Chilemba wamela pamputi
JF-Expert Member
- Jan 10, 2019
- 468
- 486
Katika vitu ambavyo mimi sivikubali kama mwana CCM ni haya mambo ya hovyo yanayo jenga chuki zisizo na msingi kwa wananchi. Yaani ina maana kulikuwa hakuna uwezekano wa kuacha uchaguzi ufanyike kisha tupindue matokeo?
Na je, aliye shauri hili alifanya kwa maslahi ya nani? Kwakweli vitu vingine vina shangaza saana. Yaani tuananza kubomoa umoja tumeo ujenga kwa miaka mingi kwa sababu ya maslahi binafsi? Mbona tumekuwa na mawazo ya kinyama namna hii.
Ikumbukwe wakati sisi wana CCM tunafanya uchaguzi wa uteuzi kulikuwa na mambo mengi ya sinto fahamu kiasi cha kupelekea maeneo mengi watu kupigana hadi ngumi kwa sababu tu watu waliwekewa viongozi wasio wapenda na kuwahitaji. Kiukweli tulijeruhiana saana kwa vitendo vile.
Sasa pata picha ya kwamba sisi tulipo letewa mtu tusiye mkubali tuli gombana na kuumia kiasi kile kwa kubakwa kwa democrasia mpaka ikabidi maeneo mengi uchaguzi urudiwe. Maumivu tuliyo yapata sembuse hawa wenzetu wana maumivu ya moyo kiasi gani kwa jambo hili? Ni chuki kiasi gani imepandwa miyoyoni mwao?
Kama unaweza ukapima kiwango cha maumivu waliyo nayo baada ya kukataliwa kusiko jali uungwana na ustaarabu tulio uabudu kwa miaka mingi unaweza pia ukajuwa ni kwa kiasi gani hawa watu wameumia.
Lakini la mwisho, hiki kilicho tokea kita sababisha mnyukano wa ndani kwa ndani baadaye kwenye chama chetu maana wanachama wetu watafikiri kwamba ukigombea nafasi ukiwa ndani ya CCM basi unauhakika wa kwamba wewe nikiongizi moja kwa moja hivyo tutarajie haya:
1. Tutaanza sisi kwa sisi kumalizana ndani ya CCM kwasababu upinzani hauko tu nje ya CCM sababu na ndani ya CCM kuna upinzani tena mkali kuliko wa nje ya CCM. Na kwasababu upinzani utakuwa tu ndani ya CCM basi maisha yale ya wakati ule ya kufia kwenye vipaza sauti yatarudi kwa kasi sababu kila mtu atapigina maslahi yake ndani ya chama.
2. Hakutakuwepo mtu wa kuwanyamazisha wana CCM katika jambo lolote ndani ya CCM kwa sababu watu wote wataamini katika CCM kama chama cha maslahi ya wanachama na kwakuwa hakuna mwenye chama chamapinduzi hiki ni chama cha wote hivyo kila mtu ana haki ya kugombea .
3. Tunatengeneza CCM yenye visasi kwasababu madaraka ya kutawala yatakuwa yanatoka ndani ya chama kimoja , ni wazi kwamba leo ukinifanyia figisu mm wakati wewe ni kiongozi ndani ya CCM siku nikichukuwa na mm au jamaa yangu wa karibu tutakulipa kisasi wewe au watoto wako kadiri ya ulivyo tundea sisi.
Nashauri CCM ya sasa inawatu wengi wanafiki wanao piga kelele kwa kuwa wana maslahi ya moja kwa moja wao wanashinda wanapiga midomu alafu wana ishi kirahisi kwenye maviyoyozi wakati sisi tunashinda huku shamba na chama ni chetu wote na tuna uwezo wa kuongoza pia. Msingi mkubwa wa CCM toka inaanzishwa sio kushinda madaraka na kutawala tu lahasha.
Msingi ulikuwa ni kuwa fanya watu wawe huru wawe wamoja na kupitia uhuru wao na umoja waweze kusaidiana katika jamii wanamo ishi na kuji letea maendeleo kwa maslahi ya nchi yao.
