 siku Saba na miezi 12 watu hufaulu kuingia kwenye daraja lingine la maisha
Kifo ni siri kama ulivyo mtihani ni wale tu wanaofaulu ndio huifahamu siri hiyo...! Tumeshawahi kusikia watu wakisema kuwa Eti fulani kanusurika kifo! Huyu hajanusurika bali kafeli mtihani wa kifo
Siri iliyo wazi ni kwamba kila mwanadamu ana siku saa na dakika yake ya kufanya mtihani wa kifo kufaulu na hatimaye kuendelea mbele
 
Sehemu ya tatu

4fe2bcbbfb23849e88a9bedeca9b0c00.jpg
Ukisoma katika maandiko yote ya kidini na philosophia za dini yoyote ile hata ile ya mashetani kila moja inakiri kuwa kifo sio mwisho wa maisha bali ni mwanzo wa kuingia katika hatua nyingine ya maisha kama kwenda mbinguni jehanam/motoni/kuzimu au kuzaliwa tena katika umbo lingine kwa zile imani nyinginezo
Kama vile tunavyofaulu mitihani ya kielimu na kupata daraja fulani au kupanda daraja fulani na kupangiwa darasa chuo au kazi fulani sehemu tofauti na classmates wako ndio hivyo hivyo hata kwenye kifo...si kila mtu baada ya kifo atakwenda akhera au peponi, kila mmoja wetu atakwenda sehemu yake kwa style yake na kwa muda wake kutokana na uchaguzi wake na kufaulu kwake (uchaguzi huu huja kulingana na matakwa ya maisha yako ya duniani)
Furaha tuliyo nayo ndugu zetu wanapofaulu mitihani yao ndio furaha tunayopaswa kuwa nayo hata wapendwa wetu wanapofaulu kutwaliwa toka ulimwengu huu na kuingia ulimwengu mwingine....
Sanaa ya kifo ni fumbo tata ni nahau tasa ni philosophia iliyokengeuka kanuni na uelewa wa dunia ya kufikirika
Jaribu kujiuliza unapata hisia gani unapoambiwa mtu kafa kwa kujinyonga kunywa sumu ajali ugonjwa kuuliza nk nk!huwa tunahitimisha kwa kusema ni Majaliwa ya Mwenyezi Mungu! Ameyataka mwenyewe!zake zilikuwa zimefika! Nk nk...! Kamwe hatusumbuki kuufumua na kuushughulisha ufahamu wetu kwa kutafakari dakika zile za mwisho marehemu alikuwa katika hali gani aliwaza nini alijisikiaje alihisi nini aliona nini na hata kama ni wauaji maswali ni hayo hayo
Kwa kawaida kila kifo hakikosi sababu na kila kifo kina maelezo yake . .mara nyingi tunahoji kidogo tunasikitika kidogo tunashughulika na msiba tunazika na maisha yanaendelea . .!!!!


ITAENDELEA
 
Sehemu ya nne

8e84adb7789211f7bce34f7b33fcd87f.jpg
Tusisahau kuwa kama ilivyo tofauti ya maswali na tofauti ya mitihani ndivyo hivyo hivyo hata katika kifo...vifo haviwezi kufanana hata siku moja hata kama mtachinjwa kwa pamoja au kupigwa risasi, kamwe hatuwezi kuwa na majibu yanayofanana na kamwe hatuwezi kuondoka kwa vifo vinavyofanana
Kama ilivyo mitihani kuna migumu na mirahisi ndivyo ilivyo hata kwenye kifo, vifo vingine vinatisha vingine vinauma vingine vinatatanisha vingine ni rahisi na havina maumivu kabisa! Cha kushangaza ni kwamba kamwe hatuwezi kujichagulia aina ya mitihani ya kifo....ukifa kwa kujinyonga au kujipiga risasi nk si uchaguzi wako kamwe....huo ndio mustakabali wako na kamwe hukuchagua mwenyewe
Hebu soma mfano huu! Huyu ni mmojawapo wa aina ya watu aliyekuwa anajiandaa kuondoka toka ulimwengu huu...ni habari ya kweli kabisa...alikuwa anahofia sana mtihani wa kifo na saa zake za mwisho zilikuwa ngumu mno! Akawa na mashaka akawa hana natumaini tena akawaza mengi, lakini mwishowe alifaulu mtihani wake na sasa hayupo pamoja nasi...natumaini akiangalia nyuma atajiona mjinga na kujicheka mno...! Atajisemea nilikuwa nahofia nini kikubwa! ?ufuatao ni ujumbe aliouacha kabla hajatwaliwa kutoka maisha haya
Maneno haya aliyanukuu kutoka kitabu cha Biblia Ayubu 7:1-17 yanasomeka hivi; Je mtu hana wakati wake wa vita juu ya nchi?na siku zake, je si kama si kama siku za mwajiriwa?
Kama mtumishi atamaniye sana kile kivuli, kama mwajiriwa anayetazamia sana mshahara wake, ni hivyo nami nimepewa miezi ya ubatili iwe fungu langu. Nami nimeandikiwa masiku yenye kuchokesha, hapo nilalapo chini nasema nitaondoka lini? Lakini Usiku huwa mrefu nami nimejibanza na kujitupatupa huko na huko hata kupambazuke
Mwili wangu umevikwa mabuu makubwa na madogo ya udongo. Ngozi yangu hufumba kisha ikafumbuka tena.siku zangu hupita upesi kuliko chombo cha kufumia, nazo zapita pasipokuwa na natumaini
Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo ; jicho langu halitayaona mema tena..! Mwisho wa kunukuu
 
