Vyama vya wafanyakazi fanyeni jitihada za kuwatetea wafanyakazi?

Mleta mada, kwa sifa ulizompelekea speaker wa bunge, hujawatendea haki mh Kasuku Bilago (marehemu), aliyekua mbunge wa Kakonko Kigoma, ambaye aliizungumzia hii hoja ya mafao mbele ya bunge lote na mwisho wa siku walio wengi ndani ya bunge walishinda kwa kuupitisha huo mswada ambao leo ni mwiba kwa mstaafu.

Mh Ester Bulaya mbunge wa Bunda mjini, ambaye ameliibua upya janga hili ambalo, kwa maneno ya Jenister Mhagama, limeanza kutumika tr 1 August mwaka huu. Hivi huyo speaker Ndugai sifa hizo anaanzaje kuzipata leo.

Kama ni wa kupata sifa, alitakiwa ni wakati ule mswada umepelekwa kwenye mhimili wake angeutendea haki kwa maslahi ya wastaafu. Leo baada ya kuona hali imekua mbaya, kelele kila kona, anaibuka na hilo aliloliongea, na wewe unaona huyo ndo msaada kwa wastaafu. Au kwakua hao wabunge wawili niliowataja hawatoki upande uupendao CCM???

Wabunge wa CCM ndiyo waliolifikisha hili hapa, na baada ya hizi kelele tunaanza kuwapa sifa.

Nimefuatilia sana jinsi ulivyowasilisha hoja yako, nimeshangaa sana kuona hujatoa acknowledgement yoyote kwa wabunge hao wawili. RIP mh Mwalimu Kasuku Bilago.
 
Sijaona mchango wa vyama vya wafanyakazi katika hii sheria kandamizi,inasikitisha sana,unashindwa kuelewa hivi vyama vinamwakilisha nani.Tuna safari ndefu sana ya kufika tulipopaswa kuwa baada ya miaka 57 baada ya uhuru!!spika mwongo na mnafiki ina maana ata yeye akujua kinachoendelea??Wastaafu wengi wanategemea pesa yao iwakomboe kimaisha.sasa hiyo 25% mtamsaidia nini mstaafu?eti nyingine kidogo kidogo,vipi umri wa mtanzania kuishi?
 
Kwa niaba ya Wafanyakazi wote Tanzania, nachukua fursa hii kumpongeza sana Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuona na kusikia kilio cha Wafanyakazi.

Niwaombe sasa Viongozi wa Vyana vya Wafanyakazi kutumia hii Momentum aliyoianzisha spika tuone matamko na kauli za kumuunga mkono spika.

Ukiisoma sheria ya kuunganisha mifuko, kama unazo akili ndogo za kutosha kutambua nyeupe na nyeusi basi hutapeleja lawama kwa wabunge pekee (ingawa bado wanalaumiwa kidogo) kwani utaona kila eneo lililotaja fao fulani, sheria inaeleza kuwa kanuni (kikokotoo) kitakuwepo kwenye kanuni zitakazotungwa na Waziri mwenye dhamana.

Pamoja na ukweli huo, niwaombe Viongozi wa vyama vya Wafanyakazi kuanzia Jumatatu muanze kutoa kauli za kumuunga mkono Spika na kueleza nini hasa hitaji la Wafanyakazi lakini pia mukiangalia mustakabali wa mifuko yenyewe ili isitokee wafanyakazi wakataka kulipwa kiasi kikubwa cha mafao huko mifuko ikishindwa hata kujiendesha na kudumu kwa vizazi vingine.

Ushauri wangu wa upande wa Serikali ni huu: Serikali yangu sikivu, huu ni muda muafaka wa Serikali (wataalamu) kukaa na wawakilishi na viongozi wa vyama vya wafanyakazi hasa vyama vya watumishi wale ambao hasa wameguswa na hizi kanuni ba kuweza kufanya actural valuation ya mifuko kwa pamoja na kuhakikisha wafanyakazi kupitia wawakilishi wao wanaelewa thamani hasa ya mali za mifuko na uwezo wa mifuko katika kujiendesha na kulipa mafao wastaafu waliopo na wanaokendelea kustaafu.

Hivi sasa Serikali hamueleweki kutokana na ukweli kwamba, haya mambo mumeyafanya sirini kana kwamba Wafanyakazi hawataelewa na wakielewa hawatapinga!!! That was very wrong!!! Kutana na wafanyakazi na ujadiliane nao na uhakikishe wameelewa na wanakuwa sehemu ya maamuzi mtakayofikia.