Mfano ni huu, Mkuu wa Wilaya huishi Ikulu ndogo ya wilaya na ni mwana CCM mwenzangu. Nikiwa nashida mimi mwana CCM nisiye Mkuu wa Wilaya ninaishi huku mtaani na wanavyama wengine wa vyama vya siasa; tunaombana chumvi, tunazikana na panapotokea lolote tunashirikiana na huu ndiyo umoja ambao tumeupigania siku zote.
Sisis hatukatai ninyi kutawala na kula nchi wakati sisi tunasota huku mtaani nikwamba kuleni nchi lakini hakikisheni umoja na mshikamano wa taifa vinakuwepo kama ilivyo kuwa misingi ya kuanzishwa kwa CCM.
Na mwisho muheshimiwa raisi kuwa makini na hawa wanao kushauri wakati mwingine hawalitakii taifa letu mema. Wanaangalia miaka 5 ya ugali na mingine 5 ijayo ya ugali lakini CCM itaendelea kuwepo na tanzania itaendelea kuwepo tu umoja wetu na mshikamano uliojengwa na waasisi ni bora kuliko maslahi yao.
Wasaidie kama wana CCM Wenzako na wanapo kuja na shida binafsi kwako lakini usiwape nafasi kubwa saana ya kuwa sikiliza na kuufanyia kazi ushauri wanao utoa kwako ukigundua tu kwamba unakiuka misingi ya umoja uhuru na mshikamano wetu. Najuwa wewe siyo mwanasia kiasili sasa lazima utazungukwa na wanaojifanya wanzijuwa mbinu na chama vilivyo. Wasikudanganye hao.
Wengi wao watakupiga mateke siku ukitoka madarakani na watasahau yoye mema uliyo watendea watakusifu kwa nadra saana huku wakikutukana kana kwamba hujafanya kitu kwa nchi na kwao binafsi. Wengi wetu ndani ya chama huongozwa kwa upepo maslahi amini haya maneno yangu.
Mungu akubariki akupe na umri siku ukipumzika madarakani uje kuurejea uzii huu amina.
Chilemba.
Na je, aliye shauri hili alifanya kwa maslahi ya nani? Kwakweli vitu vingine vina shangaza saana. Yaani tuananza kubomoa umoja tumeo ujenga kwa miaka mingi kwa sababu ya maslahi binafsi? Mbona tumekuwa na mawazo ya kinyama namna hii.
Ikumbukwe wakati sisi wana CCM tunafanya uchaguzi wa uteuzi kulikuwa na mambo mengi ya sinto fahamu kiasi cha kupelekea maeneo mengi watu kupigana hadi ngumi kwa sababu tu watu waliwekewa viongozi wasio wapenda na kuwahitaji. Kiukweli tulijeruhiana saana kwa vitendo vile.
Sasa pata picha ya kwamba sisi tulipo letewa mtu tusiye mkubali tuli gombana na kuumia kiasi kile kwa kubakwa kwa democrasia mpaka ikabidi maeneo mengi uchaguzi urudiwe. Maumivu tuliyo yapata sembuse hawa wenzetu wana maumivu ya moyo kiasi gani kwa jambo hili? Ni chuki kiasi gani imepandwa miyoyoni mwao?
Kama unaweza ukapima kiwango cha maumivu waliyo nayo baada ya kukataliwa kusiko jali uungwana na ustaarabu tulio uabudu kwa miaka mingi unaweza pia ukajuwa ni kwa kiasi gani hawa watu wameumia.