Mkuu Mshana jr,kwahiyo mtoto mchanga anae zaliwa nakufa, anakuwa amefaulu mtihani kwa haraka?.Vipi anae fariki ktk umri wa Miaka 90,je amechelewa kufaulu?.
Inasemekana siku hizi watu wanakufa angali bado vijana.Je hii inamaana siku hizi watu wanafaulu mtihani wa kifo mapema zaidi?,je hii maana yake kizazi hiki ni kizazi bora zaidi kuliko vizazi vilivyo pita?.
 
Sehemu ya nne

Tusisahau kuwa kama ilivyo tofauti ya maswali na tofauti ya mitihani ndivyo hivyo hivyo hata katika kifo...vifo haviwezi kufanana hata siku moja hata kama mtachinjwa kwa pamoja au kupigwa risasi, kamwe hatuwezi kuwa na majibu yanayofanana na kamwe hatuwezi kuondoka kwa vifo vinavyofanana
Kama ilivyo mitihani kuna migumu na mirahisi ndivyo ilivyo hata kwenye kifo, vifo vingine vinatisha vingine vinauma vingine vinatatanisha vingine ni rahisi na havina maumivu kabisa! Cha kushangaza ni kwamba kamwe hatuwezi kujichagulia aina ya mitihani ya kifo....ukifa kwa kujinyonga au kujipiga risasi nk si uchaguzi wako kamwe....huo ndio mustakabali wako na kamwe hukuchagua mwenyewe
Mtunga mtihani wa kifo ni nani? Nani anatuchagulia njia ya kufa?
 
Sehemu ya tano

ec3541f783ec204a01ecd96604d527a4.jpg
Tunajifunza nini hapa? Hii ndio sanaaa ya kifo huu ndio uhalisia wetu, maisha yetu ni mafupi mno yanapita hima na yamejaa mashaka na hatuna furaha ya kweli tumejawa na stress za kila aina tunatamani kukaa kivulini mahali patulivu penye upepo mwanana, siku zetu za kupumua si lolote bali ubatili mtupu ...Tunalala tukikesha hata alfajiri kunapopambazuka
Sanaa ya ni mtihani usiotabirika, kamwe sisi si wakazi wa hii dunia sisi ni wapitaji kwahiyo tujiandae kama mwanafunzi ajiandaavyo na mitihani ili utakapofika muda wa kuondoka tuondoke kwa amani tukiwaacha wapendwa wetu katika hali njema na bila mitafaruku
Ndugu yetu aliyenukuu hayo maneno ya Biblia takatifu alikufa alikufa kwa kunywa sumu...kabla ya kifo chake alimuaga mkewe vizuri kuwa anaenda kazini (alikuwa meneja wa bar hapa Dar) kule kazini alifanya sherehe ndogo na kuwanunulia wafanyakazi wenzake vinywaji huku akiwaasa kuhusu maisha...alikufa akiwa pekeyake chumbani
Hii ni sanaa ya kifo kamwe haikujulikana kabla..! Wale wafanyakazi wenzake wangekuwepo aliwazalo mwenzao kamwe wasingempa nafasi ya kutekeleza aliwazalo,na pengine wangemlinda na kumsihi a sifanyi hivyo au pengine wengine wangeomba wapige naye picha ya mwisho kama u kumbushio
Cha kushangaza yeye aliweza kujiandaa na kufanya yake aliyoyafanya lakini je ni wangapi ambao waliamua asubuhi wakiwa na mipango lukuki lakini kamwe hawakuweza kufika machweo???
Mitihani ni kwa ajili ya kufaulu! kufeli ni bahati mbaya. ... kwahiyo hata kwa hili tuwe tayari kwa imani zetu tukijua ya kuwa kwa hakika ipo siku saa na dakika tusiyoijua tutatwaliwa kutoka katika maisha haya ila kila mmoja wetu kwa style yake na stahili yake. Bila kujali maumivu yale ya mwisho, mwisho wa yote roho zetu zitaachana na miili yetu nasi tutaitwa marehemu
89194e6d9394cab64ad1dabb5a129a04.jpg
 
Mkuu Mshana jr,kwahiyo mtoto mchanga anae zaliwa nakufa, anakuwa amefaulu mtihani kwa haraka?.Vipi anae fariki ktk umri wa Miaka 90,je amechelewa kufaulu?.
Inasemekana siku hizi watu wanakufa angali bado vijana.Je hii inamaana siku hizi watu wanafaulu mtihani wa kifo mapema zaidi?,je hii maana yake kizazi hiki ni kizazi bora zaidi kuliko vizazi vilivyo pita?.
mtoto wa mjini hii kitu ni kama tu ilivyo kwenye elimu kuna maelfu ya watoto wala hawajawahi kuonja Ladha ya elimu walikufa mapema kabisa wengine hawakumaliza elimu zao za msingi wengine secondary basi na kwenye sanaa ya kifo ni vivyo hivyo
Hao wa miaka 90 na ushee ndio wale ma PhD
 
Back
Top Bottom