Namalizia kwa kumpongeza tena Mhe spika kwa maneno yake ya busara juu ya sakata hili na niwaombe tena viongozi wa vyama, mpeni Spika na wabunge ushirikiano na pia Jumatatu kila mmoja kwa staili yake toeni kauli za kumpongeza spika na wabunge na muwaombe wabunge hasa wa Chama Tawala walichukulie uzito suala hili kwani limegusa ndani sana katika mtima wa Mfanyakazi.

Nawasilisha
Penye ukweli uongo ujitenga!

Kama watawala walikopa katika mifuko ya hifadhi za jamii Sh8 trilioni, mpaka wakashindwa kulipa hilo deni, isiwe chanzo cha kuwakandamiza wastaafu!
Wafanyakazi wanataka utaratibu wa zamani utumike, mfanyakazi akiacha kazi anapewa stahiki zake, na kuondoka zake, atajua maisha yake mwenyewe!
 
Watanzania sana sana watumish na wastafu wanapata tabu sana awamu hii ya utawala
 
Watanzania sana sana watumish na wastafu wanapata tabu sana awamu hii ya utawala
 
Ongeeni kwa busara basi, na acheni kutumia maneno ya kejeri na dharau kwa viongozi.
Halafu sio wafanyakazi wote wanaoupinga huu mpango wa mafao.
Kumbuka hao pia wana haki yao ya kuupata huu mpango.
 
Hii kanuni ni lazima itarekebishwa tu hawana namna nyingine kwakuwa ni kandamizi mungu atasaidia
 
Vyama vya wafanyakazi wanaadaa nwanajiandaa kuita waandishi wa habari kusifia wabunge wa ccm kwa kutumia busara zao kupitisha sheria hii
 
Ongeeni kwa busara basi, na acheni kutumia maneno ya kejeri na dharau kwa viongozi.
Halafu sio wafanyakazi wote wanaoupinga huu mpango wa mafao.
Kumbuka hao pia wana haki yao ya kuupata huu mpango.
Hao ni mavi sio viongozi
 
Hata vikiwa vyama buku, vyote ni upuuzi mtupu, havina msaada kwa wafanyakazi zaidi ya unyonyaji
 
Aisee usicheke na mpumbavu anaeharibu ugali wako hasa baada ya 60+ ni zaidi ya hartari
 
Salaam TUCTA ukiwa mwavuli wa vyama vya wafanyakazi TALGWU, TUGHE, CWT, RAAWU, TUICO, nk

Salaam hizi nazituma kwenu nikiwa sehemu ya jamii ambayo kupitia makato ya 2% ya kila mwezi mnazichukua pasipo kutimiza wajibu wenu

Naomba kufahamu fedha mnazowakata wafanyakazi kila mwezi mnazitumia kufanyia shughuli ghani?

Je mlishirikishwa wakati wa kutunga sheria na kanuni mpya za mafao? endapo hamkushirikishwa kwanini mmekaa kimya katika hii sintofahamu na mkanganyiko wa kanuni mpya zenye lengo la unyonyaji kwa mfanyakazi maskini wa nchi hii??

Endapo mlishirikishwa tungependa kujua mlitoa mchango gani kwenye vikao? au mnaridhika na hali ilivyo sasa?

Mnaposema kwa mtumishi anayepokea 1,000,000 kwa mwezi aliyefanya kazi miaka 35 kwa kikokotoo cha zamani mkupuo anapokea 71,612,411 na mafao ya kila mwezi ni 371,847 halafu kwa kujisifu mnasema kikokotoo kipya mkupuo anapokea 35,806,205 na mafao ya mwezi ni 557,771 eti kuna ongezeko lakiasi cha 185,924 mnatumia vigezo gani?

Mbona hamtolei mfano mtumishi mwenye kima cha chini anapokea kiasi gani? Je endapo huyo mtumishi atafariki miaka 3 baada ya kistaafu na wategemezi wake kulipwa hiyo miaka 2 hicho kiasi kinachobaki mnakipeleka wapi?

Je mnadhani bado tunahitaji kuwa na vyama vya wafanyakazi ambavyo vipo kwa maslahi ya waajiri badala ya wafanyakazi wenyewe?

JITAFAKARINI SANA NA CHUKUENI HATUA KABLA HII FAMILIA YA WANUONGE HAIJAAMUA KUCHUKUA HATUA
Kuna suala hapa ambalo ni very technical! Unajua Wafanyakazi wa Tanzania wapo katika makundi mawili linapokuja suala la Mafao ya Uzeeni. Kuna wale waliopo katika Sekta binafsi ambao wanatumia mfuko wa NSSF na wapo Watumishi wa Umma.