Lakini la mwisho, hiki kilicho tokea kita sababisha mnyukano wa ndani kwa ndani baadaye kwenye chama chetu maana wanachama wetu watafikiri kwamba ukigombea nafasi ukiwa ndani ya CCM basi unauhakika wa kwamba wewe nikiongizi moja kwa moja hivyo tutarajie haya:
1. Tutaanza sisi kwa sisi kumalizana ndani ya CCM kwasababu upinzani hauko tu nje ya CCM sababu na ndani ya CCM kuna upinzani tena mkali kuliko wa nje ya CCM. Na kwasababu upinzani utakuwa tu ndani ya CCM basi maisha yale ya wakati ule ya kufia kwenye vipaza sauti yatarudi kwa kasi sababu kila mtu atapigina maslahi yake ndani ya chama.
2. Hakutakuwepo mtu wa kuwanyamazisha wana CCM katika jambo lolote ndani ya CCM kwa sababu watu wote wataamini katika CCM kama chama cha maslahi ya wanachama na kwakuwa hakuna mwenye chama chamapinduzi hiki ni chama cha wote hivyo kila mtu ana haki ya kugombea .
3. Tunatengeneza CCM yenye visasi kwasababu madaraka ya kutawala yatakuwa yanatoka ndani ya chama kimoja , ni wazi kwamba leo ukinifanyia figisu mm wakati wewe ni kiongozi ndani ya CCM siku nikichukuwa na mm au jamaa yangu wa karibu tutakulipa kisasi wewe au watoto wako kadiri ya ulivyo tundea sisi.
Nashauri CCM ya sasa inawatu wengi wanafiki wanao piga kelele kwa kuwa wana maslahi ya moja kwa moja wao wanashinda wanapiga midomu alafu wana ishi kirahisi kwenye maviyoyozi wakati sisi tunashinda huku shamba na chama ni chetu wote na tuna uwezo wa kuongoza pia. Msingi mkubwa wa CCM toka inaanzishwa sio kushinda madaraka na kutawala tu lahasha.
Msingi ulikuwa ni kuwa fanya watu wawe huru wawe wamoja na kupitia uhuru wao na umoja waweze kusaidiana katika jamii wanamo ishi na kuji letea maendeleo kwa maslahi ya nchi yao.
Mfano ni huu, Mkuu wa Wilaya huishi Ikulu ndogo ya wilaya na ni mwana CCM mwenzangu. Nikiwa nashida mimi mwana CCM nisiye Mkuu wa Wilaya ninaishi huku mtaani na wanavyama wengine wa vyama vya siasa; tunaombana chumvi, tunazikana na panapotokea lolote tunashirikiana na huu ndiyo umoja ambao tumeupigania siku zote.
Sisis hatukatai ninyi kutawala na kula nchi wakati sisi tunasota huku mtaani nikwamba kuleni nchi lakini hakikisheni umoja na mshikamano wa taifa vinakuwepo kama ilivyo kuwa misingi ya kuanzishwa kwa CCM.
Na mwisho muheshimiwa raisi kuwa makini na hawa wanao kushauri wakati mwingine hawalitakii taifa letu mema. Wanaangalia miaka 5 ya ugali na mingine 5 ijayo ya ugali lakini CCM itaendelea kuwepo na tanzania itaendelea kuwepo tu umoja wetu na mshikamano uliojengwa na waasisi ni bora kuliko maslahi yao.
Wasaidie kama wana CCM Wenzako na wanapo kuja na shida binafsi kwako lakini usiwape nafasi kubwa saana ya kuwa sikiliza na kuufanyia kazi ushauri wanao utoa kwako ukigundua tu kwamba unakiuka misingi ya umoja uhuru na mshikamano wetu. Najuwa wewe siyo mwanasia kiasili sasa lazima utazungukwa na wanaojifanya wanzijuwa mbinu na chama vilivyo. Wasikudanganye hao.
Wengi wao watakupiga mateke siku ukitoka madarakani na watasahau yoye mema uliyo watendea watakusifu kwa nadra saana huku wakikutukana kana kwamba hujafanya kitu kwa nchi na kwao binafsi. Wengi wetu ndani ya chama huongozwa kwa upepo maslahi amini haya maneno yangu.
Mungu akubariki akupe na umri siku ukipumzika madarakani uje kuurejea uzii huu amina.
Chilemba.