Leo nimeona video ambao imewekewa sauti ya mtu akisema wametumiwa video hiyo kwenye group la shule ya Themihill, video hiyo inaonesha mtu akifungua kitu kinachoonekana kama pen (kalamu) ambacho ndani yake kina risasi na baadaye kufyatuliwa.
Anayeelezea video hiyo anadai pen hizo zinagawiwa mashuleni na kuuzwa huku akionesha hofu ya watoto kuuana au wao wenyewe kujidhuru kwa peni hizo.
Ningependa kufahamu ukweli kuhusu video hiyo.
Salaam,
Nimesikia mtaani wanawake wanaambiana kuwa Kunywa maji ya Baridi wakati wa Ujauzito husababisha kupata mtoto mwenye matatizo ya kifua. Nimeogopa kidogo maana mdogo wangu ana mimba na anapenda sana kunywa maji ya baridi.
JamiiCheck tuaidieni kuhakiki hii.
Nimerudi tena kwenu wataalamu wa JamiiCheck,
Eti ni kweli mtu akikung'ata wakati akiwa na hasira basi anatengeneza sumu kama vilivyokuwa kwa wanyama (kama nyoka) na hivyo inaweza hata kukuua, kwa kutegemeana na jinsi hasira yake ilivyo kali?
Hii ni kweli wataalam?
Wakuu,
Nimekuja na swali hili baada ya jamaa mmoja kusema jambo hili sio la kweli, lakini mimi pia nimeshawahi sikia hii, bi mkubwa alituhadisia kuna ndugu yao mmoja aling'atwa na mbwa mwishowe alipokaribia kwenda kwenye ulimwengu mwingine alikuwa akibweka kama mbwa. Naamini hata wewe unayesoma hapa umeshawahi kusikia kuhusu hili.
Je, suala hili ni kweli au stori tu za mtaani wataalamu wa JamiiCheck?
Wakuu,
Kuna video nilikutana nayo huko mtandaoni (nimeangalia sijaiona), huyo dada alikuwa anasimulia jinsi rafiki yake alivyokufa baada ya kung'atwa chura. Chura huyo alikuwa ndani ya kiatu chake, wakati anavaa hakumuona, basi huyo chura akamng'ata kwenye kidole baada ya kushtuka (unajua jinsi wadada tunaogopa wadudu) akamtoa kwenye kiatu na kuvaa na kuendelea na kazi zake.
Baada ya siku mbili yule dada akaumwa, homa kali ikamshika kumpeleka hospitali ndio ikaonekana ni hiyo sumu ya chura, na imeshambaa mwilini kiasi ambacho hakuna msaada tena. Mwisho dada alikuwa anakoroma kama chura (kama vile inavyotokea mtu aking'atwa na mbwa mwenye kichaa) mwishowe akafa.
Sasa wakuu mimi nauliza, hawa chura tunaopishana nao majumbani ndio...
Habar JamiiCheck,
Mimi ni mjamzito, nimekuwa nasikia kuwa ulaji wa pilipili wakati wa Ujauzito kunafanya mtoto kuzaliwa na macho mekundu.
Nisaidieni kuhakiki hii maana napenda sana kula pilipili lakini naogopa mwanangu kuzaliwa na macho mekundu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.