JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

JF Prefixes:

Kuna picha nimeona Rais Mstaafu wa Marekani, Barack Obama akizindua uidhinishaji wake wa mwisho wa mgombea urais 2022 nchini Kenya ambapo alionesha wazi kumuunga mkono Naibu Rais Ndugu William Ruto. Barack Obama ana vinasaba vya Ujaluo, sijui ilikuwa vipi akashindwa kumuunga mkono Mjaluo mwenzio Mwamba Raila Amolo Odinga. Chanzo: BBC === Video halisi iliyotumika kutengeneza picha hiyo
Leo nimesoma mtandaoni kuwa Vidonda vya tumbo(Ulcers) huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Naomba kujua kama ni kweli maana siku zote mie najua vidonda vya tumbo huvipata mtu kutokana na mtindo wake wa maisha(kutokula) au kwa kutumia baadhi ya dawa ambazo zinaweza kuchubua utumbo. Sasa hii ya kuambukiza kwangu imekuwa mpya sana, tena mwandishi alifafanua zaidi kuwa eti iwapo mwenza wako ana ulcers basi uwezekano wa wewe kuupata ni mkubwa maana anaweza kukuambukiza.
Uhakiki wa Picha kwa kutumia Google Image Search ni njia muhimu ya kubaini asili au maelezo zaidi kuhusu picha fulani. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha 1. Tembelea Google Image Search Fungua kivinjari chako na nenda kwenye ukurasa wa Google. Bonyeza kwenye sehemu ya 'Images' au 'Picha' kwenye ukurasa wa kwanza wa Google, au ingiza 'Google Image Search' moja kwa moja kwenye sanduku la utafutaji wa Kifaa chako 2. Ingiza Picha Kuna njia kadhaa za kuingiza picha kwenye Google Image Search: Bonyeza kitufe cha kamera kilichopo kwenye sanduku la utafutaji ili kuwezesha utafutaji wa picha kwa kutumia kamera. Kama picha unayo kwenye kifaa chako, unaweza kuiweka moja...
Mara nyingi nikiwa na stress na kupelekea kukosa usingizi, huwa navuta sigara ili kupunguza stress hizo. Hata iwe usiku wa manane nitajitahidi niende kwenye Club zinazokesha nikafuate sigara. Suala la kuwa inanisaidia au lah, sidhani lakini pale napokuwa navuta huwa nakuwa katika hisia nyingine kabisa. Chanzo cha kutumia sigara kama relief ya stress, ni baada ya kuona kwenye muvi mara kwa mara, na ushauri kutoka kwa marafiki. Nachotaka kujua kitaalam ni kama kweli sigara inasaidia kupambana na msongo wa mawazo tunaokumbana nao mara kwa mara.
Baada ya Afrika, bara la Amerika Kusini ndilo lenye watu weusi wengi zaidi wakikadiriwa kuwa zaidi ya milioni 170 huku Brazil ikiongoza ikiwa na watu weusi takriban milioni 120. Nchi ya Argentina inatajwa kuwa mpaka sasa watu weusi ni chini ya laki mbili wakiwa takriban asilimia 0.5% kutoka asilimia 48% miaka ya 1800. Inadaiwa watu weusi baada ya kuisaidia Argentina kupigana vita na maadui zake, watu weusi waliosalia waliwekwa kwenye maeneo maalumu ambayo kwa kipindi hicho kulikuwa na ugonjwa wa hatari unaosababishwa na bacteria “Plague” ambapo serikali iliwanyimwa huduma muhimu hivyo upelekea vifo vyao. Zitto kupitia ukurasa wake wa Twiiter aliwahi kumhoji jamaa kuhusu kuishabikia Argentina, nanukuu 'Una support argentina ambayo...
Kumekuwepo na barua inayiosambaa Mtandaoni ikionesha kuandikwa na Mfalme Mswati III ametoa tangazo linalodai kuwa kutokana na uhaba wa Wanaume kwenye nchi yake, amewaomba wananchi wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara kuomba uraia kwenye nchi yake, na kila mwanaume atayeoa walau wanakwake 5 atamlipia gharama za harusi zao pamoja na kuwanunulia nyumba. Ukweli wa taarifa hii upoje?
Katika pitapita mitandaoni nimekutana na huyu chawa wa Mtoto wa Rais Museveni, Kainerugaba Muhoozi akimtuhumu Kakwenza Rukira kuingia makubaliano ya siri na umoja wa Ulaya nchini Uganda katika kuhamasisha ushoga nchini humo. Nakumbuka Uganda imezuia mahusiano ya jinsia moja na Rais Museveni amebana kweli kweli wazungu hawana pa kupumulia, naona wameamua kupitia njia za panya kuleta ushenzi wao.