Julai 2014 SSRA walileta kanuni mpya kwa mifuko yote na mbayo ndiyo sasa imerejeshwa tena ya 1/580, 12.5 na 25%. Kusema ukweli hali iliyokuwepo kwa Wanachama wa NSSF kabla ya ujio wa kanuni hizo ikikuwa mbaya kuliko neno lenyewe MBAYA!!! Yaani Mfanyakazi aliyetumikia Taifa lake kwa Miaka 30 na ambaye amestaafu akiwa na Mshahara wa Tsh. 1,000,000.00 alilipwa mafao ya Mkupuo kiasi cha Tsh. 12,600,000.00 na alipata malipo ya kila mwezi ya Tsh. 525,000.00

Baada ya kuanza kutumika kwa kanuni za mpya Julai 1, 2014 Wastaafu wa NSSF wakawa wanalipwa pensheni bora zaidi. Mfano huyu aliyekuwa amepokea Tsh 12,600,000 kama mafao ya Mkupuo analipwa Tsh. 23,275,862.07 sawa na ongezeko la 84.73%! na malipo ya kila Mwezi anapokea Tsh. 465,517.24 sawa na punguzo la 11.33% pekee ikilinganishwa na kanuni ya zamani!

Kwa maelezo hayo hapo juu, ni vyema Watanzania wote kukaelewa haya yafuatayo:

1. Haitowezekana Wafanyakazi wanachama wa mfuko wa NSSF wakaungana na wenzao wa Umma (Waliokuwa PSPF na LAPF) katika kupinga ujio wa hii kanuni mpya. Wao tayari ujio huu uliwatoa Jehanam na kuwafikisha Duniani. Sasa waungane na wenzao waliokuwa mbinguni na wanalalamikia kushushwa duniani!!!? Hiyo kiuhalisia haitawezekana!

2. Hata kama vyama vya Wafanyakazi ni bora kiasi gani, katika hali kama hii niliyoeleza katika Na. 1 hapo juu, hawataweza kupata sauti ya pamoja ya Wafanyakazi wa Tanzania.

3. Jambo kubwa hapa ni kuangalia ni namna gani Serikali itaweza kuelimisha Wafanyakazi wa Umma kwa kuwaeleza kwa uwazi sababu hasa za kuleta vikokotoo hivi kwenye scheme ya Utumishi wa umma na siyo vinginevyo!

Taifa kwa sasa linahitaji watu wenye busara sana kuweza kutuliza hali iliyopo kwa wafanyakazi kwani kila kona ya nchi wanaonekana (Watumishi wa Umma) wakiwa katika msononeko mkubwa na kuvitupia lawama vyama vyao. Hii haitasaidia, jambo la msingi ni Serikali irejee katika meza ya duara na Wawakilishi wa wafanyakazi au kujikita katika kutoa elimu ya sababu za uwepo wa Kanuni hizi ili wafanyakazi waondokane na mawazo waliyonayo hivi sasa na waelewe kuwa pamoja na kupunguzwa kwa % ya malipo ya mkupuo, lkn Serikali inayo sababu za msingi za kutaka kukuza mfumo endelevu wa hifadhi hasa wakati huu ambao tayari viashiria vilishaonesha kuwa PSPF na LAPF zilikaribia kufa.

Ni vyema wafanyakazi tukaacha mihemko na hasira zinazochanganyika na hisia za kisiasa na kuangalia dhamira ya Serikali kabla ya kulaumh kwa hili lililotokea.
 
Kuna suala hapa ambalo ni very technical! Unajua Wafanyakazi wa Tanzania wapo katika makundi mawili linapokuja suala la Mafao ya Uzeeni. Kuna wale waliopo katika Sekta binafsi ambao wanatumia mfuko wa NSSF na wapo Watumishi wa Umma.

Julai 2014 SSRA walileta kanuni mpya kwa mifuko yote na mbayo ndiyo sasa imerejeshwa tena ya 1/580, 12.5 na 25%. Kusema ukweli hali iliyokuwepo kwa Wanachama wa NSSF kabla ya ujio wa kanuni hizo ikikuwa mbaya kuliko neno lenyewe MBAYA!!! Yaani Mfanyakazi aliyetumikia Taifa lake kwa Miaka 30 na ambaye amestaafu akiwa na Mshahara wa Tsh. 1,000,000.00 alilipwa mafao ya Mkupuo kiasi cha Tsh. 12,600,000.00 na alipata malipo ya kila mwezi ya Tsh. 525,000.00

Baada ya kuanza kutumika kwa kanuni za mpya Julai 1, 2014 Wastaafu wa NSSF wakawa wanalipwa pensheni bora zaidi. Mfano huyu aliyekuwa amepokea Tsh 12,600,000 kama mafao ya Mkupuo analipwa Tsh. 23,275,862.07 sawa na ongezeko la 84.73%! na malipo ya kila Mwezi anapokea Tsh. 465,517.24 sawa na punguzo la 11.33% pekee ikilinganishwa na kanuni ya zamani!