TinEye ni nyenzo nzuri ya kutafuta picha kwenye wavuti ambayo inaweza kutumiwa kufanya uhakiki wa Picha. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha. 1. Fungua Kivinjari Chako Anza kwa kufungua kivinjari chako kwenye kifaa chako cha mkononi au kompyuta. 2. Tembelea Tovuti ya TinEye Ingiza 'TinEye' kwenye sanduku la utaftaji la kivinjari chako na bonyeza kwenye matokeo yanayofanana na tovuti rasmi ya TinEye. 3. Pakia Picha Kuna njia mbili za kupakia picha kwenye tovuti ya TinEye Bofya kwenye kitufe cha 'Pakia Picha' au "Upload' kisha pakia picha unayotaka kufanya uhakiki. Ikiwa picha tayari iko kwenye wavuti, unaweza kunakili URL (Link) ya picha hiyo na kuibandika...
Yandex ni njia nyingine ya utafutaji inayotumika sana kufanya uhakiki wa picha. JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha. 1. Fungua Kivinjari Chako Anza kwa kufungua kivinjari chako kwenye kifaa chako cha mkononi au kompyuta. 2. Tembelea Tovuti ya Yandex Ingiza 'Yandex' kwenye sanduku la utafutaji la kivinjari chako na bonyeza kwenye matokeo yanayofanana na tovuti rasmi ya Yandex. 3. Pakia Picha Kuna njia mbili za kupakia picha kwenye tovuti ya Yandex Bofya kwenye alama ya kamera iliyo kwenye sanduku la utaftaji la Yandex na chagua 'Pakia Picha' au 'Upload' kisha upakie picha unayotaka kufanya uhakiki. Ikiwa picha tayari iko kwenye wavuti, unaweza kunakili URL...
Baada ya kauli ya CDF wa Tanzania Jenerali Mkunda kusema kuwa 'Baadhi ya Wakimbizi wamepewa teuzi Serikalini katika nafasi zenye maamuzi' imenifikirisha sana nikakumbuka nilishawahi kusikia tetesi kuwa Paul Kagame wakati akiwa mkimbizi nchini Uganda, aliwahi kuhudumu kwenye jeshi la nchi hiyo na mpaka kufikia cheo cha Mkuu wa usalama wa Jeshi Uganda. Mpaka sasa tunaona jinsi Kagame anavyoisumbua Uganda labda kutokana na ukweli kuwa anaijua nje ndani. Je, ni kweli Paul Kagame aliweza kuaminiwa na kupewa cheo nyeti kwenye Jeshi la Uganda?
Matamshi ya chuki yaweza kuwa maneno au vitendo vinavyoonyesha hisia za uadui, dhihaka, au kutokuwajali kuelekea mtu au kundi fulani. Yanaweza kujitokeza kwa misingi ya tofauti za kijamii, kitamaduni, kidini, kisiasa, au mambo mengine. Chuki inafarakanisha makundi, huchangia vurugu na migogoro, na hudhoofisha jitihada zetu zote za amani, utulivu na maendeleo endelevu. Hata hivyo, sasa ukubwa na athari yake umesambazwa zaidi na teknolojia mpya za mawasiliano ambayo sasa yanawafikia watu wengi sana kwa haraka sana. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres anasema "Tunahitaji kuchukulia hotuba za chuki kama tunavyochukulia vitendo vyovyote vibaya: kwa kuzilaani, kutoziendeleza, kukabiliana nazo na ukweli na kuchagiza...
Habari wakuu, Nimeona taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki imetambulisha noti yake itakayotumika katika nchi wanachama, iliyopewa jina la SHEAFRA (SHF). Wengi wameinukuu akaunti kutoka mtandao wa X (zamani Twitter) inayojulikana Government of East Africa Moja ya chombo kikubwa kilichoinukuu akaunti hiyo ni pamoja na ITV , binafsi bado nina mashaka na hii taarifa kutokana na kwamba akaunti maalum ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ninayoifahamu siyo hii. Ukweli ni upi?
Habari Wadau, Nimekutana na tangazo la kazi likionesha kuwa Kampuni ya usafirishaji ya Tilisho inahitaji Wafanyakazi kwa nafasi ya Wakatisha Tiketi na wahudumu wa ndani ya Mabasi. Nimepata mashaka baada ya kuona ukilifuata tangazo hili ndani yake linahitaji usambaze link kwenye magroup ya WhatsApp na Facebook ili kuendelea hatua inayofuata. Je, kuna ukweli juu ya Tangazo hili?
Kuna dada zetu wanapenda sana urembo hivyo kujiongezea baadhi ya vitu kama matako, kope, lenzi kwenye macho, matiti vimekuwa vitu vya kawaida sana kwao. Ukweli hayo yote wanayojiongea yanakuwa na madhara. Mimi nipende tu kutoa hadhari kuwa kope na lenzi bandia mnavyojiongezea ni hatari kwa afya ya macho yenu. Chonde chonde ridhikeni na mlivyoumbwa navyo. Khadija Omary ni mmoja wa wahanga wa kupofuka baada ya kuwekewa kope bandia. Ni hayo tu.
Back
Top Bottom