Kwa maelezo hayo hapo juu, ni vyema Watanzania wote kukaelewa haya yafuatayo:

1. Haitowezekana Wafanyakazi wanachama wa mfuko wa NSSF wakaungana na wenzao wa Umma (Waliokuwa PSPF na LAPF) katika kupinga ujio wa hii kanuni mpya. Wao tayari ujio huu uliwatoa Jehanam na kuwafikisha Duniani. Sasa waungane na wenzao waliokuwa mbinguni na wanalalamikia kushushwa duniani!!!? Hiyo kiuhalisia haitawezekana!

2. Hata kama vyama vya Wafanyakazi ni bora kiasi gani, katika hali kama hii niliyoeleza katika Na. 1 hapo juu, hawataweza kupata sauti ya pamoja ya Wafanyakazi wa Tanzania.

3. Jambo kubwa hapa ni kuangalia ni namna gani Serikali itaweza kuelimisha Wafanyakazi wa Umma kwa kuwaeleza kwa uwazi sababu hasa za kuleta vikokotoo hivi kwenye scheme ya Utumishi wa umma na siyo vinginevyo!

Taifa kwa sasa linahitaji watu wenye busara sana kuweza kutuliza hali iliyopo kwa wafanyakazi kwani kila kona ya nchi wanaonekana (Watumishi wa Umma) wakiwa katika msononeko mkubwa na kuvitupia lawama vyama vyao. Hii haitasaidia, jambo la msingi ni Serikali irejee katika meza ya duara na Wawakilishi wa wafanyakazi au kujikita katika kutoa elimu ya sababu za uwepo wa Kanuni hizi ili wafanyakazi waondokane na mawazo waliyonayo hivi sasa na waelewe kuwa pamoja na kupunguzwa kwa % ya malipo ya mkupuo, lkn Serikali inayo sababu za msingi za kutaka kukuza mfumo endelevu wa hifadhi hasa wakati huu ambao tayari viashiria vilishaonesha kuwa PSPF na LAPF zilikaribia kufa.

Ni vyema wafanyakazi tukaacha mihemko na hasira zinazochanganyika na hisia za kisiasa na kuangalia dhamira ya Serikali kabla ya kulaumh kwa hili lililotokea.
Nawewe ni wale wale wa Lumumba...mtu kama kaitumikia serikari takribani miaka 30 na mzigo wake maximum ni 80 au 90 million apewe yote....huu ni udictator wa live wa kupora fedha za wastafu..hii haikubaliki mzee serikari yako haina nia njema kabisa na wastafu
 
Haya ni matakataka ya kufagia na kuchoma. Hayana msaada. Serikalini hawawezi sema chochote. Kwa wahindi wanachukua hela wanakaa kimya.
Wafanyakazi wanalalamika kila kona.
 
Yani wewe unampa sifa spika peke yake na kusahau Bulaya yani mtu akiwa na mahaba upende mmoja hata jambo jema litokee upande wa Pili atalipuuza
 
inaniumiza sana viongozi tuliowachagua wamekaa kimya wakati serikali ikiwapora watumishi wake penshen wasiostahili.. hivi hakuna hata kukeme au kuilaani kinachoendela hakuna. wote wamekaa kimya. kuna haja gani ya kuwa na vyama vya wafanyakazi tz?
unastaafu badala ya kupewa penshen ya 100% badala yake unapewa 25%? kemeeni hili jambo itisheni midahalo, haya ni machungu yanayotupata
 
inaniumiza sana viongozi tuliowachagua wamekaa kimya wakati serikali ikiwapora watumishi wake penshen wasiostahili.. hivi hakuna hata kukeme au kuilaani kinachoendela hakuna. wote wamekaa kimya. kuna haja gani ya kuwa na vyama vya wafanyakazi tz?
unastaafu badala ya kupewa penshen ya 100% badala yake unapewa 25%? kemeeni hili jambo itisheni midahalo, haya ni machungu yanayotupata
Wanaogopa kuitwa ikuluni
 
Back
Top Bottom